Watoto wa Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sherehe ya Watoto Mashahidi iliyofanyika katika viwanja vya Parokia ya Kristo Mfalme, Tabata jimboni humo hivi karibuni.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi (aliyeshika Fimbo ya Kichungaji), Askofu Msaidizi wa Jimbo hilo, Mhashamu Henry Mchamungu (kushoto), Askofu wa Jimbo Katoliki la Bagamoyo Mhashamu Stephano Musomba (kulia) na Mapadri wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Shirika la Masista wa Mtakatifu Fransisko wa Asizi Dada Wadogo na Masista walioweka Nadhiri za Kwanza, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri hizo.
MWANZA
Na Paul Mabuga
Hebu vuta picha: Zamani kijana wa Kitanzania hakukurupuka tu kuitwa mzazi. Kulikuwa na mifumo madhubuti ya Jando, Unyago, na yale mafunzo ya kando ya moto kutoka kwa babu na bibi, yaliyomjenga mtu kifikra na kihisia.
Lakini leo, “moto” pekee unaowaunguza vijana wetu ni wa data za simu, na mianga ya mitandao ya kijamii. Wakati mifumo hiyo ya kijadi ikipumzika kwenye makaburi ya historia, tunapaswa kujiuliza kwa uchungu: Je, vijana wetu wanajifunza wapi kuwa wazazi?
Dar es Salaam
Na Joseph Mihangwa
Chimbuko la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Mapinduzi ya Zanzibar, yaliyofanyika Visiwani humo Januari 12, 1964.
Bila Mapinduzi hayo tusingezaliwa Tanzania, wala Chama tawala cha sasa - Chama cha Mapinduzi (CCM), ambacho ni Muungano wa Vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) cha Tanganyika, na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
Chama kilichozaliwa Februari 5, 1977, miaka 13 baada ya Muungano uliofikiwa Aprili 26, 1977, ni matokeo ya kero za Muungano.
Mapinduzi haya yaliyoshangaza dunia kwa staili yake, yalifanyika kwa harakati za siasa za mrengo wa Kikomunisti, na kutia hofu nchi za Magharibi, hasa Marekani na Uingereza, zikaamua kuingilia kati kuyadhibiti Mapinduzi hayo, kuzuia kuenea kwa Ukomunisti Afrika kupitia Afrika Mashariki.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akibariki vipaji wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Mkesha wa Mwaka Mpya 2026, katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma - Mbezi Beach, jimboni humo. (Picha na Mathayo Kijazi)
Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (VIWAWA) Jimbo Kuu la Dar es Salaam wakishangilia jambo wakati wa Homilia katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Beach Mass iliyoadhimishwa ufukweni Jimbo Katoliki la Bagamoyo.
Mwenyekiti wa Parokia ya Mtakatifu Kamili Yombo Kiwalani Josephat Moshi, akiwa katika picha ya pamoja na Wanakwaya wa Kwaya ya Shirikisho ya parokia hiyo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Krismasi iliyofanyika parokiani hapo.
Masista wa Shirika la Mtakatifu Fransisko wa Asizi Dada Wadogo Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri za Kwanza iliyofanyika katika Nyumba ya Masista hao Mbagala jimboni humo.
DAR ES SALAAM
Na Nicholas Kilowoko
Siku chache mara baada ya pambano lililomalizika, kwa Hassan Mwakinyo kumtandika bondia Stanley Eribo kutoka nchini Nigeria kwa ‘KO’, katika raundi ya pili ya pambano la raundi 10, bondia Twaha Kiduku ameubeza ushindi wake.
Bondia Twaha alisema kuwa pambano hilo lililofanyika siku ya Boxing Day, lilikuwa halina hadhi kutokana na mpinzani wa bondia mwenzake Mwakinyo, kutokuwa katika kiwango kinachotakiwa.
DAR ES SALAAM
Na Nicholas Kilowoko
Kocha wa vijana wa klabu ya soka ya Simba, John Bocco, ameelezea mikakati yake mipya ya kuisaidia timu yao kubwa, kupata vijana wazawa wenye vipaji na watakaolisaidia Taifa pia.
Kwa muda mrefu nyota huyo wa zamani, ambaye alifanya makubwa ndani ya klabu ya Simba, Azam FC, na JKT Tanzania, alikuwa yupo kimya mara baada ya kumaliza kazi yake ya uchezaji.
