Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Askofu Msimbe awapa Mapadri angalizo

MOROGORO

Na Angela Kibwana

Mhashamu Askofu Lazarus Msimbe -SDS, wa Jimbo Katoliki la Morogoro, ametoa wito kwa Mapadri kutohubiri Injili ya mafanikio, kwa sababu kuna desturi ambayo inataka kuzuka hata ndani ya Kanisa Katoliki, kwa sababu baadhi ya waamini kutaka miujiza na mafanikio, hali inayosababisha baadhi yao kuhamia Makanisa mengine.
Askofu Msimbe alisema hayo katika mahubiri wakati wa kutoa Daraja la Upadre kwa Mashemasi wanne wa Shirika la Wasalvatorian, iliyofanyika Chuo Kikuu Kishiriki cha Jordan, Jimboni Morogoro.
Aidha, Askofu Msimbe alisema kuwa Mapadri wanapaswa kuhubiri Injili ya Yesu, ambayo si Injili ya kutaka mafanikio. Hivyo, ni kazi ya Mapadri kuwaeleza waamini ukweli, kwamba hakuna mafanikio yanayoweza kujitokeza bila kuvuja jasho, au kufanya kazi kwa bidii.
 Alisema kuwa kutokana na desturi iliyozuka kwa waamini wengi kutekwa na injili ya miujiza na mafanikio, Askofu Msimbe ametumia nafasi hiyo kuwatahadharisha Mapadre kutojihusisha na mitego ya kudanganya watu kukanyaga waamini wao, kukanyaga mafuta ya upako, kwa kigezo cha kujipatia utajiri.
Alibainisha kuwa Mapadri wanatakiwa kuwahubiria watu ukweli kwamba kuna mateso katika safari ya kutafuta mafanikio, waamini wanahitaji kufundishwa mbinu bora za kuwa na mipangilio mizuri, kwa sababu hakuna mtu anayeweza kupata mafanikio kwa njia rahisi.
Hata hivyo aliwaonya Mapadri, kutozigeuza Baraka zao kuwa biashara kwa sababu wamepewa bure ili kuwahudumia watu. Wasiuze baraka zao, jambo la msingi kwao ni kuhakikisha wanahubiri injili ya Yesu ambayo haitaki ulaini katika maisha.
Mapadri wanapaswa kutambua kuwa wao ni mbegu ambayo inapaswa kumea vizuri kwa kufanya mambo yampendezayo Mungu, kwani ni kielelezo katika kuyaenzi matakatifu, kwa kuwa kazi moja na muhimu ya mapadri ni kuhubiri Neno la Mungu, na wala siyo kujisifia wenyewe.
Alisema kuwa maadhimisho ya Sakramenti mbalimbali za Kanisa ndiyo dira inayoweza kumtambulisha Padre. Mapadre waepuke tabia ya kujisifia wenyewe, hivyo watu watatambua uzuri wa Padre kulingana na huduma makini kwa watu wake, hasa uadhimishaji wa Misa Takatifu.
Katika kuadhimisha Masakramenti, hasa Sakramenti ya Kitubio, Mapadri wanapaswa kuwa makini kuwatia moyo waamini wanapofanya kitubio ili kuwapatanisha na Mungu, na wala waamini wasikatishwe tamaa.
Sambamba na hayo, amewaomba mapadre hao wapya kushiriki maisha ya Jumuiya na kuziishi karama za Shirika la Wasalvatoariani, waishi kadri ya nadhiri zao kwa kuzingatia mambo ya msingi yanayowatambulisha kuwa WATAWA.
Wanapaswa kuzingatia maisha ya sala ambayo yatawasaidia kutimiza mapenzi ya Mungu na kufanya utume watakaopangiwa na wakubwa wao wa shirika, ili watekeleze kwa uaminifu na kwa uangalifu.
Aliwaomba waamini na watu wenye mapenzi mema kuwaombea Mapadri wapya na wengine waliotangulia katika utumishi huo kuwa wafuasi wema wa Kristo, ili kuwavuta vijana wengi wanaotamani kujiunga na wito huo Mtakatifu.
Mapadre wapya ni Padri Edward Lupaka, Padri Deogatius Silayo, Padri Erasmus Kayongo, na Padri Musa Ndelule.

Rate this item
(0 votes)
Last modified on Friday, 02 September 2022 08:50
Super User

Selfies labore, leggings cupidatat sunt taxidermy umami fanny pack typewriter hoodie art party voluptate. Listicle meditation paleo, drinking vinegar sint direct trade.

www.themewinter.com

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.