Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Baba Mtakatifu Fransisko (kushoto) akisalimiana na Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI wakati Papa alipomtembelea Mstaafu huyo katika makazi yake, akiambatana na Makardinali wapya.

Vatican City

Makardinali Wapya wamemtembelea na kumsalimia Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI, katika makazi yake.

Makardinali hao 20 walifanya ziara hiyo ya Kitume, baada ya Ibada ya kutangazwa na kusimikwa, ambapo walikwenda kumsalimia na kumtakia heri Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI.

Mababa Watakatifu hao wawili kwa pamoja baada ya kusalimiana na kuteta na Makardinali hao wapya, waliwabariki ili wakawashe moto wa huruma na upendo wa Mungu kwa waja wake.

Baba Mtakatifu Fransisko aliwatangaza na kuwasimika Makardinali wapya na kuwapigia kura Wenyeheri wapya wanaotarajiwa kuingizwa kwenye orodha ya Watakatifu wa Kanisa.

Wenyeheri hao ni Mwenyeheri Padri Giovanni Battista Scalabrini aliyetangazwa na Mtakatifu Yohane Paulo II, kuwa Mwenyeheri, Novemba 9, mwaka 1997.
Padre Giovanni Battista alizaliwa Julai 8, mwaka 1839 na kufariki dunia Juni Mosi mwaka 1905.

Alikuwa ni Askofu wa Jimbo Katoliki la Piacenza-Bobbio, Italia na Mwanzilishi wa Mashirika ya Wamisionari wa Mtakatifu Carlo Borromeo, maarufu kama Wascalabrini, na pia ni Muasisi wa Taasisi ya Waamini Walei Wascalabrini, iliyoanzishwa kunako mwaka 1961.

Wa pili ni Mwenyeheri Artemide Zatti, Bruda wa Shirika la Wasalesian wa Don Bosco, aliyezaliwa tarehe 12 Oktoba 1880, nchini Italia.
Akafariki dunia Machi 15, mwaka 1951 huko Viedma nchini Argentina.

Utakatifu wake unapata chimbuko lake katika huduma kwa maskini kwa kuongoza hospitali na duka la dawa kwa ajili ya maskini, kwa muda wa miaka 40.
Aprili 14 mwaka 2002, alitangzwa na Baba Mtakatifu Yohane Paulo II, sasa ni Mtakatifu, kuwa ni Mwenyeheri.

Separated they live in Bookmarksgrove right at the coast of the Semantics, a large language ocean. A small river named Duden flows by their place and supplies it with the necessary regelialia. It is a paradisematic country, in which roasted parts of sentences fly into your mouth.

DAR ES SALAAM

Na John Kimweri
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi, amewataka waamini kutoa kipaumbele na kuwakumbuka wanyonge na watu wasiojiweza katika karamu mbalimbali wanazoziandaa.
Wito huo aliutoa hivi karibuni wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa ya kutoa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, iliyokwenda sanjari na uchangiaji wa ujenzi wa nyumba ya Mapadri, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Dominiko Savio, Mikoroshini Tandika, jimboni humo.
Alisema Wakristo hawawezi kumlipa Kristo kwa kazi kubwa ya ukombozi aliyoifanya, lakini kwa njia ya kuwasaidia wengine, wanaweza kufanya utume na kazi ya kumpendeza Mungu.
“Yesu anatuambia kwamba tunapofanya karamu, tuwakumbuke wanyonge kama maskini, viwete, na wale wasio na cha kutulipa, wale ambao hutegemei nao waandae sherehe wakualike,” alisema Askofu Ruwa’ichi.
Askofu Ruwa’ichi alieleza kuwa katika Pentekoste, Roho Mtakatifu aliwashukia mitume na kuwapa nguvu, uthubutu na msukumo wa kwenda kuitangaza Injili, bila kuogopa.
Alisema kijana anayeimarishwa akimpokea Roho Mtakatifu, anakamilishwa katika neema ya ubatizo, kwa kuwa katika ubatizo huzaliwa mara ya pili, na kufanywa kuwa mtoto wa Mungu na ndugu wa Kristo.
“Katika Pentekoste, Roho Mtakatifu aliwashukia Mitume na kuwapa nguvu na uthubutu na msukumo wa kwenda kuitangaza Injili. Hawa watoto leo kwao ni Pentekoste, na watampokea tena Roho Mtakatifu, kwasababu tayari walishampokea” alisema Askofu Ruwa’ichi.
Katika hatua nyingine, Padri Canisius Hali, wa Parokia hiyo amewaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kushirikiana nao katika kazi hiyo ya ujenzi wa nyumba ya mapadri.
Kwa mujibu wa Padri Hali, alibainisha kuwa kwa sasa ujenzi huo upo katika hatua za mwisho, na kumshukuru Baba Askofu kwa ushauri na kuwa pamoja nao katika shughuli hiyo.
“Tunajenga nyumba ya mapadri ambayo ipo katika hatua za mwisho, na Baba Askofu amekuwa karibu nasi katika hatu zote, ninawaalika waamini kutoka maeneo mbalimbali ili kushirikiana nasi katika kazi hii” alisema Padri Hali.
Katibu wa Halmashauri ya Walei Parokia hiyo, Pankrasia Heri, alifafanua kuwa kwa sasa Paroko wa Parokia hiyo anaishi nje ya nyumba hiyo, na hivyo kumshukuru mmoja wa waamini ambaye ndiye aliyejitolea nyumba hiyo.
Alisema pia kuwa kukosekana kwa nyumba hiyo, na wasaidizi wengine ndani ya Parokia kama Mafrateri na mashemasi, kumesababisha utendaji kazi wa Paroko uwe mgumu.

