Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri, Shemasi na Wanakwaya wa Kwaya ya Mtakatifu Rita wa Kashia, Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia - Goba Mwisho, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, sanjari na kusimikwa Paroko mpya iliyofanyika Parokiani hapo. Kushoto kwa Askofu ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Festo Liheta.
Askofu wa Jimbo Katoliki la Zanzibar, Mhashamu Augustino Shao akibariki sanduku lililobeba mwili wa marehemu Padri Daniel Macha aliyewahi kuwa Dekano wa Dekania ya Mtakatifu Gaspar, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya kumwombea iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Domonico Mbezi Juu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.
DAR ES SALAAM
Na Edvesta Tarimo
Katika jamii nyingi, viatu vyenye kisigino kirefu vimejijengea nafasi ya kipekee kama alama ya urembo, hesima, hadhi na kujiamini kwa mwanamke. Kwa muda mrefu, kuvaa kiatu chenye kisigino kirefu kumechukuliwa kama sehemu ya mwonekano wa kitaaluma na kifahari, hususani katika mazingira ya kazi na hafla rasmi. Hata hivyo, nyuma ya mvuto huo wa nje, tafiti za kisayansi zinaendelea kuibua hoja nzito, kuhusu gharama ya kiafya inayoweza kujificha kwenye mtindo huu.
Kihistoria, kumbukumbu zinaonesha kuwa viatu vyenye kisigino havikuanza kama vazi la wanawake. Tafiti za kihistoria za mitindo zilizokusanywa na Fashion Institute of Technology, zinaonesha kuwa takribani mwaka 1000 BK, wanaume wa Uajemi waliokuwa wakipanda farasi, walitumia viatu vyenye kisigino, ili kuimarisha mshikamano wa mguu na farasi.
DAR ES SALAAM
Na David Mpangile
Ili kutimiza wajibu wao Wakristo, ikiwa ni sehemu ya matunda ya ubatizo, Waamini hujaliwa karama mbalimbali.
Mafundisho ya Kanisa yanasisitiza kuwa karama yoyote itokayo kwa Roho Mtakatifu, yafaa katika kumsaidia mwamini katika safari yake ya kuutafuta utakatifu.
Karama hiyo pia inaweza kuchangia katika ustawi wa Kanisa, na ni msaada kwa ndugu wengine katika Kristo. Hivyo ni makosa kuacha kuitumia. Hata hivyo, bado kuna kishawishi cha Walei wengi kushindwa kutumia vipawa walivyo navyo, kwa sababu wanatafsiri kwamba karama ni zile tu zinazohesabika kuwa kubwa, kama vile kutenda miujiza na kunena kwa lugha.
Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya Papa Gregori Mkuu, ambaye alikuwa Baba wa Kanisa wa mwisho na kiungo kati ya dola ya Kirumi ya zamani na ulimwengu mpya wa kishenzi. Leo tunawaletea historia ya maisha ya Mtume Muhammad na mwanzo wa Uislamu. Sasa endelea…
Maisha ya Muhammad:
Katika kipindi cha ghasia na uvamizi wa Ulaya, ndipo Muhammad alizaliwa mwaka 570. Wazazi wake walikufa akabakia yatima na akalelewa na baba mdogo. Akiwa kijana alifanya kazi katika misafara ya ngamia ya mjane mmoja tajiri aliyeitwa Khadija.
Alifanya kazi vizuri, hata baadaye Khadija alimfanya Muhammad kuwa Mkuu wa misafara yake. Muhammad akiwa na umri wa miaka 25, alimwoa mwajiri wake Khadija aliyekuwa na miaka 35. Ndoa yao ilikuwa nzuri na ilidumu.
Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Sesilia-Kisarawe II, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Padri Roger Kamuzinzi (katikati) akiamua kuanza kwa mchezo wa kuvuta kamba kati ya Wanawake Wakatoliki (WAWATA) na Utume wa Wanaume Katoliki (UWAKA) wa parokia hiyo wakati wa sherehe ya Somo wa parokia, ambapo wanawake waliibuka washindi.
