DAR ES SALAAM
LAURA CRISPIN
Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam limeanzisha Klabu ya michezo itwayo St. Joseph Sport Club’ ili kuimarisha shughuli za uinjilishaji kupitia michezo, kuboresha afya na kutoa ajira kwa vijana.
Akizungumza na Tumaini Letu katika mahojiano maalum yaliyofanyika hivi karibuni, Padri Vitalis Kassembo, Mkurugenzi wa Walei Jimbo Kuu la Dar es Salaam alisema kwamba kitu kilichowasukuma kuanzisha timu ya mpira wa miguu ya St. Joseph Sport Club ni kwa ajili ya muendelezo wa Warsha ya Walei.
“Tumeanzisha klabu ya St. Joseph Sports kwa lengo la kuinjilisha kupitia michezo, kuwafanya vijana wawe na afya nzuri pamoja na kuwapatia vijana ajira kupitia michezo, japokuwa siyo wote ni kwa wale wenye vipaji vya michezo,”alisema Padri Kassembo.
Alisema kuwa mara zote wamekuwa wakipoteza timu baada ya Warsha kuisha na kuwafanya kila mwaka kutafuta timu mpya.
Padri Kassembo aliendelea kusema kuwa wameanzisha timu hiyo kwa lengo la kuacha alama ya Jubilee ya Miaka 75 ya Jimbo Kuu la Dar es Salaam na kujenga mwili wenye afya pamoja na Roho yenye afya.
Alibainisha kwamba klabu hiyo ya St. Joseph Sport inabebwa na kauli mbiu ambayo wataishi siku zote katika michezo, ambayo ni ‘Imani, Michezo na Ushindi’.
Padri Kassembo aliendelea kusema kwamba, ikiwa wataishi katika kauli mbiu yao ya imani, michezo na ushindi basi mapato yatakayopatikana kupitia timu hiyo, yataenda kusaidia ujenzi wa Kanisa mbadala Pugu.
BAGAMOYO
Askofu wa Jimbo Katoliki la Bagamoyo, Mhashamu Stephano Musomba, alisema kuwa siasa ni neno zuri ila watu wameliharibu, kwa kutumia uongo na kupotosha.
Askofu Musomba alisema hayo wakati akitoa homilia yake, katika Ibada ya Ijumaa Kuu, iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli-Bunju, jimboni humo.
“Ukweli mara zote unauma, japo unaponya na ni mchungu, ingali huwa ni mtamu kama asali, ikiwa utatenda katika mastahili ya ukweli,” alisema Askofu Musomba.
Aidha, aliwasihi Waamini kusikiliza kila wanachoambiwa, kwa sababu kitawafanya wawe bora zaidi, japokuwa wakati mwingine huzaliwa ‘machawa’, ambao kazi yao ni kusifia bila kukosoa, wakifanya hivyo kwa ajili ya kujipatia kipato tu.
Na Mwandishi wetu
Katika kuadhimisha Sikukuu ya Pasaka mwaka huu, jamii imeonywa kuacha tabia ya kukimbilia kuchukua picha na video katika majanga, na kuanza kuzituma mitandaoni, badala yake waanze kutoa msaada kwa watu waliokumbwa na mkasa huo.
Onyo hilo lilitolewa hivi karibuni, na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akiwataka watu wenye tabia ya kupiga picha na kuchukua video kwenye majanga, bila ya kutoa msaada, kuacha mara moja kufanya hivyo.
Na Edvesta Tarimo
Matumizi ya dawa za kulevya, yanaendelea kuwa tishio kubwa kwa afya ya akili na uchumi wa taifa, huku wataalamu wakionya kuwa bila hatua za pamoja, jamii itaendelea kupoteza nguvu kazi yake, hususani vijana.
Matumizi ya madawa ya kulevya yameendelea kuongezeka duniani, huku Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya mwaka 2023, ikionesha kuwa idadi ya watumiaji wa dawa za kulevya duniani, ilifikia milioni 316, sawa na 6% ya idadi ya watu wenye umri wa kati ya miaka 15–64.
Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya Kanisa kuibuka kuwa Mlezi wa Elimu, Leo tunaendelea kuwaletea historia ya kuibuka kwa mashirika yalianzishwa kwa ajili ya kuimarisha moyo huo Mtakatifu wa kidini. Sasa endelea…
Wakartusiani:
Wakartusiani walikuwa aina ya wakaa pweke, kwa mfano wa Mtakatifu Antoni wa Jangwani, ila waliishi pamoja bila mawasiliano. Wamonaki hawa walisali pamoja na kufunga, bila kuongea au kuwa na mawasiliano na watu wengine wa nje.
Hawa walianzishwa na Mtakatifu Bruno mwaka 1084. Shirika hili lilikuwa thabiti kiasi kwamba mashirika mengine yalipolegea, lenyewe lilibaki imara bila kupakwa uchafu wa dunia. Palikuwa na msemo kwamba, hapajakuwa na ulazima wa kurekebisha shirika hili, kwa sababu halijateteleka kwa uozo (never reformed because never deformed).