 

Ujenzi wa Kituo cha Afya cha kisasa katika Kata ya Lukobe, Mkoani Morogoro ukiendelea.

MOROGORO

Na Angela Kibwana

Serikari ya Tanzania imetoa Shilingi milioni 500/- zilizotokana na tozo za miamala ya simu, kukamilisha mradi mkubwa wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha kisasa katika Kata ya Lukobe, Mkoani Morogoro.
Kukamliki kwa mradi huo kutawanufaisha zaidi ya wananchi 35,000 watakaopata shida za kiafya kutoka Kata ya Lukobe na Kata jirani, Mkoani humo.
Akizungumza wakati wa kukagua mradi huo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Ally Machela alisema kuwa tayari Serikali imetoa shilingi milioni 500/= zilizopokelewa na Manispaa ya Morogoro kukamilisha ujenzi wa kituo hicho.
“Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro inatekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kata ya Lukobe kitakachohudumia wananchi 35,000 baada ya kukamilika kwake,”alisema Machela.
Alifafanua kuwa fedha zilizotolewa katika awamu ya kwanza ambazo ni kiasi cha Shilingi milioni 250/=, zilitumika kujenga maabara,jengo la wagonjwa wa nje, na kibanda cha kuchomea taka.
Aidha, alifahamisha kuwa katika awamu ya pili, Serikali ilitoa Shilingi milioni 250/- kwa ajili ya majengo mawili ambayo ni jengo la wazazi, jengo la kufulia nguo, na jengo la upasuaji.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro Dk. Charles Mkombachepa, alisema kuwa kituo hicho cha afya kitaongeza tija kwa wananchi kwa sababu kina uwezo wa kuhudumia watu 35,000 kutoka Kata ya Lukobe, Mkundi, Kihonda na Kata nyingine jirani.
Aliongeza kuwa kituo hicho kina majengo mbalimbali ya kutolea huduma kwa wagonjwa, kati yao kuna jengo la wanawake; jengo la wagonjwa wa nje; jengo la wazazi; jengo maalum kwa ajili ya upasuaji wajawazito; na huduma nyingine za afya ya mwanamke.
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood, baada ya kuridhishwa na ujenzi wa kituo hicho, aliahidi kutoa magari mawili yenye thamani ya Shilingi milioni 172/- kubebea wagonjwa  katika Kituo cha Afya Lukobe, na Kituo cha Afya Tungi kinachojengwa  kwa mapato ya ndani ya Manispaa.
Nao baadhi ya wakazi wa Kata ya Lukobe walisema kuwa wanamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha ili kukamilisha ujenzi huo.
Naye Mwandishi Victor Wambura anaripoti kuwa, wasomi nchini wameiomba Serikali kutimiza ahadi yake kwa wananchi kwa kuzielekeza tozo ili kuboresha miradi ya maendeleo ya jamii, hivyo kuondoa malalamiko ya wananchi kuhusu tozo hizo.
Akizungumza na gazeti la Tumaini Letu, Mchumi na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar salaam (UDSM) Dk. Martin Chegere, alisema kuwa hakuna tozo yoyote itakayomfurahisha mtu, na hakuna mtu anaependa kitu kinachomchukulia pesa yake, ikiwa hakipo kwenye matumizi yake.
“Tumeahidiwa kwamba vikichukuliwa basi vitarudi kwa mfumo utakaotusaidia kuweka mazingira mazuri ya afya, elimu na miundombinu, hizo ndizo ahadi tulizoahidiwa na viongozi wetu,” alisema Dk. Chegere.         
Alisema pia kuwa Serikali inatakiwa kuwatendea watu haki, kulingana na ahadi ya kuboresha miundombinu ya kijamii, kwa sababu wananchi wanaumia wakiona vitu hivyo havitendeki, hasa kwa kutumia kodi hiyo ya tozo.
Aidha, Dk. Chegere alisema kwamba usahihi wa tozo utakuwepo pale ambapo Serikali itarejesha kwa wananchi kwa namna bora zaidi ya kuwapatia huduma.
Aliwasihi wananchi kuiunga mkono Serikali, kwani hata kwenye Bibilia Takatifu, Yesu aliwaambia wanafunzi wake kuwa ya Kaisari mpe Kaisari na ya Mungu mpe Mungu, ikiwa na maana ya kwamba serikali nayo inahitaji mapato.
Naye Mchumi na Muhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar esalaam Dk. Innocent Pantaleo, alisema kuwa Wananchi wanatakiwa kuiunga mkono Serikali kwa kukusanya mapato, na kudai kwamba kwa sasa wahisani hawaleti pesa za kutosha kama ilivyokuwa awali.
Aidha, Dk. Pantaleo aliiomba Serikali kuzingatia usawa kwa kumwangalia mwananchi mwenye kipato cha chini, ili kuondoa matabaka.
Hata hivyo, alisema Serikali izingatie kuboresha maeneo ambayo yanamgusa huyo mwananchi anaetozwa kodi kwa kuboresha miundombinu ya kijamii, kama vile ya afya, elimu na miundombinu, kwani hicho ndicho kilio cha wengi.