Mapadri kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya kumwombea marehemu Padri Daniel Macha iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Domonico Mbezi Juu jimboni humo.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akikabidhi zawadi kwa wawakilishi wa wagonjwa wanaopatiwa huduma za afya katika Zahanati ya Consolata, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Kuombea Wagonjwa Kijimbo, iliyofanyika katika Kituo cha Consolata Sisters (Kwa Bruda) - Mbagala Misheni, jimboni humo. Kushoto ni Katibu wa Idara ya Afya Jimbo, Pauline Archard.
Washiriki katika Semina ya kuwajengea vijana uwezo wa kujiajiri na kuajiriwa, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Semina hiyo iliyoratibiwa na Tumaini Media, iliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Parokia ya Kristo Mfalme - Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam. (Picha na Mathayo Kijazi)
Mwanza
Na Paul Charles Mabuga
Simulizi ya Amos Katama (sasa marehemu) ni kioo cha maumivu ya kizazi kizima. Kauli yake kuhusu “soli ya 20 ya kiatu kuchakaa akitafuta ajira” si dhihaka, bali ni kovu la kisaikolojia linalowatafuna wahitimu wengi. Amos aliondoka duniani akiwa na Shahada ya Uandishi wa Habari mkononi, lakini mfuko ukiwa mtupu. Hali hii inatufanya tujiulize: Je, vyuo vyetu vinazalisha wasomi au vinazalisha watafuta kazi waliofungwa pingu za kifikra?
DAR ES SALAAM
Na Remigius Mmavele
Lipua Lipua ni mojawapo ya bendi ambayo ilitamba sana miaka ya 1970, ambayo ilikuwa na wanamuziki mahiri katika uimbaji, upigaji vyombo, pamoja na utunzi wa nyimbo zilizogusa hisia za wapenzi wengi wa muziki.
Asili yake inaweza kufuatiliwa hadi 1973, mwaka ambao Bella Bella alipojitenga na lebo ya Veve, akitafuta uhuru wa kisanii, ambapo katika mabadiliko ya kejeli, wimbo kutoka wakati huo huo ulichochea kutajwa kwa kundi jipya.
Newyork, Marekani
Waandaaji wa mashindano ya Milan-Cortina 2026, wanasema kuwa wanachunguza kwa nini medali za Olimpiki zinavunjika, baada ya wanariadha kadhaa kukumbwa na matatizo hayo.
Washindi wawili wa medali ya dhahabu wa Marekani, Breezy Johnson na Alysa Liu, walifichua kwamba utepe huo ulitoka nje ya medali hiyo, mara baada ya kupokea zawadi yao.
London, Uingereza
Tottenham Hotspurs wako kwenye vita vya kushushwa daraja, anasema nahodha wa zamani wa Uingereza Wayne Rooney.
Kichapo cha 2-0 kutoka kwa Manchester United, kiliongeza mwendo wao wa kutoshinda katika Ligi ya Premia, hadi mechi saba na kuwaacha vijana wa Thomas Frank, wakiwa nafasi ya 15 kwenye jedwali na pointi sita pekee, juu ya eneo la kushushwa daraja.
DAR ES SALAAM
Na Arone Mpanduka
Licha ya timu nne za Ligi Kuu kuwa nyuma ya ratiba, kutokana na ushiriki wa michuano ya kimataifa, uongozi wa Bodi ya Ligi umesema kuwa unasaka njia bora, ya kuhakikisha hakutakuwa na viporo vingi msimu huu.
Kwa sasa timu za Simba, Yanga, Azam FC na Singida Black Stars, zimeonekana kuwa na mechi chache zaidi za kucheza, ikilinganishwa na timu nyingine, kutokana na ushiriki wao wa kimataifa.