Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Nottingham, England
Andy Murray anajiandaa kwa Wimbledon yake ya 15, itakayoanza Julai 3 mwaka huu, huku nyota huyo mwenye umri wa miaka 36, lakini hatazami kustaafu hivi karibuni.
Andy Murray anatumaini Wimbledon ya mwaka huu haitakuwa yake ya mwisho, akisema kwamba anataka kujituma kwa kucheza kwa kiwango cha juu sana kabla ya kutundika daluga lake.
Murray alitolewa katika robo fainali na Sam Querrey huko Wimbledon mnamo 2017, na kazi yake ilionekana kuwa mwisho baada ya kutolewa kwenye Australian Open mnamo mwaka 2019, lakini upasuaji wa kurekebisha nyonga yake ulimpa nafasi ya pili mchezaji huyo wa zamani wa Ulimwengu.
Ushindi wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 katika michuano ya hivi majuzi ya Nottingham Challenger, ulimpeleka kwenye cheo chake cha juu zaidi tangu upasuaji wake wa nyonga akiwa nambari 38 duniani.
Murray aliorodheshwa katika nafasi ya 839 duniani mnamo Julai 2018 alipopata nafuu baada ya upasuaji wake wa kwanza wa nyonga, kushindana na Grand Slams tena kulionekana kuwa tumaini la kusikitisha, lakini amepambana, na sasa ana matumaini makubwa ya kushindana tena katika daraja la juu la mchezo huo.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Ukikatiza katika mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, hasa muda wa jioni, utakutana na vikundi vya vijana wakicheza soka.Mara nyingi huwa wanakuwa na timu zao zenye majina yaliyobeba mitaa wanayoishi.
Pia, huenda mbali zaidi na kuanzisha ligi za mtaani ambazo hutumika kuburudisha nafsi zao na za mashabiki wao.
Wachezaji hunufaika na zawadi zinazowaniwa kwenye ligi husika kama vile mbuzi, ng’ombe, kuku pamoja na malipo ya kiasi kidogo cha fedha, huku mashabiki wakinufaika na burudani wanayopata kupitia timu za mitaa yao.
Utamaduni huo wa soka la mtaani umeibua jina maarufu la ‘Ndondo’.Jina hili limeibuka tangu miaka ya zamani, hasa kutokana na mtindo wa ligi na wachezaji wake.
Mtindo wenyewe ni namna wachezaji wanavyopatikana na kutumika katika timu za mitaani.
Neno ‘ndondo’ limeibuka kutoka kwenye wali maharage, na kama usivyofahamu, mboga ya maharage imepewa jina la ndondo, kivipi? Katika miaka ya zamani, wachezaji wengi wa mtaani malipo yao hasa yalikuwa wali na maharage, kwa maana kwamba mchezaji akitakiwa na timu fulani kwa ajili ya mechi za mtaani, atatakiwa kukusanyika na wenzake mapema kabla ya mchezo, na kinachofuatia ni kula wali na maharage, kisha mechi ikimalizika anapewa neno ‘asante’ na kuondoka.
Ikitokea viongozi husika wa timu wakijiongeza, mchezaji anapata walau nauli ya kwenda na kurudi pamoja na wali maharage.
Katika miaka ya hivi karibuni hadi sasa kumekuwa na mabadiliko kiasi, kwani licha ya mchezaji kula wali na maharage, pia hupewa posho fulani ambayo ndani yake inaweza kumsaidia kwa nauli na kununua mahitaji yake mengine madogo madogo.
Kutokana na kuwepo kwa staili hiyo, ndipo neno ‘ndondo’ likawa linatumika na kuvuma, hata wachezaji wenyewe wa mtaani wakikodiwa sehemu kwenda kuichezea timu fulani, utasikia “Ninakwenda kwenye ndondo”, akimaanisha anakwenda ‘kupiga’wali maharage na kucheza soka.
Huko kwenye soka la ‘ndondo’ masuala ya usajili yapo kama yalivyo kwenye ligi kubwa, ingawa tofauti yake ni kwamba usajili wa soka la mtaani hufanyika kulingana na mashindano maalum, na si msimu mzima wa mwaka ama miaka.
Kwenye soka la ‘ndondo’, kwa mwezi mchezaji anaweza kuchezea hata timu 10 zinazoshiriki michuano tofauti kwenye maeneo tofauti, kwa mfano, anaweza kuchezea timu A ya ligi fulani ya Ilala, na wakati huo huo akawa anachezea timu X ya ligi fulani ya mtaani huko Temeke, ilimradi tu hayo mashindano ya mtaani yawe hayana muingiliano wowote.
Kuna wakati hata wachezaji wanaocheza Ligi Kuu ama Daraja la Kwanza, nao wamekuwa wakiongeza nguvu kwenye ligi hizi za mtaani, wakiamini kwamba wanatoa mchango kwa timu za mitaa yao ambazo zimewalea na kufika walipofika.
Kwenye ligi hizo za mtaani, kama ikitokea kuna ligi ya kuwania kombe la mbuzi, basi mbuzi huyo atachinjwa na kuliwa na wali, pamoja na wachezaji wote walioshiriki kupata ubingwa.