Nairobi, Kenya
Mwendesha baiskeli wa Kenya Suleiman Kangangi amefariki dunia kufuatia ajali ya mwendo kasi katika mbio za magari nchini Marekani siku ya Jumamosi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 ambaye alikuwa akishiriki mbio za changarawe za Overland huko Vermont, shindano la kilomita 59 la barabara za udongo, likijumuisha takriban futi 7,000 za kupanda.
Kangangi alimaliza wa tatu katika Tour of Rwanda mwaka wa 2017 alipokuwa akikimbilia timu ya UCI Continental ya Ujerumani, Bike Aid, kabla ya kubadili mbio za changarawe.
Kwa upande wake Rachel Ruto, mke wa rais mteule William Ruto wa Kenya, alichapisha kwenye Twitter, “Sote tutamkosa kama mtu binafsi. Kenya imepoteza bingwa. Pumzika kwa amani Sule”.
Nayo taarifa ya klabu yake ilisema, “Sule ni nahodha wetu, rafiki, kaka. Yeye pia ni baba, mume na mwana”.

Kamati ya Uongozi wa Kitaifa ya Kushughulikia Mambo ya Kitume iliyoteuliwa na Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Ethiopia, ikiwa katika picha ya pamoja.

ADDIS ABABA, Ethiopia

Baraza la Maskofu Katoliki nchini Ethiopia limeunda Kamati ya uongozi Kitaifa, ili kushughulikia changamoto mbalimbali za Kitume.
Maaskofu hao wamepitia masuala msingi ya Kitume ya Kanisa, fursa na changamoto katika mkutano wao wa kawaida wa 53, na kuunda Kamati ya Uongozi ya Kitaifa itakayofanyia kazi maandalizi ya Mpango Mkakati wa Miaka 10, ili changamoto zilizojitokeza wakati wa mkutano huo, ziweze kutatuliwa ipasavyo.
Kamati ya uongozi ya Taifa itaongozwa na Katibu Mkuu Mchungaji Abba Teshome Fikre, na itakuwa na wajumbe 10 wakiwemo Naibu Katibu Mkuu, maafisa na wakuu wa CMRS, na Mshauri wa ndani.
Kamati ya kitaifa tayari imeanza kazi yake ya kujadili Mchakato wa Mpango Mkakati, kuandaa mikakati ya utekelezaji na jukwaa la awali la uhamasishaji. Kwa kuzingatia hili katika wiki chache zilizopita, kamati imeandaa Mpango Kazi wa Miezi Sita ijayo.
Kuanzia Agosti 10 hadi 13, awamu ya kwanza ya kazi imekuwa ziara katika Majimbo mbalimbali, na maandalizi ya mpango wa kina yamefanyika katika Majimbo sita, ambayo ni pamoja na Jimbo Kuu Katoliki la Addis Ababa, Vikariati ya Meki, Jimbo Katoliki la Kitume la Vazi, Vikariati za Hawasa, Sodo, Hossana, Jimma-Bonga, na Eparchy ya Emdibir.
Katika mchakato huo, majadiliano mbalimbali yalifanywa na Maaskofu na viongozi husika kuhusu Mpango Mkakati huo.
Baadhi ya ajenda zilizoonyeshwa katika mjadala ni pamoja na Asili ya Mpango Mkakati wa kina wa Kanisa; Umuhimu wa Mpango Mkakati wa Miaka 10; Mchakato na Changamoto za Sasa za Huduma ya Dayosisi; Wajumbe wa Kamati ya uongozi ya dayosisi wakishirikiana na kamati ya Taifa.
Kwa kuongezea, mafunzo mafupi kuhusu itifaki za mawasiliano na jukwaa pepe, yalitolewa ili mawasiliano ya kazi zijazo yawe na ufanisi.
Majadiliano mengine yatafanyika katika maeneo ya Eparchy ya Bahirdar-Dessie, Vicariate ya Nekemet, na Dayosisi ya Gambella, na wawakilishi wa makuhani wa Eparchy of Adigrat watafanya mkutano huko Addis Ababa.
Mpango Mkakati wa Kanisa nzima ni mojawapo ya maelekezo ya kazi yanayofuata yaliyoamuliwa na Baraza la Maaskofu, Mpango Mkakati wa Miaka 10 wa Kanisa utatayarishwa kwa kuzingatia maono ya pamoja ya Kanisa, kwa kuzingatia huduma ya kichungaji, maendeleo ya kijamii. na maelekezo ya kiutawala ya Kanisa.
Mpango wa miaka 10, unatathmini mipango ya awali iliyofanywa na taasisi za Kanisa, pamoja na ile ambayo imeanzishwa na inayotekelezwa. Muda mfupi wa mipango mkakati, changamoto katika utekelezaji na ukosefu wa tathmini kwa wakati, ulielezwa kuwa sababu kuu za kutotekelezwa.
Kamati ya Uongozi iligawa Mpango Mkakati katika awamu nne za utekelezaji, na kuweka ukomo wa muda kwa kila moja. Hatimaye, Mpango Mkakati unalenga Mashirika ya Kanisa kufanya kazi pamoja kwa ajili ya maono ya pamoja ambayo yanasimamia utume na maadili ya Kanisa Katoliki.

GULU, Uganda
Maandalizi ya kutangazwa Padri Joseph Ambrozoli kuwa Mwenyeheri yanaendelea vizuri, tukio litakalofanyika wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu itakayofanyika Jimbo Kuu Katoliki la Gulu, Uganda Novemba 20, mwaka huu.
Mchungaji John Baptist Odama wa Jimbo Kuu Katoliki la Gulu alisema kuwa Kamati Kuu ya Maandalizi (COC) yenye kamati ndogo 16 imeundwa, na wote wanafanya kazi ya kuona jinsi ya kuwapokea watu watakaokuja kuhudhuria ibada hiyo.

