Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Dar es Salaam

Na Mwandishi wetu

Paroko Msaidizi wa Paroki ya Mtakatifu Rita wa Kashia -Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Kanuti Martin Nyoni, amewataka Waamini waendelee kusali na kumuomba Mwenyezi Mungu, ili Taifa liendelee kuwa na viongozi waadilifu, wenye kusikia sauti yake Mwenyezi Mungu, katika kuwalinda na kuwaongoza raia.
Padri Nyoni alitoa wito huo hivi karibuni, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu, ya kuwaombea Watu wote waliouawa na kujeruhiwa, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu iliyofanyika parokiani hapo.

Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu, amewataka Waamini kumshukuru Mungu kwa kila jambo, kwani yeye ndiye muweza wa yote. 
Askofu Mchamungu alitoa wito huo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, iliyokwenda sanjari na kutoa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara Kwa vijana 31, iliyofanyika Parokia ya Mtakatifu Yohane Paulo II, Miembesaba-Kibaha jimboni humo. 

Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu

Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), imewatembelea wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mbwenitete jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Sayansi Duniani, kwa lengo la kuwahamasisha vijana hao kujikita katika ubunifu na matumizi ya sayansi, katika kutatua changamoto za kijamii.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Mratibu Mkuu wa Tafiti na Bunifu kutoka COSTECH, Dkt. Prosper Masawe, amesema kuwa amevutiwa na ubunifu mbalimbali uliooneshwa na wanafunzi wa shule hiyo, ambao unaonesha uwezo mkubwa wa kubuni suluhu za changamoto katika jamii.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Mhifadhi Mwandamizi wa Makumbusho ya Taifa (NMT), Sechelela Magoile, amesema kuwa matumizi ya teknolojia yanapaswa kuiakisi jamii, na kuwawezesha Wananchi kupata taarifa sahihi, kuhusu maendeleo ya kisayansi, kukuza uelewa na kuweka jamii salama.
Alisema hayo katika kuadhimisha Siku ya Sayansi Duniani, iliyofanyika katika Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam.

Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu

Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA), kinalaani vurugu, mauaji na uharibifu wa mali, vilivyotokea wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Chama hicho pia kimetoa pole kwa wote waliopoteza ndugu au mali, na kuunga mkono  agizo la Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, la kufanya uchunguzi wa kina, na kuwawajibisha wahusika wote kwa mujibu wa sheria.

Dar Es Salaam

Na Mwandishi Wetu

Katika kuadhimisha Wiki ya Magonjwa Yasiyoambukiza, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), imezindua rasmi kitengo kipya cha kusafisha damu (dialysis unit), kwa wagonjwa wa moyo wanaopata matatizo ya figo, hatua inayolenga kuboresha huduma za tiba jumuishi kwa wagonjwa hao.
Kitengo hicho chenye mashine za kisasa, zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200, kimeanza kutoa huduma mara moja baada ya kuzinduliwa, kikiwa na uwezo wa kusafisha damu kwa zaidi ya wagonjwa nane kwa siku.

Mbeya

Na Mwandishi wetu

Maaskofu wa Majimbo mbalimbali ya Kanisa Katoliki nchini, wameadhimisha Misa Takatifu za kuwaombea watu waliouawa na kujeruhiwa, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu, huku wakitoa kauli tofauti tofauti na kukemea, kuhusu hali ya uvunjifu wa amani iliyotokea wakati wa uchaguzi huo.

Dar es Salaam

Na Mwandishi wetu

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi OFMCap, amesema kuwa hakuna amani bila haki, kwani haki ni msingi wa lazima wa amani.
Askofu Mkuu Ruwa’ichi alisema hayo katika Adhimisho la Misa Takatifu, ya Kuwaombea watu waliouawa katika wiki ya Uchaguzi Mkuu Tanzania, iliyoadhimishwa hivi karibuni, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu, jimboni humo.

Dar es Salaam

Na Laura Mwakalunde

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewaonya Waamini kutoruhusu wao kuwa karakana ya shetani.
Alisema hayo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya uzinduzi wa nyumba ya Mapadri, iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Consolatha-Mbezi Makabe.
“Kila Mkristo inampasa kuwa na maamuzi kwa kuachana na mambo ya kale, aibu ya giza, kwani inasikitisha kuona Mkristo anakwambia bado kidogo,” alisema Askofu Mkuu Ruwa’ichi.
Aidha, aliwataka Waamini watambue kuwa wao ni warumi wa leo, kwa sababu Mtume Paulo huwa anafundisha ukweli wa mambo ya kale, ya aibu na ya giza, kwa kutoruhusu akili na utashi wao kuwa kichaka cha dhambi.

Same

Na Mathayo Kijazi

Kutokana na kuwepo kwa matukio ya ajali za barabarani za mara kwa mara, Askofu wa Jimbo Katoliki la Same, Mhashamu Rogath Kimario, ameandaa mkakati wa kujenga Groto ya Bikira Maria Mwombezi wa Wasafiri, kando ya barabara katika eneo la Maligo jimboni humo, ili kusaidia kuzuia ajali hizo.
Askofu Kimario aliyasema hayo hivi karibuni, ambapo alibainisha kuwa eneo hilo mara nyingi hutumiwa na wasafiri, kama sehemu ya huduma za maliwato, hivyo ni vema kujenga Groto hiyo ili wasafiri wapate huduma za kiroho, ikiwemo kuombea safari zao.
Aliongeza kuwa wanafanya hivyo ikiwa pia ni sehemu ya maandalizi, kuelekea katika Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 50, tangu Same ilipotangazwa kuwa Jimbo Katoliki, ambayo kilele chake ni Februari 3, 2027, hivyo katika kamati yao ya maandalizi, wameona ni vema kujenga Groto hiyo ya Bikira Maria Mwombezi wa Wasafiri.

Page 1 of 56