Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

MELBOURNE, Australia
Novak Djokovic anasema bado anapata kiwewe anapotembelea Melbourne, miaka mitatu baada ya kufukuzwa kwa sababu ya kanuni za Covid-19 za Australia.
Djokovic, ambaye hakuchanjwa dhidi ya virusi hivyo, visa yake ilifutwa na serikali ya Australia kwa misingi ya afya na utaratibu mzuri.
Alilazimika kukaa katika hoteli ya uhamiaji kwa siku tano, huku akikata rufaa bila mafanikio dhidi ya uamuzi huo, na hatimaye kulazimika kuondoka nchini humo, kumaanisha kwamba alikosa michuano ya Australian Open 2022.
Djokovic alirejea Melbourne mwaka uliofuata, vizuizi vya Covid vikipunguzwa, na akashinda Grand Slam kwa mara ya 10 ya rekodi.
“Mara kadhaa ya mwisho nilipotua Australia kupitia udhibiti wa pasipoti na uhamiaji, nilikuwa na kiwewe kidogo kutoka miaka mitatu iliyopita, lakini athari zingine bado hukaa pale ninapopitisha udhibiti wa pasipoti, nikiangalia tu ikiwa kuna mtu kutoka eneo la uhamiaji anakaribia”, alisema Djokovic.