DAR ES SALAAM

Na Nicolaus Kilowoko

Kocha Msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars Mecky Mexime amefunguka kuwa kwa sasa Watanzania wanapaswa kuganga yajayo, hasa katika kuwekeza nguvu na mapenzi juu ya timu yao ya Taifa.
Mexime ameyasema hayo mara baada ya Watanzania wengi kusikitishwa na matokeo ya Taifa kushindwa kufurukuta katika mashindano mbalimbali wanayoshiriki, na kusababisha wengi kuumia.
Mexime alisema kuwa kwenye mpira hakuna kukata tamaa, na matokeo siku zote ni ya pande tatu, hivyo kwa sasa si vyema kulaumu sana, ila ni kuongeza nguvu kwa pamoja kama Watanzania.
Alisema kuwa timu ya Taifa ni ya Watanzania wote, na si ya mtu mmoja. Hivyo, kila jambo linawezekana ikiwa mataifa mengine yanafanikiwa kushiriki mashindano makubwa, hata Tanzania inaweza kushiriki katika mashindano hayo.
“Siku zote kuteleza siyo kuanguka, na hata kama ukianguka, unapaswa kusimama tena. Watanzania wazidi kupenda vya kwao na kuongeza nguvu kwa pamoja katika kuijenga timu yetu, na siyo kulaumu mtu”, alisema Mexime.
Alisema kuwa mchezo wa mpira kwa sasa ni vyema wote kwa pamoja tukatengeneza mkakati wa pamoja ili tuweze kufanya vyema katika michuano inayofuata na inayoshiriki timu hiyo.
Stars ilishindwa kufurukuta katika uwanja wa Benjamin Mkapa wakati wa mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya wachezaji wanocheza ligi za ndani, CHAN, mbele ya timu ya Taifa ya Uganda kwa kufungwa bao 1-0.
Huu ni mwendelezo wa matokeo mabovu ambayo Stars wameendelea kuyapata baada ya misimu iliyopita kushindwa kufuzu kucheza Kombe la Dunia, Afcon, Chan pamoja na michezo mbalimbali ya kirafiki.
Meck Maxime anachukua nafasi ya kocha msaidizi mara baada ya kuvunjwa kwa benchi la ufundi la Stars kutokana na matokeo mabovu. Hivyo anaungana kwa sasa na kocha Mkuu, Hanour Janza, akisaidiwa na kocha wa magolikipa, Juma Kaseja.
TFF ilitangaza kukubaliana na aliyekuwa kocha wa timu hiyo Kim Poulsen kumbadirishia majukumu, na sasa atabaki katika timu za vijana za Taifa.
Ikumbukwe kuwa Kim alitangazwa na TFF kuwa Kocha Mkuu wa Stars, Februari 15 mwaka 202, kabla yake aliwahi kuwa kocha wa Stars mwaka 2012 na 2013.
Kim mpaka anawekwa pembeni, amepoteza mechi 7, akipata ushindi kwenye mechi 6, na sare kwenye mechi 4. Alipewa mkataba wa miaka mitatu kuinoa timu ya Stars.

ARUSHA

Na Mwandishi wetu

Mkurugenzi wa Idara ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto, Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Padri Dennis Ombeni amewataka Raia wa Jumuiya ya Afrika Mashariki popote walipo, kuwa mstari wa mbele kulinda uhai wa mtoto angali bado tumboni.
Mambo yanayojumuisha katika kumlinda na kumtetea mtoto, yakiwemo ya ukuaji, kumlinda katika nyanja zote kiuchumi, kiafya na kiakili, na ustawi wa Mtoto.
Padri Ombeni aliyasema hayo katika warsha kwa Vijana na wazazi iliyofanyika jijini Arusha iliyolenga kuwajengea uelewa kuhusu athari zilizopo kwenye muswada wa ujinsi na afya ya kizazi wa Jumuiya ya Afika Mashariki wa mwaka 2021.
