Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme, Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Cornel Mashare (kushoto), na Mwenyekiti wa Parokia hiyo, Frederick Akilimali, wakionesha cheti cha shukrani kutoka kwa Askofu Mkuu wa Jimbo hilo, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi kwa kufanya vizuri katika kuitegemeza Tumaini Media mwaka 2023.

Mgeni rasmi katika Mahafali ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi Golden’light, jijini Dar es Salaam, John  Magwisha (kulia), akikabidhi zawadi kwa Gladness Jonathan (kushoto),  mmoja wa Waalimu wa shule hiiyo, wakati wa sherehe za Mahafali hayo zilizofanyika shuleni hapo. (Picha na Yohana Kasosi)

Baadhi ya Waamini wa Parokia ya Kung’ara kwa Yesu Kristo, Mbezi Mshikamano, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha na Yohana Kasosi)

Masista wanaofanya kazi za kitume kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Mahafali ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi ya Golden’light, Mbezi Mpigi Magohe, jijini Der es Salaam. (Picha na Yohana Kasosi)

Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari – Bombambili, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Sheejan Kallarakkal MSFS (mwenye kanzu nyeupe), akiwa katika picha ya pamoja na Wazee na Wastaafu, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Shukrani kwa Mungu kwa Wazee na Wastaafu wa Dekania ya Pugu, iliyoadhimishwa katika Parokia ya Bombambili. (Picha na Mathayo Kijazi)

Padri Dickson Sambala- O.CARM, akibariki vipaji wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu iliyofanyika Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli, Bunju, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, iliyofanyika parokiani hapo. (Picha na Yohana Kasosi)

Baadhi ya Waamini wa Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kuhitimisha Ziara ya Kuitembeza Sanamu ya Bikira Maria wa Fatima, iliyofanyika Parokia ya Mtakatifu Vincent wa Paulo, Vikindu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, na baadaye waliikabidhi kwa Jimbo Katoliki la Lindi. (Picha na Yohana Kasosi)

Mdau wa Tumaini Media, Anitha Kihwele na mumewe Joseph Kihwele, wakitabasamu baada ya kukabidhiwa cheti cha shukrani na Padri Cornel Mashare (kushoto), Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme, Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, kutokana na mchango wa Mama Kihwele katika kuhamasisha majitoleo ya tegemeza Tumaini Media. Cheti hicho kimetolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo hilo, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi. Nyuma yao ni Meneja Utawala Tumaini Media, Joseph Kessy.

Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Fransis wa Asizi, Kongowele, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika iliyofanyika parokiani hapo. (Picha na Yohana Kasosi)

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Wakristo wametakiwa kuepuka kuwapenda wanzao kwa sababu ya vitu au misaada wanayopata, bali wafanye hivyo kwa sura na mfano wa Mungu.
Hayo yalisemwa hivi karibuni na Padri Dickson Sambala- OCARM, wakati akihubiri katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kuwashukuru Wanaparokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli – Bunju, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, kwa kumlea katika kipindi cha Uchungaji wake, iliyoadhimishwa parokiani hapo.
“Unaposali, unatengeneza matunda ya upendo, kwani unapopenda, unatengeneza matunda ya huruma kwa ajili ya kuwahudumia wengine, na unapowahudumia wengine, unatengeneza amani ndani ya mioyo ya watu….;
“Unatakiwa kuondoa matabaka kati ya walio nacho na wasio nacho. Unawaheshimu watu kwa sababu wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, lakini siyo kwa sababu ni matajiri, siyo kwa sababu wanatusaidia hiki au kile,” alisema Padri Sambala.
Katika homilia yake, Padri Sambala aliwaasa Wakristo kuepuka kuwa na upendo wa masharti, kwani upendo huo huchagua baadhi ya watu.
Aliongeza kuwa upendo wa kweli ni ule wa kidugu unaowafanya watu kuwa kitu kimoja, na kuwafanya kupokea baraka za Mungu.
Aidha, Padri Sambala aliwashukuru waamini wa Parokia hiyo kwa ushirikiano waliompatia na kuipongeza Tumaini Media kwa kazi kubwa ya uinjilishaji kupitia vyombo vyake vya habari.
Naye Roselinda Msele, Katibu wa Kamati ya Liturjia Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli – Bunju, aliwaomba watu wenye mapenzi mema kuchangia ujenzi wa kanisa jipya la Parokia hiyo, ili ukamilike kwa wakati uliopangwa.
Naye Diana Peter, Mlezi wa Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu wa Parokia hiyo, aliwasihi wazazi kuendelea kuwalea watoto katika maadili ili kupata watu wema.