DAR ES SALAAM
Na Arone Mpanduka
Mkuu wa Kitengo cha Habari cha klabu ya soka ya Azam FC, Thabit Zacharia maarufu kama Zaka Zakazi, amesema kuwa kitakwimu winga wa Taifa Stars Simon Msuva, bado ataendelea kuwa juu katika ufungaji wa mabao mengi katika kikosi hicho, kuliko mchezaji mwingine yoyote.
Akitoa ufafanuzi kuhusiana na ubishani unaoendelea, wa kumlinganisha Msuva na mchezaji wa zamani wa Taifa Stars Mrisho Ngassa, Zaka alisema kwamba nyota hao wanalinganishwa kimakosa, kwa sababu Msuva ana mabao 21 aliyoifungia Taifa Stars pekee, huku Ngassa mabao yake yakichanganywa na aliyoifungia Kilimanjaro Stars, ambayo ni ya Tanzania Bara pekee.
London, Uingereza
Meneja wa Arsenal Mikel Arteta, amekiri kuwa watakuwa wakiangalia kwa makini usajili unaowezekana, wakati wa dirisha la uhamisho la Januari.
The Gunners walitumia takribani pauni milioni 250 msimu huu wa joto, na kuleta wachezaji wapya nane, huku wakitafuta kuongeza ubora katika kikosi chao, ili kukabiliana na orodha ya mechi zilizojaa, na kushindania mataji katika mashindano mengi.
Msimu uliopita kampeni ya Arsenal iliharibiwa na majeraha, kwani walikuwa bila mlinzi Gabriel Magalhaes, kwa sehemu ya mwisho ya msimu na walicheza na kiungo Mikel Merino, kama mshambuliaji wa muda, walipomaliza wa pili katika Ligi Kuu kwa msimu wa tatu mfululizo, na walitolewa katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa na Paris St-Germain.
Msimu huu The Gunners pia wamekuwa wakisumbuliwa na majeraha, mara baada ya kumpoteza Kai Havertz tangu siku ya ufunguzi, huku nahodha Martin Odegaard na Bukayo Saka, Gabriel Martinelli, Noni Madueke na Max Dowman wakiwa wamekosa nafasi.
Sasa baada ya majeraha kuwaathiri zaidi wachezaji washambuliaji, ni safu ya nyuma ya Arsenal inayoteseka, Arteta alilazimika kumchezesha Declan Rice, katika nafasi isiyojulikana ya beki wa kulia dhidi ya Brighton siku ya Jumamosi, kwa sababu Jurrien Timber alikuwa majeruhi, na Riccardo Calafiori alipata tatizo wakati wa mazoezi ya kupasha misuli.
Melboune, Australian
Uwanja wa Kriketi wa huko mjini Melbourne umekadiriwa kuwa hauridhishi, Baraza la Kriketi la Kimataifa (ICC) limethibitisha.
Uamuzi huo unamaanisha kuwa, Uwanja wa Kriketi wa Melbourne unapata pointi moja ya upungufu. Ikiwa uwanja unapata pointi sita za upungufu katika kipindi cha miaka mitano, unasimamishwa kuandaa kriketi ya kimataifa kwa miezi 12.
Ni mara ya kwanza uwanja nchini Australia, kuonekana kuwa chini ya kiwango, tangu ICC ibadilishe mfumo wake miaka miwili iliyopita.
Wiketi thelathini na sita zilianguka katika vipindi sita katika mechi ya Boxing Day, huku harakati nyingi za kushona zikitolewa kwa wapiga mpira wa kasi.
“Kwa wiketi 20 zikianguka siku ya kwanza, 16 siku ya pili na hakuna mpigaji hata mmoja aliyefikia nusu karne, uwanja ulikuwa hauridhishi kulingana na miongozo, na uwanja unapata pointi moja ya upungufu,” alisema mwamuzi wa mechi Jeff Crowe.
DAR ES SALAAM
Na Arone Mpanduka
Mchezo wa skwashi ulianzishwa karne ya 19 nchini Uingereza. Ulianza kama mabadiliko ya mchezo wa racquetball, na kuendelezwa katika shule za wasichana na wavulana.
Mchezo huu ulienea haraka katika nchi za Uingereza, kisha ulienea duniani kote, hasa katika nchi zilizoathiriwa na Wazungu kama Canada, Marekani, Australia, na baadhi ya nchi za Afrika.