Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Tozo zatumika ujenzi Kituo cha Afya Morogoro

Ujenzi wa Kituo cha Afya cha kisasa katika Kata ya Lukobe, Mkoani Morogoro ukiendelea.

MOROGORO

Na Angela Kibwana

Serikari ya Tanzania imetoa Shilingi milioni 500/- zilizotokana na tozo za miamala ya simu, kukamilisha mradi mkubwa wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha kisasa katika Kata ya Lukobe, Mkoani Morogoro.
Kukamliki kwa mradi huo kutawanufaisha zaidi ya wananchi 35,000 watakaopata shida za kiafya kutoka Kata ya Lukobe na Kata jirani, Mkoani humo.
Akizungumza wakati wa kukagua mradi huo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Ally Machela alisema kuwa tayari Serikali imetoa shilingi milioni 500/= zilizopokelewa na Manispaa ya Morogoro kukamilisha ujenzi wa kituo hicho.
“Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro inatekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kata ya Lukobe kitakachohudumia wananchi 35,000 baada ya kukamilika kwake,”alisema Machela.
Alifafanua kuwa fedha zilizotolewa katika awamu ya kwanza ambazo ni kiasi cha Shilingi milioni 250/=, zilitumika kujenga maabara,jengo la wagonjwa wa nje, na kibanda cha kuchomea taka.
Aidha, alifahamisha kuwa katika awamu ya pili, Serikali ilitoa Shilingi milioni 250/- kwa ajili ya majengo mawili ambayo ni jengo la wazazi, jengo la kufulia nguo, na jengo la upasuaji.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro Dk. Charles Mkombachepa, alisema kuwa kituo hicho cha afya kitaongeza tija kwa wananchi kwa sababu kina uwezo wa kuhudumia watu 35,000 kutoka Kata ya Lukobe, Mkundi, Kihonda na Kata nyingine jirani.
Aliongeza kuwa kituo hicho kina majengo mbalimbali ya kutolea huduma kwa wagonjwa, kati yao kuna jengo la wanawake; jengo la wagonjwa wa nje; jengo la wazazi; jengo maalum kwa ajili ya upasuaji wajawazito; na huduma nyingine za afya ya mwanamke.
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood, baada ya kuridhishwa na ujenzi wa kituo hicho, aliahidi kutoa magari mawili yenye thamani ya Shilingi milioni 172/- kubebea wagonjwa  katika Kituo cha Afya Lukobe, na Kituo cha Afya Tungi kinachojengwa  kwa mapato ya ndani ya Manispaa.
Nao baadhi ya wakazi wa Kata ya Lukobe walisema kuwa wanamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha ili kukamilisha ujenzi huo.
Naye Mwandishi Victor Wambura anaripoti kuwa, wasomi nchini wameiomba Serikali kutimiza ahadi yake kwa wananchi kwa kuzielekeza tozo ili kuboresha miradi ya maendeleo ya jamii, hivyo kuondoa malalamiko ya wananchi kuhusu tozo hizo.
Akizungumza na gazeti la Tumaini Letu, Mchumi na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar salaam (UDSM) Dk. Martin Chegere, alisema kuwa hakuna tozo yoyote itakayomfurahisha mtu, na hakuna mtu anaependa kitu kinachomchukulia pesa yake, ikiwa hakipo kwenye matumizi yake.
“Tumeahidiwa kwamba vikichukuliwa basi vitarudi kwa mfumo utakaotusaidia kuweka mazingira mazuri ya afya, elimu na miundombinu, hizo ndizo ahadi tulizoahidiwa na viongozi wetu,” alisema Dk. Chegere.         
Alisema pia kuwa Serikali inatakiwa kuwatendea watu haki, kulingana na ahadi ya kuboresha miundombinu ya kijamii, kwa sababu wananchi wanaumia wakiona vitu hivyo havitendeki, hasa kwa kutumia kodi hiyo ya tozo.
Aidha, Dk. Chegere alisema kwamba usahihi wa tozo utakuwepo pale ambapo Serikali itarejesha kwa wananchi kwa namna bora zaidi ya kuwapatia huduma.
Aliwasihi wananchi kuiunga mkono Serikali, kwani hata kwenye Bibilia Takatifu, Yesu aliwaambia wanafunzi wake kuwa ya Kaisari mpe Kaisari na ya Mungu mpe Mungu, ikiwa na maana ya kwamba serikali nayo inahitaji mapato.
Naye Mchumi na Muhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar esalaam Dk. Innocent Pantaleo, alisema kuwa Wananchi wanatakiwa kuiunga mkono Serikali kwa kukusanya mapato, na kudai kwamba kwa sasa wahisani hawaleti pesa za kutosha kama ilivyokuwa awali.
Aidha, Dk. Pantaleo aliiomba Serikali kuzingatia usawa kwa kumwangalia mwananchi mwenye kipato cha chini, ili kuondoa matabaka.
Hata hivyo, alisema Serikali izingatie kuboresha maeneo ambayo yanamgusa huyo mwananchi anaetozwa kodi kwa kuboresha miundombinu ya kijamii, kama vile ya afya, elimu na miundombinu, kwani hicho ndicho kilio cha wengi.

Rate this item
(0 votes)
Last modified on Friday, 02 September 2022 09:29
Super User

Selfies labore, leggings cupidatat sunt taxidermy umami fanny pack typewriter hoodie art party voluptate. Listicle meditation paleo, drinking vinegar sint direct trade.

www.themewinter.com

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.