Wengi wao walikufa mashahidi, wakati wa Waprotestanti kwa kukataa kuacha Utawa. Kwa kufuata mfano huo, yalianzishwa mashirika mengine kama Wasistesiani, walioimarishwa na Mtakatifu Bernardo wa Clairvaux mwaka 1090.
Wanakwaya wa Kwaya ya UKWAKATA Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakiimba wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Jumatatu ya Pasaka, Kijimbo iliyoadhimishwa katika Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu - Manzese jimboni humo. Wengine ni Waamini walioshiriki Adhimisho hilo.
Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia - Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakishiriki Adhimisho la Misa Takatifu ya Ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika parokiani hapo.
Wanakwaya wa Kwaya ya Familia Takatifu Parokia ya Mtakatifu Maximillian Maria Korbe - Mwenge, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika picha ya pamoja na baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sikukuu ya Pasaka iliyofanyika parokiani hapo. (Na Mpigapicha wetu)
DAR ES SALAAM
Na Remigius MMavele
Madilu System alikuwa mwanamuziki maarufu wa Kongo anayejulikana kwa ustadi wake wa hali ya juu wa sauti ambaye alipata umaarufu hasa kama mmoja wa waimbaji wakuu katika kundi la TP OK Jazz, bendi kubwa zaidi ya Kiafrika kuwahi kutokea.
Madilu aliyezaliwa mnamo Mei 28, 1952 jijini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo jina lake halisi Jean De Dieu Makiesse alianza kazi yake ya muziki mnamo 1969 na bendi iliyoitwa Symba, wakati wa mwanzo wa kazi yake, alikuwa mwimbaji wa bendi kadhaa ikiwa ni pamoja na Bamboula iliyoongozwa na Papa Noel, Les Etoiles, Festival des Macquisards iliyoongozwa na Sam Mangwana na Michelino na Fiesta Populaire iliyoongozwa na Faugus Izeidi.
DAR ES SALAAM
Na Arone Mpanduka
Mchezo wa kikapu wa tatu kwa tatu, maarufu kama 3x3, ni aina ya michezo ya mpira wa kikapu inayochezwa na timu mbili za wachezaji watatu kila moja, kwenye nusu uwanja (half-court) na bango moja la goli.
Mchezo huu una kasi ya juu, unadumu kwa dakika 10, ambapo timu ya kwanza kufikisha pointi 21, inapewa ushindi. Ni mchezo rasmi wa FIBA na sasa ni mchezo wa Olimpiki.
MADRID, Hispania
Baada ya zaidi ya miaka 14 huko Atletico Madrid, kocha Diego Simeone ameanza kufikiria maisha mapya nje ya klabu hiyo, huku maswali kwa mashabiki, yakiwa mengi kuhusu wapi atakapokwenda.
Tangu alipowasili kama Meneja mwaka wa 2011, Diego Simeone ameibadilisha Atletico Madrid, kutoka timu isiyofanya vizuri, ikipambana kupata uthabiti ndani na barani Ulaya, na kuwa timu yenye ushindi mkubwa, na kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Nairobi, Kenya
Mshindi wa zamani wa Marathon ya New York Albert Korir, amepigwa marufuku kwa miaka mitano, baada ya kukubali kutumia dawa za kuongeza nguvu mwilini.
Dar es Salaam
Na Nicolaus Kilowoko
Wakati kukiwa na uchunguzi wa vitendo vya upangaji wa matokeo, katika mashindano mbalimbali ya soka Tanzania Bara, huko visiwani Zanzibar, viongozi wa soka wameanza kuwashughulikia wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo.
Katibu wa Mashindano ya Kombe la FA Zanzibar, Ali Bakari, alielezea namna timu zinavyojihusisha na upangaji wa matokeo, katika mashindano ya Kombe la Shirikisho, na kutolea mfano timu waliyoifungia ya Taifa Jang’ombe, kutokana na kupanga matokeo.
Dar es Salaam
Na Mwandishi wetu
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu, amewataka Viongozi wa Halmashauri ya Walei, wanaochaguliwa ngazi mbalimbali za Kanisa Katoliki, kufanya kazi za kitume na sio kuleta majungu, umbea na kuchonganisha Mapadri.
Wito huo aliutoa wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia - Goba Mwisho, iliyokwenda sambamba na kumsimika Paroko mpya wa Parokia hiyo Padri Festo Liheta.
Askofu Mchamungu alisema kuwa viongozi wengi wa Halmashauri ya Walei, huwa wanasahau majukumu yao waliyochaguliwa katika kazi ya Kanisa, bali utakuta wanafanya kazi za Paroko au Paroko msaidizi na kuwamiliki Makasisi hao, “Msifanye hivyo viongozi, bali fanyeni kazi mlizochaguliwa na Waamini, acheni malumbano kila wakati na Mapadri.”