Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (Tanzania Football Federation:TFF), Wallace Karia amesema kuwa wapo kwenye mchakato wa kuongeza idadi ya makocha katika timu ya Taifa Stars ili iweze kufanya vizuri.
Taifa Stars kwa sasa inasubiri upangaji wa timu(team draw) ya kujua kundi gani litakalokuwa la wapinzani watakaokutana nao katika fainali za Afrika zitakazofanyika kuanzia Januari 13 hadi Februari 11 mwakani 2024, nchini Ivory Coast.
Akizungumza na Kituo cha Redio cha UFM jijini Dar es salaam kwenye mahojiano maalum, Karia alisema kwamba wamepanga kufanya maandalizi makubwa ili Tanzania ifike mbali katika fainali hizo.
Alisema pia kuwa timu hiyo ina makocha wasaidizi wakiongozwa na Adel Amrouche, lakini kuna ulazima wa kuwa na benchi pana la ufundi, kama zilivyo timu za mataifa mengine.
“Tunaamini na Serikali itatusaidia katika eneo hili muhimu.Tunataka tupate wataalamu wa kutosha.Unakuta wenzetu benchi lao la ufundi lina wataalamu 15, na kila mmoja anafanya majukumu yake.Kwa kuwa tunakwenda kushindana na watu wa ngazi ya juu, tunataka walau tuwe na makocha saba,”alisema Karia.
Alisema pia kwamba wanataka hadi kufikia kwenye mechi za kalenda ya Federation of International Football Assocation(FIFA) za mwezi Oktoba, timu iwe na benchi pana la ufundi, na kwamba tayari hao makocha wapo, na kilichosalia ni kuwasainisha tu mikataba.
Alisema pia kwamba kuna makocha wengine walishaanza kuonekana kwenye benchi hilo, ingawa wamekuwa kama wanajitolea. Hivyo mipango ikikamilika na wao kusainishwa mikataba, watakuwa tayari kutangazwa makocha wapya.
Akizungumzia maandalizi ya jumla kuelekea fainali hizo, Karia alisema kuwa wameshaongea na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ambayo imewataka kuwasilisha mpango mkakati wa maandalizi, ili waangalie sehemu ipi Wizara inaweza kuwaunga mkono.
“Mwezi Oktoba kuna mechi za Kalenda ya FIFA ambazo tutazitumia kuiandaa timu yetu, na mwezi Novemba kuna nafasi pia ya mechi za timu za taifa, nako pia tutaangalia uwezekano wa kuiandaa timu yetu kuelekea michuano hiyo ya Januari,”alisema Rais huyo wa TFF.
Katika fainali zake mbili za Afrika zilizopita za miaka ya 1980 na 2019, Stars iliishia hatua ya makundi, na kutolewa pasipo kuingia 16 bora.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi (kushoto), akibariki visakramenti wakati wa ziara yake ya Kichungaji aliyoifanya hivi karibni katika Kituo cha Hija, Pugu. (Picha na Yohana Kasosi)

Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme, Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Cornel Mashare (kushoto), na Mwenyekiti wa Parokia hiyo, Frederick Akilimali, wakionesha cheti cha shukrani kutoka kwa Askofu Mkuu wa Jimbo hilo, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi kwa kufanya vizuri katika kuitegemeza Tumaini Media mwaka 2023.

Mgeni rasmi katika Mahafali ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi Golden’light, jijini Dar es Salaam, John  Magwisha (kulia), akikabidhi zawadi kwa Gladness Jonathan (kushoto),  mmoja wa Waalimu wa shule hiiyo, wakati wa sherehe za Mahafali hayo zilizofanyika shuleni hapo. (Picha na Yohana Kasosi)

Baadhi ya Waamini wa Parokia ya Kung’ara kwa Yesu Kristo, Mbezi Mshikamano, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha na Yohana Kasosi)

Masista wanaofanya kazi za kitume kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Mahafali ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi ya Golden’light, Mbezi Mpigi Magohe, jijini Der es Salaam. (Picha na Yohana Kasosi)

Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari – Bombambili, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Sheejan Kallarakkal MSFS (mwenye kanzu nyeupe), akiwa katika picha ya pamoja na Wazee na Wastaafu, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Shukrani kwa Mungu kwa Wazee na Wastaafu wa Dekania ya Pugu, iliyoadhimishwa katika Parokia ya Bombambili. (Picha na Mathayo Kijazi)

Padri Dickson Sambala- O.CARM, akibariki vipaji wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu iliyofanyika Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli, Bunju, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, iliyofanyika parokiani hapo. (Picha na Yohana Kasosi)

Baadhi ya Waamini wa Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kuhitimisha Ziara ya Kuitembeza Sanamu ya Bikira Maria wa Fatima, iliyofanyika Parokia ya Mtakatifu Vincent wa Paulo, Vikindu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, na baadaye waliikabidhi kwa Jimbo Katoliki la Lindi. (Picha na Yohana Kasosi)

Mdau wa Tumaini Media, Anitha Kihwele na mumewe Joseph Kihwele, wakitabasamu baada ya kukabidhiwa cheti cha shukrani na Padri Cornel Mashare (kushoto), Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme, Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, kutokana na mchango wa Mama Kihwele katika kuhamasisha majitoleo ya tegemeza Tumaini Media. Cheti hicho kimetolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo hilo, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi. Nyuma yao ni Meneja Utawala Tumaini Media, Joseph Kessy.