Baadhi ya Vijana waimarishwa katika Parokia ya Watakatifu Wote Kiluvya, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara parokiani hapo. (Picha na Yohana Kasosi)
Paroko wa Parokia ya Watakatifu Wote Kiluvya Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Justus Rugaimukamu, akiwabariki waamini waliotoa Zaka wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara parokiani hapo hivi karibuni. (Picha na Yohana Kasosi)
Baadhi ya Vijana walioimarishwa kwa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara katika Parokia ya Mtakatifu Andrea Mtume, Bahari Beach, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu parokiani hapo. (Picha na Yohana Kasosi)
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu (katikati) na Padri Danipaso Bitegeko, Paroko wa Parokia ya Watakatifu Wote Kiluvya (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Familia ya Mzee Tumaini Makwesa, baada ya Adhimisho la Sakramenti ya Kipaimara parokiani hapo hivi karibuni. (Picha na Yohana Kasosi)
Wanaume Katoliki Uwaka wa Parokia ya Mtakatifu Dominico, Mbezi Juu Jimbo Kuu la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Uwaka Day parokiani hapo hivi karibuni. (Picha na Yohana Kasosi)
Askofu wa Jimbo Katoliki la Bunda, Mhashamu Simon Masondole, Mapadri, Viongozi wa Halmashauri ya Walei Parokia na Kigango, wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali Venance Mabeyo (kushoto kwa Askofu), baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, sanjari na Harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Kigango cha Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu – Kilimahewa Juu, Parokia ya Mtakatifu Agostino – Salasala, Jimbo Kuu la Dar es Salaam. (Picha na Mathayo Kijazi)
Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu kwenye viwanja vya Seminari ya Mtakatifu Maria, Visiga-Kibaha mkoani Pwani walipopeleka majitoleo yao kuwategemeza Waseminari. (Picha na Michael Ally)
Vijana wa Parokia ya Mtakatifu Nicholaus – Kunduchi, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika maandamano ya kuingia kanisani kwa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara. (Picha na Mathayo Kijazi)
Kwaya Shirikisho ya Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) Jimbo Kuu la Dar es Salaam wakiimba wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu shukrani kwenye viwanja vya Seminari ya Mtakatifu Maria, Visiga-Kibaha jimboni humo walifanya hija ya kuitegemeza Seminari hiyo.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu (aliyeshika fimbo ya kichungaji) akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri, Sista mlezi, Viongozi wa Parokia na watoto waliopokea Komunio ya Kwanza katika Parokia ya Mtakatifu Andrea Mtume, Bahari Beach jimboni humo. Kushoto kwa Askofu ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Marco Loth. (Picha zote na Yohana Kasosi)
BOURNEMOUTH, Uingereza
Bournemouth wamekubali mkataba wa mkopo wa msimu mzima kwa mlinda mlango wa Chelsea, Kepa Arrizabalaga.
Uhamisho huo unatarajiwa kumaliza nia ya Bournemouth kwa mlinda mlango wa Arsenal Aaron Ramsdale, lakini pia Kepa, 29, pia ameongeza mkataba wake Stamford Bridge hadi mwisho wa msimu wa 2026.
Mkataba wake ulitarajiwa kukamilika Juni 2025, ambao ungemruhusu kuondoka Chelsea kwa uhamisho wa bure mwishoni mwa muda wake wa mkopo na Chelsea.
Kepa anasalia kuwa kipa ghali zaidi duniani kuwahi kuhamia The Blues mwaka 2018 kutoka klabu yake ya utotoni, Athletic Bilbao, kwa £71m.
Amekuwa akifanya mazoezi, pamoja na wachezaji wengine 14, mbali na kikosi cha kwanza cha meneja Enzo Maresca, na inaaminika kuwa hana mustakabali Stamford Bridge.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania alitumia msimu uliopita kwa mkopo Real Madrid, ambapo alicheza mechi 20 kama mbadala wa Thibaut Courtois aliyejeruhiwa, akishinda La Liga na Ligi ya Mabingwa.
LONDON, Uingereza
Mipango ya Kituo cha Tenisi karibu na mji wa Sir Andy Murray wa Dunblane, imefutwa kutokana na masuala ya kupanga na kupanda kwa gharama.
Mradi wa (£20m), ulioongozwa na mama yake Judy Murray, ulilenga kujenga jumba la jamii la michezo mingi katika Park of Keir, kuashiria urithi wa tenisi wa familia ya Murray.
Chama cha Tenisi cha Lawn (LTA) kiliahidi pauni milioni 5 kwa mradi huo lakini kilikutana na upinzani kutoka kwa wanakampeni ambao walisema haupaswi kujengwa kwenye ardhi ya ukanda wa kijani.
Shirika la hisani la Judy Murray, Murray Play Foundation, lilisema, “Kwa masikitiko makubwa na huzuni,” sasa halitaendelea.
Ongezeko kubwa la gharama za ujenzi na nishati, mchakato wa upangaji wa muda mrefu na mijadala inayoendelea na bodi zinazosimamia, zilitajwa kuwa sababu za kuuacha mradi huo.
DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Mwaka 2024 unaendelea kushuhudia tasnia ya muziki nchini Tanzania ikiendelea kushamiri, huku wasanii wakizidi kujipatia umaarufu na utajiri mkubwa.
Muziki wa Bongo Flava umevuka mipaka ya Afrika Mashariki, ukiwavutia mashabiki lukuki duniani kote.
Kupitia vipaji vyao vya kipekee na bidii katika kazi zao, baadhi ya wanamuziki wamefanikiwa kujikusanyia utajiri mkubwa wa kutikisa.
Taarifa zinadai kuwa orodha hii ya wasanii matajiri zaidi Tanzania mwaka 2024, na kuufanya muziki wa Tanzania kupata thamani sokoni, na hivyo kuzibwaga nchi nyingi za jirani kutopata mpenyo.
Diamond Platinumz,
Nasibu Abdul Juma almaharufu kama Diamond Platnumz au Simba wa WCB anaendelea kutamba kileleni mwa orodha ya wasanii matajiri zaidi Tanzania.
Utajiri wake unatokana na muziki wake unaoendelea kutikisa pande mbalimbali za Afrika na Dunia kiujumla mathalan katika biashara mbalimbali, ikiwemo lebo yake ya WCB, uwekezaji katika mali isiyohamishika, na mikataba kibao ya matangazo.
Maisha yake ya kifahari yamekuwa yakionekana kupitia magari yake ya kifahari, nyumba za kifalme, na safari kwenda nchi za kigeni.
Juma Jux
Juma Mussa Mkambala almaharufu kwa jina la kisanii kama Juma Jux amejizolea utajiri mkubwa kupitia muziki wake unaovuma, hasa nyimbo zake za mapenzi zinazogusa hisia za wengi.
Uwezo wake wa kuandika nyimbo zenye mashairi ya kuvutia na sauti yake tamu vimemfanya kuwa mmoja wa wasanii wanaotafutwa sana Tanzania.
Jux amekuwa miongoni mwa wasanii wanaoishi maisha ya kifahari nchini Tanzania, uku akishuhudiwa kumiliki imagari ya kifahari mbalimbali, ikiwemo Mercedes Benz E-Class ya mwaka 2021, ambayo gharama yake ni zaidi ya dola elfu 53 bila ya kodi ambazo ni karibia shilingi milioni 160 za Kitanzania.
Harmonize
Konde Boy, Harmonize, amejipatia nafasi ya tatu katika orodha hii kutokana na muziki wake unaopendwa na mamilioni, lebo yake ya Konde Music Worldwide, na biashara zake nyingine, ikiwemo ya Redio.
Ubunifu wake katika muziki na mtindo wake wa kipekee, umemfanya kuwa miongoni mwa wasanii wanaolipwa pesa nyingi zaidi kwa show nchini.
Nafasi ya tatu ikifuatiwa na msanii Zuchu, Marioo, Nandi, Ommy Dimpoz, Rayvanny, Ali Kiba na Niki wa pili akimalizia nafasi ya kumi.
Muziki unalipa ukiiufanya kwa bidii na kwa ubunifu zaidi, kwani ni sehemu ya ajira ya vijana wengi kwa sasa nchini.
DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Uongozi wa klabu ya soka ya KMC umejitoa katika mbio za ubingwa msimu huu kutokana na kutokuwa na misuli ya kutosha katika kushindana na vilabu vingine.
Mtendaji wa klabu hiyo Daniel Mwakasungura alisema kuwa bado wanaendelea kujitafuta, huku akiweka wazi kuwa bado hawapo katika ramani za waokupambana na wenye uwezo wa kifedha .
Mwakasungura alifunguka kuwa wameliona hilo kwa mwaka huu, na kuamua kuijenga timu yao ili ikishakuwa sawa, waanze kupambana kwa misimu mingine ya ligi huko baadaye lakini kwa sasa bado hawana wachezaji wenye uwezo wa kiushindani.
Alisema kuwa kwenye upande wa soko la usajili, wenzao wamewaacha mbali sana kuliko wao, kwani gharama ambazo wanatumia vilabu vingine katika kusajili wachezaji, ni kubwa kuliko za wao, na hivyo kusababisha hata kupokonywa wachezaji wengi wzuri.
“Unajua kwenye soko la ushindani unatakiwa ujitutumue kweli sasa sisi tunamuona mchezaji, na tunatamani kumsajili lakini unakuta fedha tunayotoa ni ndogo kuliko ambayo wenzetu wakiamua kuitoa kwa mchezaji huyo huyo”, alisema Mwakasungura.
Alisema pia kuwa kwa sasa wao wanajenga timu ili iwe tishio kwa miaka inayokuja, kwani tayari wameshaanza kujipata katika namna ya uchezaji, hivyo vimebaki vitu vichache ambavyo wao kwa kusaidiana na bechi la ufundi, wanavitengeneza.
KMC msimu uliopita ilibaki kidogo kushuka kwenda kucheza Ligi ya Championship, lakini walijipapatua na kuendelea kubaki katika Ligi Kuu. Kwa msimu, na sasa wanachokifanya ni kujihakikishia nafasi ya kutoshuka Daraja ili malengo yao ambayo waliyaweka, yaweze kutimia.