Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

VATICAN CITY, Vatican

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Leo XIV, amekazia kuhusu furaha ya Mama Kanisa kwa zawadi ya Bikira Maria aliyekingiwa dhambi ya asili, kielelezo cha usafi na utakatifu, ili aweze kumzaa Kristo Yesu, Mwana wa Mungu kwa ajili ya wokovu wa walimwengu, Sherehe ambayo ilitangazwa Desemba 8, 1854 na Papa Pio IX.
Papa aliyasema hayo katika Maadhimisho ya Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, sherehe ambayo ilitangazwa Desemba 8, 1854 na Papa Pio IX.

VATICAN CITY, Vatican

Mwadhama Pietro Kardinali Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, amefanya hija ya kitume nchini Msumbiji, kama sehemu ya Maadhimisho ya Kumbukizi ya Miaka 30, tangu Vatican ilipoanzisha uhusiano wa Kidiplomasia na Msumbiji, Desemba 14, 1994, miaka 30 iliyopita, sanjari na Jubilei ya Miaka 50 tangu Msumbiji ijipatie uhuru wake wa bendera.
Hayo yalijiri kuanzia Desemba 5 hadi 10, 2025, ambapo tayari Kardinali huyo amekutana na kuzungumza na Viongozi Wakuu wa Serikali ya Msumbiji, wakiongozwa na Rais Margarida Adamugy Talapa.

Mwanza

Na Paul Mabuga

Maandishi yaliyoandikwa kwenye bajaji zetu, ambayo  kwa  muhtasari na kwa  muktadha wa yaliyokusanywa katika makala haya, unaweza kusema ni kama kutoka, “Enzi za Mwalimu” hadi “Kwenye Ndoa Yenu...”:, na vilevile ni maneno yanayosema mengi yenye kusisimua, kuibua hisia, kufurahisha na hata kufikirisha, sembuse kutia hofu na kuogofya.

Ni kwamba licha ya barabara za miji yetu hapa nchini, kujaa watu na shamrashamra za kelele za honi, lakini  pia zimesheheni  falsafa ya Mswahili.. Sio kwenye vitabu au kwenye mikutano ya hadhara, bali kwenye mabango madogo yaliyobandikwa, au kuandikwa nyuma ya magari yetu ya usafiri, na vyombo vingine maarufu kama Bajaji.

Dekano wa Dekania ya Kilimahewa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Paul Kamuhabwa akiwa katika picha ya pamoja na vijana waliopata Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wa Parokia ya Bikira Maria Malkia-Kilimahewa jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti hiyo. Mstari wa nyuma ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Daudi Ngate.

Dar es Salaam

Na Pd. Richard Mjigwa- C.PP.S

Ilikuwa ni Novemba 8, mwaka 1984, Mtakatifu Yohane Paulo II (Papa), alipochapisha Waraka unaojulikana kama “Tot tantaeque” yaani “Bikira Maria ameidhinishwa kuwa Mlinzi na Mwombezi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, Sherehe inayoadhimishwa kitaifa kila mwaka ifikapo Desemba 9.
Katika mkesha wa uhuru wa Tanganyika, Mtakatifu Yohane XXIII, alitunga Sala Maalumu kwa ajili ya kuiombea Tanganyika, ili uhuru wake uweze kuwanufaisha watu wake.

DAR ES SALAAM

Na Edvesta Tarimo

Afya ya akili ni moja ya vipengele muhimu zaidi vya ustawi wa binadamu, lakini mara nyingi hupewa nafasi ndogo katika mjadala wa afya. 
Hata hivyo utafiti unaonesha kwamba, afya ya akili inajumuisha hali ya kiakili, kihisia na kijamii ya mtu, na ni msingi wa jinsi anavyokabiliana na changamoto za kila siku. 
Licha ya kwamba kila mtu anapitia magumu maishani, kuna njia za kujikinga dhidi ya athari za majeraha ya kihisia (kiwewe), na kujenga uthabiti wa kukabiliana na hali ngumu.

Waimarishwa wa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wa Parokia ya Mtakatifu Maria Magdalena – Kimara Mtoni, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti hiyo iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha na Mathayo Kijazi)

Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Joseph Cottolengo – Masaki - Kisarawe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha na Mathayo Kijazi)

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi (mwenye Fimbo ya Kichungaji) akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri na Viongozi wa Kamati Tendaji ya Parokia ya Mtakatifu Teresa wa Calcutta - Kivule, baada Adhimisho la Misa Takatifu ya Kutabaruku Kanisa na Altare.

Masista wa Shirika la Dada Wadogo wa Mtakatifu Fransisko wa Asizi Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri za Daima na Jubilei ya Miaka 25 ya Utawa iliyofanyika hivi karibuni.