Kupitia mkutano huo, Padri Ombeni alieleza kusikitishwa juu ya mauaji katika jamii kati ya wanandoa yanayotokea kwa kisingizio cha wivu wa mapenzi jambo alilosema ni ouvu na linapaswa kukemewa kwa nguvu zote kwani linaingilia Uhai ambao asili yake ni Mungu.
“Maandiko Matakatifu kupitia Bibilia yanaeleza kwa namna kuu mbili, juu ya thamani ya uhai katika Bibilia, Maandiko Matakatifu yanatetea uhai, hasa pale kwenye Agano la Kale, ambapo baada ya Mungu kumuumba Adamu na kumpatia msaidizi wake Eva, aliwabariki na kusema, enendeni mkazae na kuijaza dunia,”alisema Padri Ombeni.                          
Alisema pia kuwa uhai wa mwanadamu ni kitu kitakatifu, hivyo unapaswa kulindwa na kutunzwa tangu kutungwa mimba hadi kifo chake cha kawaida. Hivyo muswada huo wa Ujinsi na Afya ya kizazi haupaswi katika Mataifa ya Jumuiya Afrika Mashariki kwani unakwenda kinyume na Utu, Dini na tamaduni za watu hao.
Kwa mujibu wa Padri Ombeni Mswaada huo unatishia uwepo wa Dini na Imani za Watu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, pia unadhalilisha Mila na Desturi za watu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kwani hautoi nafasi kwa wahudumu wa afya kutumia dhamiri zao katika kutoe elimu ya afya ya uzazi kwa wanaowahudumia.
Kutokana na hayo na mengine maovu yaliyoko katika Mswaada huo ambao umeakisiwa na kupigiwa debe na baadhi ya vikundi vyenye nia ovu na watu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Padri Ombeni amewataka watanzania wote kuungana na wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kuupinga Muswaada huo.
Mmoja wa Washiriki wa Mkutano huo, aliyejitambulisha kwa jina la Anna Anatoli alisema ulimwengu umekosa hofu ya Mungu  na ndiyo maana imefika hatua wanadamu wanaweka mikakati ya kutowesha Uhai bila kuwa na hofu ya kwamba kazi hiyo ni ya kwake Mungu Muumba ambaye yeye ni asili ya Uhai wenyewe.
“Hatuna sababu ya kushabikia mambo kutoka mataifa ya mbali ambayo kwao wamefika mahali wameona Uhai si zawadi kutoka kwa Mungu kwenda kwa mwanadamu, natamani kuona tunabaki na vyakwetu huku tukiendelea kuwajengea hofu ya Kimungu watoto wetu,”alisema Anna.
Kwa upande wake Betty Sammaye aliwataka wazazi kusimama na kuwapeleka watoto wao Kanisani kwani Mtoto akikuwa kwenye uwepo wa kumcha Mungu ataweza kusimama na kujitetea na Neema ya Mungu itakuwa ndani katika kumwongoza.
Betty amewataka wazazi kuchukua muda kuzungumza na watoto wao, kwani vitu vinabadilika mno kila siku, na kamwe wasikubali watoto wao kutoka nje ya himaya yao bila kufahamu kwa kina ni wapi hasa wanakwenda na wanakwenda kufanya nini.
Muswada huo wa Afya ya Kizazi na Ujinsi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Mwaka 2021 unaelezwa kukiuka maadili, Utu na Dini za watu wa Jumuiya ambao una vipengele vinavyochochoa ngono kwa watoto na Vijana, na pia utoaji mimba.
Na ikiwa muswada huo utaachwa upite, basi itazilazimu nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutunga Sheria kulingana na matakwa ya muswada huo.

