Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Wadau wa soka tusikimbize kuku mweusi gizani

Na Arone Mpanduka

Hivi karibuni tumeshuhudia Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) likimtimua kocha wa timu ya taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen, baada ya kutoridhishwa na mwenendo wake ikiwemo Taifa Stars kupoteza kwenye mchezo wa nyumbani wa kuwania tiketi ya kufuzu fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani.
Wapo watu walioshangaa, na wapo walioona kuwa maamuzi yaliyofanywa ni sahihi kwa sababu kocha haajiriwi ili afukuzwe hasa kama ikitokea kushindwa jukumu alilopewa.
Kwa miaka mingi sasa tumekuwa tukiajiri makocha kwa timu ya taifa na kisha kuwatimua, huku tukiwashushia lawama nzito kwamba wao ndiyo sababu kuu ya timu zetu kushindwa. Mwaka 2006 Rais Jakaya Kikwete kwa wakati ule, alituonyesha njia kwa kumleta kocha wa kigeni Marcio Maximo kutoka nchini Brazil, na hapo ndipo tukawa tunaamini moja kwa moja kwamba suluhisho kuu la timu zetu za taifa kufanya vizuri ni kuajiri makocha wa kigeni.
Ninadhani kuna mahali tunakwama, na pengine hatufahamu suluhisho lake, na hata kama tunalifahamu, tunaamua kujifanya hatufahamu. Unapofanya jambo ambalo hujui, unakwenda wapi na ukaendelee kulilazimisha, itakuwa sawa na kufukuza kuku gizani, ukidhani utamkamata.
Ukweli ni kwamba mafanikio ya timu zetu za taifa yamekuwa yanapatikana kwa kubahatisha, na si katika mifumo sahihi. Bado tunaogopa kuanza na sifuri ili twende mbele, na badala yake tunataka kulazimisha, tukiamini kwamba tutafika tunapopataka.
Kuna vitu havipo sawa, na inabidi turekebishe ili soka letu lifike tunapopataka.Na vitu hivyo vinaanzia katika ngazi ya familia, Serikali na vyombo vinavyohusika na mchezo wa soka.
Tatizo kubwa tulilonalo ni kutokuwa na mfumo bora wa kufikia mafanikio ya mpira wa miguu, vinginevyo tutaishia kuilaumu TFF na makocha wanaokuja kufundisha timu zetu.
Tukianzia ngazi ya familia, wachezaji wote waliopo wana wazazi au walezi wao. Je, nini mchango wao katika malezi ya kimwili na kisaikolojia kwa watoto wao? Kwa sababu leo hii tunaweza kuwa na wachezaji wazuri wazawa lakini hawana nidhamu.
Kitu ambacho ni muhimu kwa maisha ya mchezaji kinachoweza kumpeleka nje ya nchi kucheza soka la kulipwa, na hatimaye kuongeza ubora kwenye timu za taifa, ni ufundi au umahiri wa kucheza soka.
Jambo lingine katika familia ni suala la lishe bora. Je, umewahi kujiuliza ni kwa nini wachezaji wa kizazi hiki wana maumbo madogo madogo, ikilinganisha na wale wa miaka 30 iliyopita? Wazazi katika hilo wanahusikaje?
Ukija katika ngazi ya klabu, je, vilabu vyetu vinaendeshwa kwa weledi, kwa maana ya kuandaa timu zetu za wakubwa? Kuna uwekezaji wa kiwango gani katika miundo mbinu ya soka?
Kwa sababu ukichunguza kwa makini utabaini, kwamba klabu chache za Ligi Kuu zina mifumo mizuri ya kutengeneza vijana, lakini zingine hazina, na hata yakitokea mashindano ya vijana, wanachofanya ni kuokota vijana wa mitaani ili kuiridhisha TFF.
Tukija kwa Serikali, je, kuna viwanja vingapi vya wazi ambavyo vilikuwa vinatumika kwa michezo zamani, lakini sasa hivi vimegeuzwa kuwa ofisi za watu binafsi, gereji, shule ama baa? Na katika hilo hilo la viwanja, ni shule ngapi za umma za Msingi na Sekondari zina viwanja vye michezo? Watoto watacheza wapi? Vipaji tutaviibua wapi? Na hapo ndipo msingi wa soka wa nchi yoyote unapoanzia.
Je, kuna waalimu wangapi wa michezo waliofuzu kwenye eneo hilo katika shule zetu za umma za msingi na sekondari, na je, kuna shule ngapi zenye vipindi na ratiba za michezo kama ilivyokuwa zaidi ya miaka 40 iliyopita?
Majibu ya jumla ni kwamba kwa sasa hakuna maeneo mengi ya wazi, na hata shule nyingi za umma ninazoziona mitaani hazina viwanja vya kuchezea. Mfano mzuri ni Shule ya Msingi Tabata Liwiti, ambayo ipo jirani kabisa na ofisi za Tumaini Media ambayo uwanja wake wa soka linajengwa jengo la Shule ya Sekondari. Pongezi kwa kuweka jengo hilo, lakini watoto watachezea wapi?
Hapo Wizara husika na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) wanapaswa kutengeneza na kusimamia mfumo ulio bora ambao ndio utakuwa muongozo wa nchi. Nilisikia sera ya michezo inakamilishwa, lakini bado sifahamu ilipofikia.
Itaendelea wiki ijayo.

Rate this item
(1 Vote)
Last modified on Friday, 02 September 2022 09:16
Super User

Selfies labore, leggings cupidatat sunt taxidermy umami fanny pack typewriter hoodie art party voluptate. Listicle meditation paleo, drinking vinegar sint direct trade.

www.themewinter.com

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.