DAR ES SALAAM

Na Deus Helandogo

Raga, maarufu kama Rugby, ni mchezo ulioanzishwa mwanzoni mwa karne ya 19 katika Mataifa ya Uingereza na Marekani, na una namna nyingi ya kuchezwa, kama vile kwa kutumia mikono pamoja na miguu, huhusisha wachezaji 15 kwa kila upande wa timu shindani
Mchezo huu ni maarufu sana kwenye Mataifa ambayo yana shabihiana kiutamaduni na Taifa la Uingereza, ikiwemo Umoja wa Jumuiya ya Madola kama vile Austalia, Kenya, Afrika Kusini, Canada na Namibia, kwenye baadhi ya Mataifa mchezo huu ni mchezo ambao una sifa ya kuwa mchezo wa Kitaifa
Raga ilianza pamoja na mchezo wa mpira wa miguu, na baadae sheria za michezo hiyo miwili zikatofautiana  na kuwa michezo miwili tofauti. Raga ikabaki ikichezwa kwa kutumia mikono na miguu, huku mpira wa miguu akaanza kuchezwa  kwa kutumia miguu tu
Mpira unaotumika kuchezea Raga umetengenezwa kwa mfumo wa umbo mviringo, mithili ya yai unaoweza kubebeka na kukimbia nao, ukiwa mkononi, na inapotokea kuurusha haumsumbi mchezaji huurusha kwa haraka
Takwimu zinaonesha kuwa mchezo huu umezidi kukua kwa kasi ulimwenguni  kwani huchezwa na kila jinsia na umri wowote. Mwaka 2023, ilithibitika kuwa zaidi ya watu milioni kumi (10) hucheza  mchezo huu  duniani kote.
Na katika kipindi hicho, watu milioni 8.4 walikuwa wamesajiliwa na Chama cha mchezo huo duniani ambacho kifupi chake ni (IRFB), na Mataifa 116 yana vyama vinavyoongoza mchezo wa Raga duniani kote.
Kuanzia miaka ya 1863, mchezo huu ulikuwa unachezwa kama ridhaa kwa kujifurahisha zaidi, na siyo kazi rasmi ambayo ilikuwa na maslahi, mpaka ilipofika mwaka 1995 ndipo sheria mpya zilitungwa na kuurasimisha mchezo huu ambapo ulianza kulipa wachezaji, makocha  na waamuzi,  hivyo watu wakaanza kunufaika na mchezo wenyewe.
Mchezo wa kwanza wa Raga wa Kimataifa  ulichezwa mnamo 27 Machi, 1871 kati ya Scotland na Uingereza huko Edinburgh, Scotland ilishinda mchezo huo kwa bao moja, hadi kufikia mwaka 1881, ambapo Ireland na Wales zilikuwa na timu za uwakilishi katika mashindano ya Kimataifa
Mashindano muhimu zaidi katika mchezo wa Raga ni Kombe la Dunia la Raga, mashindano ya wanaume, ambayo yamekuwa yakifanyika kila baada ya miaka minne tangu kuzinduliwa kwa michuano hiyo mnamo mwaka 1987.
Afrika Kusini ndiyo Mabingwa watetezi baada ya kuifunga New Zealand 11-12 katika fainali ya Kombe la dunia la Raga 2023 nchini Ufaransa.
Lakini katika historia, Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya kushinda makombe, kwani imeshinda Kombe la Dunia mara nne (1995, 2007, 2019 na 2023).
New Zealand imeshinda taji hilo mara tatu (1987, 2011 na 2015); Australia imeshinda mara mbili (1991 na 1999); na Uingereza mara moja (2003).
England ndio timu pekee kutoka Kaskazini mwa Bara la Ulaya ambayo imeshinda Kombe la dunia la Raga
Kombe la Dunia la Raga limeendelea kukua tangu kuanzishwa kwake mwaka 1987 kwani mashindano ya kwanza, ambayo timu 16 zilishiriki ilionyeshwa kwa nchi 17, na jumla ya watazamaji milioni 230 wa televisheni, walishuhudia. Mauzo ya tiketi wakati wa hatua za bwawa na fainali za mashindano hayo, yalikuwa chini ya milioni Kombe la Dunia la mwaka 2007 lililoshindaniwa na nchi 94, na mauzo ya tiketi yalikuwa  3,850,000.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Mshambuliaji wa Yanga, Kennedy Musonda, amefunguka juu ya ukweli wa maisha yake binafsi, huku akiweka wazi kuwa malengo yake ya kwanza yalikuwa ni kuwa Mhandisi, lakini mwisho wa siku mambo hayakwenda vile ambavyo alikuwa anataka.
Nyota huyo (pichani) ambaye anamudu uwanjani kwenye nafasi ya mshambuliaji wa kati na pembeni alisema kuwa mwanzo alikuwa anataka kuwa Mhandisi kabla ya soka kummbadilishia mwelekeo na hatimaye akaacha kile alichokuwa anatamani kukifanya.
Musonda alisema kuwa alitakiwa kwenda chuo kwa ajili ya kusomea Uhandisi, lakini soka lilimbadilishia mfumo wa maisha na sasa amekuwa mfumania nyavu uwanjani.
“Mwanzo nilitakiwa kwenda chuo kusomea Usanifu wa Majengo, lakini mpira ulinipa mwelekeo mwingine wa maisha ndiyo kama hivi kwa sasa, nachezea Yanga”, alisema Musonda.
Kuhusu kazi yake na majukumu yake uwanjani kama mchezaji sasa wa Yanga, Musonda amepanga kufunga mabao zaidi na kuisaidia Yanga kushinda kila mchezo wake msimu huu.
Lakini, kwa upande mwingine Musonda alifunguka juu ya ugumu anaoupata wa namba tangu asajiliwe ndani ya Yanga huku akiweka wazi kuwa juu ya mkanganyiko wa mashabiki wake, wanaojiuliza juu ya kwa nini hafunguki akiwa na Yanga huku kwenye timu yake ya Taifa akifunga.
Musonda alisema kuwa kwenye timu yake ya Taifa, anapata nafasi sana na ndiyo maana anafunga sana, lakini kwa upande wa klabu imekuwa tofauti, kwani hapati nafasi sana. Mpaka sasa amecheza mara 20 pekee, hali inayopelekea kupata changamoto ya kupachika mabao.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Wakati wa kufanyika kwa droo na hata baada ya kuanza kwa michuano ya Afrika ambayo Simba na Yanga wanashindania Ubingwa, mashabiki wengi na wadau wa soka walikuwa na maoni tofauti juu ya timu zao wakizichambua katika viwango vya juu, lakini kwa sasa hali imekuwa tofauti, kwani maji na unga vimeanza kujitenga.
Mpaka sasa bado mambo hayajaenda sawa kwa klabu za Tanzania ambazo zinashindana katika michuano hiyo ya Afrika msimu huu, tofauti na ilivyotarajiwa.
Simba inashiriki Kombe la Shirikisho kutokana na kushika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi msimu uliopita, huku watani zao klabu ya soka ya Yanga ikishiriki michuano ya Klabu Bingwa Afrika, na hii ni baada ya kuwa Mabingwa msimu iliopita katika Ligi Kuu Soka Tanzania Bara.
Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya soka ya Simba, Ismail Aden Rage, aliweka wazi kuwa klabu ya soka ya Yanga bado hawajawa katika kiwango bora kama walivyokuwa katika misimu miwili ya nyuma na hilo limechangia kuwepo kwenye nafasi waliyopo sasa.
Rage alisema na kuweka wazi mara baada ya kufanya tathmini yake katika mchezo wao uliopita waliocheza katika dimba la Benjamini Mkapa, akidai kuwa walipata nafasi nyingi za kufunga, lakini walishindwa kuzitumia ipasavyo dhidi ya wapinzani wao TP Mazembe.
Alisema kuwa bado Yanga wana safu mbovu ya ushambuliaji ambayo inawasababisha washindwe kupata matokeo chanya kwenye mechi zake msimu huu.
Yanga ilipata ushinda wa mabao 3-1 dhidi ya TP Mazembe katika mechi ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, iliyochezwa Jumamosi, Januari 4 mwaka huu.
Kuhusu Simba, Rage alisema kuwa, bado inajitafuta, japokuwa imefanya vyema katika michezo yake mitatu kati ya minne, ambayo mpaka sasa imeshacheza katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho, wakipata ushindi huku wakifungwa mchezo mmoja.
Watanzania wengi bado hawana matumaini ya dhati juu ya klabu hizo kutokana na nafasi walizokuwa nazo kwenye misimamo ya makundi yao, huku kwa sasa ni mahesabu ya vidole tu ndiyo yaliyobaki.
Yanga kwa kuchechemea katika michezo minne, ameshinda mchezo mmoja, akipata sare mchezo mmoja huku akifungwa michezo miwili, na amekusanya alama nne, akishika nafasi ya tatu katika msimamo wa kundi lake michuano ya Klabu Bingwa Afrika, hatua ya makundi.
Simba nayo ni kama wanaingia wanatoka, kwani katika michezo minne, ameshinda michezo mitatu, akifungwa mchezo mmoja, akijikusanyia alama tisa, akishika nafasi ya pili kwenye hatua ya makundi katika michuano ya Kombe la Shirikisho.
Timu zote hizo zinatarajiwa kutupa karata zao nyingine katika viwanja vya ugenini January 12 ambapo klabu ya Simba watawafuata Bravos ya Angola huku klabu ya soka ya Yanga ikiwafuata Al Hillal ya kutokea kule Sudan.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akiwa katika picha ya pamoja na Kamati Tendaji ya Parokia ya Mtakatifu Cesilia, Kisarawe II, jimboni humo. Kulia kwa Askofu ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Roger Kamuzinzi, na kushoto ni Paroko Msaidizi. (Picha na Yohana Kasosi)

