Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Maslahi yalivyotibua safari ya Extra Musica

Kundi la Extra Musica Kundi la Extra Musica

Dar es Salaam

Na Arone Mpanduka

Bendi ya Extra Musica ambayo ilitamba sana zamani, ilianzishwa mwaka 1993 jijini Brazzaville, Jamhuri ya Congo, ikiasisiwa na wanamuziki akina Ibabi Okambi Rogatien ‘Roga Roga’, ambaye ni mahiri kwa kulicharaza gitaa la solo. Aidha, Roga Roga ndiye kiongozi wa kundi hilo hadi sasa.
Muasisi mwingine ni Espe Bass, ambaye ni muungurumishaji wa gitaa la besi. Mwaka 1995, wanamuziki wa bendi hiyo waliachia albamu yao ya kwanza ya Nouveaux Missiles, iliyowatambulisha vyema kwenye ulimwengu wa muziki.
Albamu hiyo ilipambwa na nyimbo nyingi kali, hususan ule Fred Nelson. Wanamuziki walioshiriki kwenye albamu hiyo, mbali na Roga Roga na Espe Bass, ni pamoja na Guy Guy Fall, Quentin Moyascko, Oxygen Mbon Slyvain, Dou Dou Copa ‘Elenga Laka Bienvenu’, Dominique, Christian na Herman Nagasaki, ambao wote ni waimbaji, pamoja na kunengua.
Wanamuziki wengine walikuwa akina Killa Mbongo aliyekuwa ‘rapa’, Durell Loemba, ambaye ni mcharazaji wa gitaa la rhythm. Kwa upande wa uchanganyaji ‘drums’, yupo Ngolali G’Ramatoulaye na Christian Kingstall aliyekuwa anabofya kinanda.
Wanamziki wa bendi hii ya Extra Musica walijizolea sifa lukuki, wakapendwa na wapenzi wengi kwa jinsi walivyo wajuzi katika kulishambulia jukwaa wakinengua katika maonesho yao yote, ikiwahusisha wanamuziki wenyewe kunengua, tofauti na bendi nyingine ambazo hutumia wanenguaji wa kike.
Ndiyo sababu wao walipenda kujiita ni La Difference, yaani, ni wa tofauti.
Kwenye albamu hiyo ya kwanza, kulikuwa na wanamuziki wengine ambao hawakupata nafasi ya kurekodi, wakiwemo akina Pinochet Thierry, Regis Touba, Cyrille Molanga na Arnaud Luguna.
Albamu hiyo ya Nouvoeaux Missiles, ilisababisha wanamuziki wengine nje ya bendi yao kuvutiwa nayo, mmojawapo alikuwa Samba Brice Abillissi, aliyeamua kujiunga nao.
Albamu ya pili ya Confirmation ya mwaka 1996, ilipelekea kundi hilo kuzidi kutikisa vilivyo, hadi wakapata mialiko mingi barani Afrika na Ulaya.
Inaelezwa kuwa albamu hiyo ya Confirmation iliuza nakala nyingi mno kuzidi ile ya mwanzo.
Lakini mafanikio hayo yalisababisha kuzuka kwa mgogoro mkubwa wa kimasilahi, hali iliyofanya baadhi ya wanamuziki wake wakiwamo akina Christian na Guy Guy Fall, kujiondoa kundini, japokuwa kuondoka kwa wanamuziki hao, Extra Musica iliendelea kuwa imara.
Ilipotoka albamu ya tatu ya Ouragan mwaka 1997, wanamuziki Herman Nagassaki na Samba Brice Abilliss, waliziba vilivyo mapengo ya Guy Guy Fall na Christian.
Mgogoro wa chini kwa chini ulikuwa ukifukuta miongoni mwa wanamuziki wa bendi hiyo, na uongozi. Baadhi ya wanamuziki walishindwa kuvumilia, wakaihama bendi hiyo. Wanamuziki hao walikuwa ni Arnaud Laguna, Quentin Mayascko, Durell Loemba, Cyrille Malonga, Regis Touba na Pinochet Thierry.
Wakaenda kuunda kundi lao jingine walilolipa jina la Z.I. International, chini ya uongozi wa Cyrille Malonga, Regis Touba, Pinochet Thierry na Durrell Loemba.
Baada ya bendi ya Extra Musica kukimbiwa na wanamuziki hao, walikaa chini na kuamua kuwatafuta wanamuziki wengine vijana wenye vipaji vikubwa.
Walifanikiwa kuwapata vijana hao akina Gildas Pozzi, na Emery Mboma. Wakati huo huo, Sonor alichukua nafasi ya ucharazaji wa gitaa la rhythm lilokuwa likishikwa na Durell Loemba.
Mara baada ya kuwaingiza vijana hao kundini, mwaka 1998 waliachia albam yao ya nne ya Extra Major. Albamu hiyo ilivunja rekodi ya mauzo ya albamu zote za awali na kuwaletea tuzo nyingi Barani Afrika, ikiwemo ya Kora kwa kuteuliwa kuwa bendi bora ya muziki katika Bara la Afrika.
Mwaka uliofuatia, waliachia albamu nyingine tano zilizokuwa kali mno.
Kati ya albamu hizo ile ya Shalai ilisababisha kuwapata wanamuziki wengine wakali, akina Papy Batin Maboulango na Boudouin Massipi.
Rapa wao wa kutumainiwa Killa Mbango, alijitoa kundini akaachana na muziki. Lakini baadaye alirejea kundini. Extra Musica, japo ilichukua kipindi kirefu kutoa albamu ya sita ya Trop C’Est Trop katika mwaka 2001.
Rapa mwingine alijulikana kwa jina la Arafat, nae alijiunga na bendi hiyo, akichukua nafasi iliyoachwa wazi kwa mara nyingine tena, na Killa Mbongo.
Baada ya kutoka na albamu hiyo, waliamua kubadilisha kidogo majina ya bendi yao ikaitwa Extra Musica Zagul.
Mara baada ya kutoa albamu ya saba ya Obligatoire mwaka 2004, mwimbaji wao Dou Dou Copa naye akajiondoa kundini, akafuatiwa na Oxygene mwaka 2005.Kuodoka kwa wanamuziki hao hakukuathiri Extra Musica Zagul, kwani waliachia albamu ya nane ya La Main Noire mwaka 2006, na nyingine ya tisa ya Sorcellirie ‘Kindoki’ katika mwaka 2011.
Licha ya hekaheka nyingi, bendi ya Extra Musica ilisimama tena na kwa sasa muasisi Roga Roga bado anakomaa na kundi la Extra Musica Original, huku wimbo wa Bokoko uliotoka mwaka 2021, ukiendelea kuwa maarufu.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.