Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Waamini waombwa kuzingatia Liturjia

Mwenyekiti wa Tume ya Kichungaji, Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Malawi, Mhashamu Martin Anwel Mtumbuka (wa pili kulia), akiongoza sherehe ya Jubilei ya Shirika la Wanawake Wakatoliki nchini humo. Mwenyekiti wa Tume ya Kichungaji, Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Malawi, Mhashamu Martin Anwel Mtumbuka (wa pili kulia), akiongoza sherehe ya Jubilei ya Shirika la Wanawake Wakatoliki nchini humo.

LILONGWE, Malawi

Mwenyekiti wa Tume ya Kichungaji Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Malawi, Mhashamu Martin Anwel Mtumbuka, amewataka Wakatoliki kuzingatia na kufuata Liturjia katika Madhimisho ya Misa Takatifu.
Mhashamu Mtumbuka ambaye pia ni Askofu wa Jimbo Katoliki Karonga, Lilongwe nchini humo, alisema kuwa hatua yake ya kuwasimamisha washiriki kwa muda kusoma nia ya maombi wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu kwa ajili ya Shirika la Wanawake Wakatoliki mjini, ililenga kuwafundisha waamini kuheshimu agizo la Misa.
Waandaji wa hafla hiyo walipanga safu ya maombi yanayohusu nyanja zote za maisha ikiwa ni pamoja na kuliombea Kanisa la Ulimwengu, Kanisa la mahali, viongozi wa kisiasa, watoto na vijana lakini kwa lugha mbalimbali za kienyeji kwa lengo la kuonyesha kwamba Kanisa linaunganisha Wamalawi wa tamaduni na lugha mbalimbali.
Baada ya maombi hayo kufanywa kwa lugha ya kwanza ‘ndogo’, badala yake waliitikia kwa utaratibu, baadhi ya waamini walipiga makofi na kufoka, jambo lililomkera Askofu Mtumbuka na kurekebisha hali hiyo mara moja.
“Ndugu hawa wanawake wanaomba Mungu, na siyo wewe. Acha kelele na kupiga makofi kwa maana bado tuko kwenye Misa. Waache watuombee kwa niaba yetu kwa utaratibu,” alishauri, na maombi yaliendelea kwa lugha nyingine.
“Kwa niaba ya Maaskofu wenzangu, nataka niwaelekeze kwamba kuanzia sasa na kuendelea, hatutaki kuona tena tulichokiona leo. Najua bado tuna kazi nyingi za kitaifa mbele yetu na tutakuwa waangalifu sana...;
“Tumechoshwa na hili, na mimi binafsi sitakaa na kutazama maingiliano yasiyo ya lazima wakati wa Misa. Tunapokuwa na watu wanaosali kwa lugha zao za kitamaduni wanamwomba Mungu, tuweke mazingira ya namna hiyo ambayo yanafaa kwa maombi kila wakati,” alisema Askofu Mtumbuka.
Kwa upande wao Chama cha Wanawake Wakatoliki nchini Malawi, kilisema kuwa mwongozo uliotolewa na Askofu Mwenyekiti wa Tume ya Kichungaji na kubahatika kumpata Rais wa zamani wa shirika hilo ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya Umoja wa Wakatoliki Duniani, Lucy Jocelyne Vokhiwa, utasaidia kuwapa mwelekeo mzuri katika sala.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.