Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Magenge ya waasi yawaua Watawa

Watawa wawili wa Shirika la Dada Wadogo wa Mtakatifu Teresa waliokuwa wakifanya kazi katika shule moja huko Mirebalais, nchini Haiti, wameuawa na magenge yenye silaha kali walipokuwa wamejificha katika nyumba na msichana mmoja wakati wa mashambulizi ya silaha.
Aidha, magenge hayo yenye silaha kali yaliingia ndani ya nyumba hiyo na kuwaua watawa hao pamoja na watu wengine wote waliokuwapo.
Katika ujumbe wake Baba Mtakatifu Fransisko baada ya sala ya Malaika wa Bwana Dominika ya 5 ya Kwaresima, pamoja na mambo mengine, alitoa wito wake katika maeneo yanayojihusisha na matumizi ya silaha, kuachana na ghasia zilizopo.
Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Port-au-Prince, nchini Haiti, Mhashamu Max Leroy Mésidor, alivithibitishia Vyombo vya Habari vya ndani kuhusu kutokea kwa tukio hilo, na kuongeza “Ni hasara kubwa kwa jumuiya.”
Watawa hao ni Sista Evanette Onezaire na Sista Jeanne Voltaire waliuawa hivi karibuni, huku Jiji la Mirebalais likikabiliwa na mashambulizi ya silaha na muungano wa wahalifu Viv Ansanm, ambapo ghasia hizo pia zilichukua sura ya mashambulizi dhidi ya wafanyabiashara, vituo vya polisi na hata gereza, na kwamba zaidi ya wafungwa 500 waliripotiwa kutoroka.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.