Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu amezindua Warsha kwa Waamini wote wa Jimbo hilo, inayotarajiwa kufanyika Novemba 29 mwaka huu, katika viwanja vya Parokia ya Kristo Mfalme - Tabata.
Uzinduzi huo aliufanya hivi karibuni Posta jijini Dar es Salaam, akiwasihi Waamini wote kujiandikisha na kushiriki kwa wingi katika Warsha hiyo, ambapo ndani yake kutakuwa na semina itakayohusisha mada mbalimbali.

Dar es Salaam

Na Laura Mwakalunde

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewasihi Waamini kuacha kuzificha imani zao kwa kubadilika badilika kila wakati.
Aliyasema hayo hivi karibuni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Martha- Mikocheni jimboni humo.

Morogoro

Na Angela Kibwana

Kanisa Katoliki limehitimisha mfungo maalumu kote nchini, ambapo Wakatoliki walifunga, kuabudu Ekaristi Takatifu na kuiombea nchi haki na amani, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Hatua ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), kutoa sala maalumu na agizo la kuwashirikisha Waamini kufunga, kusali na kuombea haki na amani si mara ya kwanza, bali limefanya hivyo mara kwa mara hasa inapoonekana kuna viashiria vya uvunjifu wa amani, ambayo ni tunda la haki.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amelipongeza Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), kwa kuongezeka kwa thamani ya soko hilo na kufikia shilingi trilioni 21.0, katika kipindi cha kufikia Julai mwaka huu.
Waziri Mkuu Majaliwa alisema  kwamba, soko hilo limeongeza ukuaji wa mauzo ya hisa kwa zaidi ya asilimia 246, pamoja na ongezeko la idadi ya wawekezaji hadi zaidi ya akaunti 683,000, ikiwa ni ishara ya ukuaji imara wa sekta ya mitaji nchini.

Ahadi ya serikali ya kufikisha umeme wa gridi ya taifa katika wilaya zote za Mkoa wa Kagera, imetekelezwa baada ya kusaini mikataba ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 220, kutoka Benako-Ngara hadi Kyaka wilayani Misenyi.
Aidha, hatua hiyo imekwenda sanjari na kituo cha kupoza umeme cha Benako cha msongo wa kilovoti 220/33, na kutoa uhakika kwa Mkoa huo kupata umeme wa gridi na kuacha kutegemea umeme kutoka Uganda.

Askofu wa Jimbo Katoliki la Kahama Mhashamu Christopher Nkoronko, (pichani) amewataka Waimarishwa kuwa tofauti na wengine hasa wanapokuwa kanisani, nyumbani au shuleni.
Alisema hayo hivi karibuni, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, iliyofanyika katika Parokia ya Watakatifu Joachim na Anna-Mwime Jimbo Katoliki la Kahama.

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Waandishi wa Habari wametakiwa kuwa wabunifu na wenye kujitolea kufanya vitu vya tofauti katika kazi zao, ili waweze kuzalisha vipindi na habari zenye ubora.
Hayo yalisemwa na Derik Murusuri, Mwezeshaji katika Semina ya Waandishi wa Habari, iliyofanyika hivi karibuni Msimbazi Centre, jijini Dar es Salaam.

Mtwara

Na Mwandishi wetu

Askofu wa Jimbo Katoliki la Musoma, Mhashamu Michael Msonganzila amewataka wanawake kuwa wanyenyekevu kama Mama Bikira Maria.
Alisema hayo wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 40 ya Parokia, na Miaka 20 ya Utume wa Padri Fintani Mrope, Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme, Tandahimba Jimbo Katoliki la Mtwara, iliyofanyika parokiani hapo.
Askofu Msonganzila alisema kwamba Waamini wengi wanayumbayumba kila sehemu katika imani, hiyo yote ni kutangatanga bila kuelewa wanachokitafuta.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akipokea Baraka ya Kwanza kutoka kwa Padri mpya Oresto Kapugi wa Shirika la Mungu Mwokozi (SDS), wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Daraja la Upadri iliyoadhimishwa katika Parokia ya Bikira Maria Nyota wa Bahari, Kisiju Jimboni humo. (Picha na Yohana Kasosi)

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Wazazi wametakiwa kutoa ushirikiano kwa Maparoko katika parokia zao, ili watoto wao waendelee na mafundisho ya kuwajengwa katika imani baada ya sakramenti zao.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mungu - Vijibweni, Kigamboni jijini Dar es Salaam.
“Wazazi na walezi toeni ushirikiano kwa Paroko wenu, ili watoto hawa waendelee kupatiwa majiundo, waendelee kupatiwa Mafundisho ya Imani hata baada ya kupokea Sakramenti hii ya Kipaimara,” alisema Askofu Mkuu Ruwa’ichi.
Aidha, Askofu huyo aliwataka vijana kuwa watumishi wa Bwana kikamilifu, huku wakiitambua hadhi yao pamoja na wito wao.
Alisiwahi kuwa watumishi kweli wa Yesu Kristo, badala ya kuwa Wakristo goi goi, wala Wakristo tia maji tia maji katika maisha yao
“Kuweni watumishi kweli wa Yesu Kristo, msiwe Wakristo goi goi, wala Wakristo tia maji tia maji katika maisha yenu. Itambueni hadhi yenu na wito wenu kama Wakristo,” alisema Askofu Mkuu Ruwa’ichi.
Aliongeza kuwa kwa kupokea Sakramenti hiyo Takatifu ya Kipaimara, sasa vijana hao wamehitimisha awamu ya kuwa watoto, akiwasihi kudumu katika imani, huku wakiyashika yale yote waliyofundishwa.
Aliwasihi kuendelea kuimarisha imani na maadili, akimsihi Paroko wa parokia hiyo kusimamia ili vijana hao waendelee kupatiwa mafundisho (majiundo), endelevu.
Askofu Mkuu Ruwa’ichi alisema kwamba kwa kuwa hizi ni zama za kelele, upo umuhimu wa kuwasimamia vyema watoto hao ili waendelee kukua katika misingi ya imani, kwani wasiposimamiwa vyema, watapotea.
Katika homilia yake, Askofu huyo aliwasihi vijana, wazazi na Waamini wote kwa ujumla, kupendana kama vile Kristo anavyowapenda, kwani Kristo amewapenda bila kujibakiza.