Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Kardinali Pengo awaasa vijana

DAR ES SALAAM

Na Laura Chrispin

Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es salaam amewaasa Vijana 129 waliopokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara kuishi katika viapo walivyoweka kwa Mungu kwa ajili ya kazi ya kuhubiri Injili kwa mataifa.
Alitoa wosia huo hivi karibuni wakati wa homilia yake katika adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara katika Parokia ya Mtakatifu Maria Faustina, Lulanzi-Kibaha, Jimboni humo.
“Inawapasa mtambue kuwa mkiishi vyema, ahadi zenu mlizo weka kwa Mungu, basi tambueni mtapewa uwezo wa kujua na kutambua lile analolitaka Mwenyezi Mungu kwa wakati na kwenye mazingira ya wakati huo”Alisema Kardinali Pengo
Aliwataka Waamini watambue Pentekoste ya kwanza ya Mitume, ambao walipewa uwezo wa kuhubiri injili kwa mataifa bila ya uwoga na wasiwasi, hata Mwinjili Yohane anasimulia kuwa Mitume walikuwa wakijificha ndani kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi, lakini waliposhukiwa na Roho Mtakatifu, uwoga uliondoka, kwani Roho huyo aliwafanya kuwa na ujasiri.
Kardinali Pengo alisema kuwa viongozi wa Kiyahudi hawakupenda na hawakutaka kusikia habari za Yesu na yeyote aliyekuwa akitangaza imani ya Kristo, alikuwa ni adui kwa viongozi hao.
Sambamba na hayo alisema jambo ambalo kwa sasa linatia hofu, ni kuhusu watu wanaopotea katika mazingira ya kutatanisha, na kesho yake kukutwa wameshauawa, na kwamba hali hiyo inawasukuma watu kujiuliza matendo kama hayo yanafanywa na nani.
Kardinali Pengo alisema kuwa hayo yanayotendeka ya watu kuuawa na mtu akijitokeza kusema ukweli naye anauawa ndiyo sababu ya watu wengine kuogopa kusema ukweli, na kuwataka Waimarishwa wazidi kumwomba Roho Mtakatifu awatoe hofu katika kufanya kazi zao, na kuwataka wamtumie vyema Roho wa Mungu.
Pia, aliwataka Waamini wote watambue kuwa chimbuko la maafa yote ni dhambi, na wakati mwingine dhambi hizo ni katika kutafuta utajiri, au ukosefu wa imani, wazazi kwa watoto wao kwa kutambua kuwa watoto wao ni chimbuko la Utajiri.
Kardinali Pengo aliwataka Waamini wajitahidi kuishi bila dhambi na kushuhudia imani huku wazazi na walezi wakiwaombea vijana wanaopokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara ili waweze kuishi imani yao na kutangaza habari njema ya wokovu bila uwoga.
Vilevile aliwataka waamini kuwakumbusha vijana hao mambo yote watakayo yaahidi na kuwasaidia kwa kukaa nao siku zote za maisha yao ili wasisahau kumuomba Mungu awasimamie katika vita yao ya kupambana na dhambi.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.