Waamini wa Parokia ya Bikira Mama wa Kanisa, Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sikukuu ya Krismas iliyoadhimishwa hapo hivi karibuni.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akibariki matoleo wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Noeli katika Parokia ya Mtakatifu Agustino – Salasala. Kushoto ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Peter Assenga. (Picha na Mathayo Kijazi)

Padri Denis Kunambi, Paroko wa Parokia ya Roho Mtakatifu Segerea, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam akikabidhi vitendea kazi kwa Kamati Tendaji ya Kigango cha Kuzaliwa Bikira Maria, Kisukuru, Parokia ya Roho Mtakatifu, Segerea, wakati wa Misa Takatifu ya Uzinduzi wa Kigango hicho.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba -OSA, akimbatiza mtoto Kiernani James katika Parokia ya Mtakatifu Boniventura, Kinyerezi jimboni humo wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ambapo watoto 93 walibatizwa, na Watoto 43 walipata Sakramenti ya Ekaristi Takatifu. (Picha na Yohana Kasosi)

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akiumwagia maji mti baada ya kuupanda katika Parokia ya Mtakatifu Cesilia, Kisarawe II, Kigamboni jimboni humo. Wengine ni Mapadri, Viongozi wa Halmashauri ya Walei, na baadhi ya Waamini. (Picha na Yohana Kasosi)