Mbali na yote, mechi za mitaani ndizo zinazosaidia kuibua vipaji vya wachezaji ambao leo hii wanang’ara katika timu za Ligi Kuu nchini, hasa kutokana na kukosa mfumo thabiti wa kukuza vipaji vya vijana wadogo, kama ilivyo katika nchi zingine.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Kocha mkuu wa timu ya KMC ya Kinondoni Jamhuri Kihwelo amesema anataka kufanya mpango wa kumshawishi golikipa mstaafu Juma Kaseja, ili msimu ujao arejee langoni kuitumikia tena timu hiyo.
Kaseja alitangaza kustaafu soka mwishoni mwa msimu wa 2021/2022 akiwa na timu ya KMC na kuhamia kwenye jukumu lingine la kuwa kocha wa magolikipa wa timu za taifa.
Kihwelo, maarufu kama Julio, hivi karibuni alivutiwa na kiwango kilichoonyeshwa na nyanda huyo wa zamani wa Moro United, Simba SC, Yanga na Taifa Stars, wakati alipoichezea timu ya Ali Kiba katika mechi ya hisani dhidi ya timu ya Mbwana Samatta.
Katika mechi hiyo ya tamasha la SamaKiba, Kaseja alionyesha kwamba bado ana kitu anaposimama langoni, licha ya timu yake kufungwa mabao 4-2 na timu ya Samatta kwenye uwanja wa Azam Complex, jijini Dar es salaam.
“Kaseja bado ni kipa mzuri sana licha ya kustaafu.Nikiwa kama kocha wa KMC, nitamshawishi ili aweze kurudi na kuitumikia timu hii msimu ujao,”alisema Julio.
Alisema kwamba Mungu akipenda atamchukua kipa huyo na kumrejesha ndani ya KMC kwa sababu ni mtu anayejitambua kwa kujali mazoezi, na bado uwezo wa kudaka anao.
Hadi gazeti linaingia mtamboni, juhudi za kumpata Kaseja mwenyewe ziligonga mwamba kufuatia simu yake kuita bila kupokelewa, ingawa mara ya mwisho wakati ametangaza kustaafu soka, alidai kuwa amefanya hivyo ili kuwapa nafasi vijana wanaochipukia kwa sasa.
Mbali na hilo, inaelezwa kwamba alichoshwa na maneno ya watu waliokuwa wakimzodoa kwa madai kwamba anaziba nafasi za vijana, wakati yeye tayari umri wake umekwenda.
Kaseja alianza kuonekana kwenye medani ya soka la ushindani mwaka 2000 akiichezea Moro United aliyojiunga nayo ikiwa Ligi Kuu, akitokea Shule ya Sekondari ya Makongo, na kucheza kwa msimu mmoja.
Mwaka uliofuata alijiunga na Simba aliyoichezea kwa mafanikio kwa zaidi ya miaka 10 kwa misimu tofauti.
Pia, Kaseja aliichezea Yanga katika vipindi viwili kama ilivyo kwa Simba, na baadaye alijiunga na Kagera Sugar, kisha kutimkia Mbeya City, na kumalizia KMC.

Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Nicholaus wa Tolentino, Msingwa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara hivi karibuni parokiani hapo.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu, akiwa katika picha ya pamoja na Utume wa Kwaya Katoliki Tanzania (UKWAKATA) Parokia ya Mtakatifu Nicholaus Tolentino, Msingwa jimboni humo. Wengine ni Mapadri wanaofanya Utume parokiani hapo.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu (katikati) na Mapadri, wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Kamati Tendaji ya Halmashauri ya Walei Parokia ya Mtakatifu Nicholaus Tolentino, Msingwa, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara parokiani hapo. (Picha zote na Yohana Kasosi)

Vijana wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima wa Karmeli, Bunju Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, walioimarishwa kwa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti hiyo hivi karibuni.

Wanachama wa Shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Misa Takatifu ya Sherehe ya Somo wao, iliyoadhimishwa katika Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, Manzese jimboni humo.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, akimpongeza Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, kwa kuadhimisha Jubilei ya Miaka 25 ya Ukardinali wake, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akisalimiana na kijana James Peter, mwamini wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli, Bunju, jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara. Kulia ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Dominic Somola.