Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Mchakato waanza NEMC kuwa NEMA

Mh. Hamis Hamza Hamis Mh. Hamis Hamza Hamis

Dodoma

Na Julieth Sasili

Serikali imeanza kufanya marekebisho ya kubadili muundo wa Baraza la Taifa na Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (National Environment Management Council:NEMC,) na kuwa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira (National Environment Management Authority:NEMA).
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Khamis Hamza Khamis alisema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Maryam Azan Mwinyi aliyetaka kujua ni lini Serikali itawasilisha Marekebisho ya Sheria ya Mazingira ili kuipa NEMC uwezo wa hadhi ya Mamlaka.
Alisema kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais inatarajia kuwa hadi kufikia Juni mwaka 2024, Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191, uwasilishwe katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua zaidi.
Naibu Waziri Khamis (pichani) alisema kuwa marekebisho hayo ya kubadili muundo huo ni moja ya masuala yanayopendekezwa kufanyiwa marekebisho, ili NEMC iwe Mamlaka.
Akijibu maswali ya nyongeza ya mbunge huyo, Waziri Khamis alisema kuwa miongoni mwa majukumu ya mameneja wa kanda wa NEMC ni kusimamia sheria, pamoja na kutoa elimu kwa jamii.
Alitumia nafasi hiyo kuwapongeza kwa utendaji kazi mzuri, na kusema kuwa majukumu hayo yanaweza kufanyiwa marekebisho kulingana na sheria itakavyopendekeza.
Hivyo, Naibu Waziri Khamis alibainisha kuwa NEMC itakayofahamika kama NEMA, itaendelea kushirikiana kwa ukaribu na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira ya Zanzibar (ZEMA), katika utekelezaji wa majukumu, ili usimamizi wa mazingira nchini uwe endelevu na wenye mafanikio.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.