Dekano wa Dekania ya Kilimahewa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Paul Kamuhabwa akiwa katika picha ya pamoja na vijana waliopata Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wa Parokia ya Bikira Maria Malkia-Kilimahewa jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti hiyo. Mstari wa nyuma ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Daudi Ngate.
Dar es Salaam
Na Pd. Richard Mjigwa- C.PP.S
Ilikuwa ni Novemba 8, mwaka 1984, Mtakatifu Yohane Paulo II (Papa), alipochapisha Waraka unaojulikana kama “Tot tantaeque” yaani “Bikira Maria ameidhinishwa kuwa Mlinzi na Mwombezi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, Sherehe inayoadhimishwa kitaifa kila mwaka ifikapo Desemba 9.
Katika mkesha wa uhuru wa Tanganyika, Mtakatifu Yohane XXIII, alitunga Sala Maalumu kwa ajili ya kuiombea Tanganyika, ili uhuru wake uweze kuwanufaisha watu wake.
DAR ES SALAAM
Na Edvesta Tarimo
Afya ya akili ni moja ya vipengele muhimu zaidi vya ustawi wa binadamu, lakini mara nyingi hupewa nafasi ndogo katika mjadala wa afya.
Hata hivyo utafiti unaonesha kwamba, afya ya akili inajumuisha hali ya kiakili, kihisia na kijamii ya mtu, na ni msingi wa jinsi anavyokabiliana na changamoto za kila siku.
Licha ya kwamba kila mtu anapitia magumu maishani, kuna njia za kujikinga dhidi ya athari za majeraha ya kihisia (kiwewe), na kujenga uthabiti wa kukabiliana na hali ngumu.
Waimarishwa wa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wa Parokia ya Mtakatifu Maria Magdalena – Kimara Mtoni, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti hiyo iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha na Mathayo Kijazi)
Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Joseph Cottolengo – Masaki - Kisarawe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha na Mathayo Kijazi)
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi (mwenye Fimbo ya Kichungaji) akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri na Viongozi wa Kamati Tendaji ya Parokia ya Mtakatifu Teresa wa Calcutta - Kivule, baada Adhimisho la Misa Takatifu ya Kutabaruku Kanisa na Altare.
Masista wa Shirika la Dada Wadogo wa Mtakatifu Fransisko wa Asizi Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri za Daima na Jubilei ya Miaka 25 ya Utawa iliyofanyika hivi karibuni.
Mwanza
Na Paul Charles Mabuga
Kichapo cha 2-0 kutoka kwa Azam FC, si tu kwamba kimepunguza kasi ya Simba kwenye mbio za ubingwa, bali kimetupa picha ya kutisha: Simba inaumwa, na wapinzani wamegundua dawa ya ugonjwa wake.
Matokeo haya yanazua swali gumu: Je, timu hii imegeuka kuwa Mnyama wa Karatasi? Uchambuzi huu unakwenda ndani kabisa, ukifichua kwa nini udhaifu mmoja unajirudia, na jinsi benchi la ufundi linavyoshindwa kuleta ufumbuzi, dhidi ya mbinu za kisasa za mpinzani. Hii ni muhimu kwa kuwa timu imefungwa namna ile ile, kama ilivyotokea kwa Stade Malien.
DAR ES SALAAM
Na Remigius Mmavele
Papy Tex mwimbaji mwenye sauti ya kuvutia na ya kipekee jina lake lake halisi ni Matolu Dode Jean , alizaliwa Juni 28, 1952 katika jiji la Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Baba yake mzazi alikuwa ni raia wa nchi ya Angola na mama yake kutoka Kongo ya Kati, alilelewa na Joséphine Matolu. Ni mwanamuziki maarufu duniani, mwandishi , mtunzi na mtayarishi wa muziki ambaye sauti yake ya huzuni na nyimbo zake zimeacha alama katika fikra za watu na bado zinaacha kumbukumbu zisizofutika katika kumbukumbu ya pamoja.
New York, Marekani
Mfululizo wa ajabu wa LeBron James wa michezo 1,297 ya NBA ya msimu wa kawaida, akifunga pointi 10 au zaidi ulimalizika huku Los Angeles Lakers, wakishinda Toronto Raptors kwa pointi 123-120.
James mwenye miaka 40, yuko katika msimu wake wa 23 ambao haujawahi kutokea, alifunga pointi nane dhidi ya Raptors na kutoa pasi 11, ikiwa ni pamoja na pasi ya Rui Hachimura, kufunga bao la ushindi lililomshinda mchezaji huyo.
London, Uingereza
Tottenham wanasema wanachunguza madai kwamba kiungo Yves Bissouma, alirekodiwa akivuta nitrous oxide.
Gazeti la The Sun lilichapisha picha, ambazo lilidai zilimuonesha mchezaji huyo wa kimataifa wa Mali, mwenye umri wa miaka 29 akivuta dutu hiyo, ambayo pia inajulikana kama gesi ya kuchekesha au NOS.
DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Singida Black Stars, imeandaa mkakati wa kuhakikisha katika kipindi hiki cha mapumziko, wanafanya maboresho machache ambayo yalikuwa ndani ya kikosi chao.
Kupitia kwa msemaji wao Hussein Massanza alisema kwamba, kupoteza kwenye mchezo wao dhidi ya TRA United, kumewafanya waone mapungufu mengi ndani ya klabu yao, ambayo kocha wao Miguel Gamond anakwenda kuyafanyia marekebisho.
DAR ES SALAAM
Na Nicolaus Kilowoko
Kocha mkuu wa klabu ya soka ya Yanga, Pedro Goncalves, amefunguka kuhusu umuhimu wa kufanya usajili, kuelekea katika dirisha dogo la usajili, huku matamanio yake makubwa ni kuwa na kikosi chenye ushindani, katika mashindano ambayo wanashiriki msimu huu.
Goncalves alisema kuwa kufanya usajili ndani ya klabu yake, ni jambo zuri ila ataangalia hasa ni maeneo gani ya kufanya maboresho, kwani tayari ameendelea kuwajumuisha wachezaji wote waliosajili msimu huu, katika mechi mbalimbali.
Dar es Salaam
Na Mwandishi wetu
Paroko Msaidizi wa Paroki ya Mtakatifu Rita wa Kashia -Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Kanuti Martin Nyoni, amewataka Waamini waendelee kusali na kumuomba Mwenyezi Mungu, ili Taifa liendelee kuwa na viongozi waadilifu, wenye kusikia sauti yake Mwenyezi Mungu, katika kuwalinda na kuwaongoza raia.
Padri Nyoni alitoa wito huo hivi karibuni, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu, ya kuwaombea Watu wote waliouawa na kujeruhiwa, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu iliyofanyika parokiani hapo.