Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

TFF yapania kuwekeza kwenye VAR

Wambula Wambula

Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini(TFF), limeahidi kuendelea kuwekeza kwenye teknolojia ya Msaidizi wa Video (VAR) kwa kutoa elimu kwa waamuzi wengi zaidi, na hata kuzalisha wakufunzi wazawa ili kuhakikisha usimamizi wa mechi nchini, unaendana sawa na mabadiliko kulingana na wakati kwa kufuata viwango vya kimataifa.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Sheria, Habari na Masoko wa Shirikisho hilo, Boniface Wambura ambaye pia ni Msimamizi Mkuu wa Kozi mbalimbali, zinazowezeshwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Alisema kuwa wanahitaji kuona mabadiliko chanya kwenye usimamizi wa mechi nchini, hivyo kupitia VAR wanaamini watapunguza malalamiko ya maamuzi na kuongeza ubora wa ligi na mashindano mengine wanayosimamia.
Alisema kwamba anaamini hadi kufikia muda rasmi wa kuanza matumizi ya teknolojia hiyo katika Ligi ya Tanzania, waamuzi wengi watakuwa na weledi mkubwa kuhusiana na matumizi yake.
Wambura alisema kuwa kozi hizo zitaendelea kutolewa kwa makundi mbalimbali, ili kuongeza zaidi idadi ya namba kubwa ya waamuzi wenye ujuzi wa kutumia teknolojia hiyo ya VAR.
Tayari TFF ilitangaza mpango wa kuanza kutumia baadhi ya mashine za VAR, ili kupunguza malalamiko ya kimaamuzi ingawa bado kuna uhitaji mkubwa wa mashine nyingi, ili kila uwanja uwe unatoa haki ya kimaamuzi.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.