Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Abate Christian Temu –OSB wa Abasia ya Ndanda, Jimbo Katoliki la Mtwara, amesema kuwa maisha ya Mkristo ni kama Hija, kwani kila wakati anakuwa safarini kuelekea mbinguni kwa Mwenyezi Mungu.
Aidha, Abate Temu amewasihi Wakristo kutoogopa jambo lolote, akiwasihi kuwa majasiri kwani Mungu yupo nao, na masuala ya amani na haki ni matunda ya Kimungu.
Abate Temu alitoboa siri hiyo hivi karibuni katika homilia yake, katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kufunga Jubilei ya Miaka 2025 ya Ukristo, iliyoadhimishwa katika Kituo cha Hija - Pugu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.

DAR ES SALAAM

Na Angela Kibwana

Zaidi ya shilingi milioni 200, zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa nyumba ya Padri, katika Parokia mpya ya Bikira Maria wa Rozari-Msomwero, jimboni Morogoro, ambayo itakuwa ni hatua muhimu ya kukamilisha makazi ya Padri, anayefanya utume parokiani hapo, kwa lengo la kusogeza huduma  za kiroho kwa Waamini.
Akizungumza kwa mahojiano maalumu, Paroko wa Parokia hiyo Padri Chediel Mloka, amebainisha kuwa parokia hiyo mpya ilitangazwa miaka mitatu iliyopita, na Askofu Lazarus Vitalis Msimbe SDS, wa Jimbo Katoliki Morogoro, ili kunusuru imani za Waamini ambao walikuwa wanapata huduma za kiroho, katika Parokia ya Ilonga.
Alisema kuwa kwa sasa wakati anaendelea kusubiri kukamilika kwa nyumba hiyo, anaishi nyumba ya kupanga umbali wa Kilomita nne toka yalipo makazi hayo, hadi kufika kanisani hapo.

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Wakristo wamesisitizwa kuwa wanakanisa halisi, hasa katika zama hizi zenye ugeugeu na ubabaishaji mwingi, ili waendelee kuwa na roho zenye uadilifu na uungwana.
Kauli hiyo ilitolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 25, ya Parokia ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili - Mavurunza, jimboni humo.

Na Mwandishi Wetu

Katika makala haya kuhusu Ubatizo wa Bwana, Mwadhama Protace Kardinali Rugambwa katika mahubiri yake, ametumia fursa hii kufafanua alama muhimu, zilizojionesha wakati Kristo Yesu alipobatizwa mtoni Yordani.

Anasema kwamba alama ya kwanza ni Maji: Alama ya kifo na uhai; Mbingu zikamfunukia, Roho Mtakatifu akashuka juu yake kama hua; Alama ya pili ni kufunguka kwa mbingu; Alama ya mabadiliko ya ndani ya mwanadamu, mbele ya Mwenyezi Mungu; Alama ya tatu ni Roho Mtakatifu aliyemshukia Kristo Yesu na sauti ya Baba wa milele ikasikika: Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu.

Ubatizo ni sakramenti inayotuingiza katika Ukristo, ni sakramenti inayotuondolea dhambi ya asili na adhabu zake zote. Ni kwa njia ya Ubatizo tunazaliwa upya kwa maji na Roho Mtakatifu, na hivyo tunakuwa ni watoto wa Mungu na wa Kanisa.

DAR ES SALAAM

Arone Mpanduka

Michel Kuka Mboladinga, ambaye pia anajulikana kama Michel Kuka, Michel Nkuka, au kwa jina la utani “Lumumba” na “Lumumba Vea”, ni shabiki wa soka wa timu ya taifa ya DR Congo, anayejulikana kwa tabia yake ya kipekee, wakati wa mechi za timu ya taifa ya kandanda ya DR Congo. 
Amekuwa shabiki kindakindaki wa taifa la Congo tangu mwaka 2013, ambapo amekuwa akisimama jukwaani bila kutikisika katika michezo yote. Amekuwa akiiga mkao wa sanamu ya mwanasiasa wa zamani na mkombozi wa taifa hilo, Patrice Lumumba mjini Kinshasa.
Jamaa huyu amejizolea umaarufu zaidi kwa vyombo vya habari vya kimataifa, wakati wa Kombe la Mataifa ya Afrika la 2025, nchini Morocco. 

London, Uingereza
Kiungo wa kati wa Tottenham, Rodrigo Bentancur, anahitaji upasuaji wa misuli ya paja, na anatarajiwa kukosa angalau miezi mitatu.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay, ambaye amekuwa mchezaji muhimu kwa timu ya Thomas Frank msimu huu, alipata jeraha hilo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Spurs dhidi ya Bournemouth wiki iliyopita.

London, Uingereza
Mshindi wa fainali wa zamani wa Wimbledon, Milos Raonic, alisema kwamba amekuwa mtu mwenye bahati zaidi kutimiza ndoto zake, alipotangaza kustaafu kutoka tenisi.
Mkanada huyo mwenye umri wa miaka 35, alimshinda Roger Federer na kufikia shindano la Wimbledon mwaka wa 2016, ambapo alishindwa moja kwa moja na Andy Murray wa Uingereza.
Raonic, ambaye alishinda mataji nane ya ngazi ya ziara, alifikia kiwango cha juu cha dunia cha tatu mwaka huo huo, baada ya pia kufika nusu fainali ya Australian Open.

DAR ES SALAAM

Na Nicolaus Kilowoko

Kocha Mkuu wa klabu ya soka ya Simba, raia wa Afrika Kusini Steven Barker, baada ya kuiongoza klabu hiyo kwenye michezo mitatu ya michuano ya Mapinduzi Cup 2026, ametoa maagizo kwa uongozi wa klabu hiyo, kusajili wachezaji wanne kwenye dirisha dogo la mwezi Januari.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Shirikisho la ngumi Tanzania (BFT), limeandaa mikakati ya kumleta bondia maarufu duniani, Manny Pacquiao, nchini Tanzania, kwa ajili ya mashindano ya semi Pro fights ya BFT.
Lengo la BFT kumleta Pacquiao nchini Tanzania, ni kwa ajili ya uzinduzi wa mashindano hayo, pia atashiriki matukio ya kijamii ya kuinua mchezo wa ngumi hapa nchini.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Klabu ya Singida Black Stars, imesema kuwa haina ukaribu wala urafiki wowote na klabu ya Yanga, hasa kwenye kupeana wachezaji na kupeana matokeo, kama watu wanavyodai.
Singida imeyasema hayo, wakati wimbi la kuuziana na kupeana wachezaji wa mkopo likishamiri, katika kila dirisha la usajili hapa nchini.
Katika dirisha dogo la sasa la usajili, Singida iliwatoa kwa mkopo wachezaji Mohammed Damaro na Marouf Tchakei kwenda Yanga, huku Yanga ikimtoa Mamadou Doumbia kwa mkopo kwenda Singida, jambo ambalo wadau wa soka wakalazimika kuweka hadharani shaka yao, kuhusiana na timu hizo mbili.

Page 1 of 61