NAIROBI, Kenya

Askofu Mkuu Hubertus Maria van Megen, Balozi wa Kitume nchini Kenya na Sudan Kusini, amewataka waamini kujitahidi kupyaisha nyuso zao na kujitoa katika huduma kwa wengine, ikiwa ni njia mojawapo ya kufanya dunia kuwa mahali bora kwa kila mtu.
Katika mahubiri yake wakati wa sherehe za kuitisha kwa ajili ya kuanza kwa Chuo Kikuu cha Tangaza mwaka wa masomo 2022/2023, Askofu Mkuu Megen, alitoa mfano wa Zaburi 104:30 na kuwataka Wakristo kubadili mienendo yao na kuishi kulingana na sheria. viwango ambavyo Mungu huweka katika Neno Lake.
“Mara nyingi tunaimba na kumsihi Roho Mtakatifu aufanye upya uso wa dunia, lakini vipi kuhusu uso wako? Kwa nini usiseme, “Bwana, itume roho yako na uufanye upya uso wangu?”
Askofu Mkuu Megen alisema kuwa ni wakati stahiki kwa waamini na wanafunzi hao kumwomba Roho wa Mungu kwa hekima na mwelekeo katika kutimiza malengo ya mwaka mpya wa masomo wa chuo hicho kinachomilikiwa na Wakatoliki.
Aidha, aliwataka Wakatoliki kumruhusu Roho Mtakatifu kuwaongoza katika utume wao, huku akiwatahadharisha kuhusu madhara yanayoweza kuepukika ya udhaifu wa kibinadamu, ambao mara kwa mara huwafanya kutafuta anasa za dunia.
“Wanadamu wana mwelekeo wa kuuumba ulimwengu wao usiolingana na kanuni za Neno; tunashawishiwa sana na ulimwengu na kuishia kuishi kulingana na mahitaji ya mwili,” alisema Askofu Mkuu Megan.
Askofu Mkuu Megen alihusisha zaidi Zaburi na amri kuu zaidi, akisisitiza kwamba ilikuwa njia pekee ya kupata ushirika wa kweli na Mungu.
Mwakilishi huyo wa Kitume alisisitiza mafundisho ya Roho Mtakatifu, kuhusu kumtumikia Mungu huku akizungumzia ongezeko la watu, wakiwemo wa kidini, kuingia katika makundi na matabaka ya kijamii.
Askofu Mkuu Megen alilielezea Kanisa kuwa ni taasisi ya kibinadamu inayoundwa na watu ambao, kama watakatifu, wanaweza kukabiliwa na kasoro za kibinadamu.