Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DIDIER MASELA: Kijana ambaye wazo la kuanzisha kundi la Wenge Musica lilianzia kwake

NA REMIGIUS MMAVELE

Januari 12, 1966, katika Mji wa Matadi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, alizaliwa mtoto ambaye alipewa jina Didier Masela Ndudi Bakisa Ntadilu, ambaye baadae alikuja kuwa maarufu katika sanaa ya muziki, akiendelea kutumia jina lake lile lile Didier Masela.
Ni baba wa watoto, yaani ana mke na watoto, hivyo yeye ni baba wa familia. Didier ni mwanzilishi wa kundi la Wenge Musica, ambaye anasema wazi kuwa hakuzaliwa jijini Kinshasa, akitamba kwamba haoni aibu yeyote kutamka hadharani, kuwa amezaliwa kijijini.
Kitendo cha kuwa muasisi wa kundi la Wenge Musica, hakijamfanya athaminike kama mwanzilishi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, licha ya kwamba ni kweli wazo la kuundwa kundi la Wenge Musica alilitoa yeye, Didier anafikiri kutokana na wazo lake hilo, amewasaidia watu walio wengi. Anaamini kwamba, wako wengi ambao walikuwa hata hawajitambui kama wao ni wasanii, alikuwa akiwahimiza, kuwashurutisha na kuwasukuma. 
Didier anasema kwamba, ubunifu wa wazo hutokana kwanza na mtu mmoja na wala sio wawili, wazo hilo linaweza likakubalika na watu wengine. Kwa maana hiyo, wazo la kuanzisha kundi la Wenge Musica, lilitokana na yeye Didier, tena ni yeye ambaye aliwaita kila mmoja kati ya watu ambao anawafahamu. Watu kama Alain Prince Makaba, Werrason na Jb Mpiana, aliwaleta yeye katika kundi la Wenge Musica.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.