Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Yanga yajitoa ufahamu Ligi Kuu Tanzania Bara

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Licha ya ratiba na takwimu za msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kuonyesha kwamba Yanga imebakiza michezo minne ili kumaliza msimu huu, wenyewe wanasisitiza kwamba wamesaliwa na mechi tatu pekee.
Yanga imebakiza mechi dhidi ya Namungo FC (nyumbani), Tanzania Prisons (ugenini), Dodoma Jiji (nyumbani) na Simba SC (nyumbani).
Mbali na ratiba kuonyesha hivyo, wenyewe wamesisitiza kwamba kwa sasa anazifukuzia pointi zao tisa, ili wamalize Ligi na kushangilia ubingwa wa nne mfululizo wa Ligi Kuu.
Afisa Habari wa Klabu hiyo Ali Kamwe (Pichani) alisema kuwa wao wanachotambua kwa sasa wana kazi kubwa ya kuhakikisha wanashinda mechi tatu zilizo mbele yao.
“Tuna mechi tatu zilizobaki mbele yetu, tutajitahidi kuhakikisha tunapata ushindi mechi zetu zote ili kutangaza ubingwa, hiyo nyingine hatuifahamu na haituhusu. Mashabiki wetu tunawasihi wasianze sherehe sasa hivi, ni mapema mno kwa sababu hatujamaliza mechi zetu tatu,” alisema Kamwe.
Hadi sasa wapenzi wa soka wanasubiria siku ambayo Bodi ya Ligi itaweka wazi tarehe ya mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga, ambao ulipangwa kuchezwa Machi 8 mwaka huu lakini ukaahirishwa.
Bodi hiyo bado imeonekana kuwa na kigugumizi cha kupanga tarehe ya mechi hiyo, kufuatia Yanga kupeleka malalamiko katika Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo Duniani (CAS).
Tayari CAS hivi karibuni ilitoa siku 10 kwa walalamikiwa kuwasilisha utetezi wao, baada ya Yanga kupeleka rufaa yao kuhusiana na kile kilichotokea Machi 8.
Mchezo wa Simba na Yanga una umuhimu mkubwa, kuchezwa kwa sababu huenda ndio ukawa mchezo utakaompata bingwa wa Ligi Kuu msimu huu.
Hiyo itatokea endapo Simba na Yanga wote wakaendelea kushinda bila kupoteza pointi yoyote, hadi watakapokutana wenyewe kwa wenyewe.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.