Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Tabora

Na Munir Shemweta

Zoezi la uthamini wa maeneo, yatakayopitiwa na ujenzi wa Mradi wa Reli ya Kisasa (Standard Gage Railway-SGR), kipande cha sita kutoka Tabora hadi Kigoma, linaendelea kwa kasi katika Wilaya sita za mikoa hiyo.
Wilaya hizo ni Tabora Mjini, Uyui, Urambo, Kaliua, Uvinza pamoja na Wilaya ya Kigoma.
Timu kutoka Ofisi ya Mthamini Mkuu wa Serikali, ikiongozwa na Mthamini Kiongozi FRV James Mark Mwanakatwe, ipo mkoani Kigoma, ikiendelea na kazi ya uhamasishaji pamoja na ukusanyaji taarifa za mali uwandani, kwa wananchi ambao maeneo yao yanaguswa na mradi huo.

Bagamoyo

Na Mathayo Kijazi

Wakristo wametakiwa kuepuka kiburi na majivuno, kwa kudhani bila wao mambo hayawezi kufanyika katika Kanisa, na jamii kwa ujumla.
Hayo yalisemwa hivi karibuni na Askofu wa Jimbo Katoliki la Bagamoyo, Mhashamu Stephano Musomba -OSA, wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, sanjari na kutoa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, katika Parokia ya Mtakatifu Toma – Muungano, jimboni humo.
“Tunaona katika Injili ya leo, yule Farisayo anamwambia Mungu ‘Mbona huoni? Mimi niko moja, mbili, tatu, mimi nafanya hiki na hiki, siwezi kuwa kama huyo, huyo ni mdhambi, huyo anatoza ushuru. Kwa hiyo anaona kwamba yeye ni bora kuliko yule mwingine. Na ndio maana kwa kuigaiga, tunaweza kusahau njia yetu ya kumwelekea Mungu.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Waamini wametakiwa kufuata mafundisho ya Bwana Yesu Kristo na mwenendo wake, kwa kuwarithisha watoto wao Imani Katoliki.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni, na Paroko wa Parokia  ya Mtakatifu Augustino-Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar  es Salaam, Padri Peter Assenga, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Ubatizo na Ekatisti.
“Mkristo kamili lazima awe amebatizwa na mwenye kushiriki Ekaristi Takatifu, na kufanya maungamo mara kwa mara,” alisema Padri Assenga.
Aidha, aliwasihi Waamini kutopokea Ekaristi Takatifu kama pipi, kwa sababu ni kufuru na ni dhambi.

ASMARA, Eritrea

Kanisa nchini Ethiopia na Eritrea, limeadhimisha Jubilei ya Miaka 50, ya kuinuliwa hadi utakatifu wa Mtakatifu Justin De Jacobis, kwa Misa Takatifu ya Shukrani iliyoongozwa na Askofu Mkuu Menghisteab Tesfamariam, akiambatana na wakubwa wa kidini na Mapadri zaidi ya 20, wa sherehe katika Kanisa Kuu la Mama Yetu wa Msaada wa Daima-Kidane Mehret.
Katika barua yake kwa Waamini wote na makutaniko ya kidini nchini, Askofu Mkuu Tesfamariam, aliwaalika kushiriki katika tukio hilo maalumu la kumshukuru Mungu na kumheshimu Mtume wa Imani Katoliki nchini, Mtakatifu Justin de Jacobis, ambaye alipandishwa cheo na Baba Mtakatifu Paulo VI, mnamo Oktoba 26, 1975.

NAIROBI, Kenya

Wanafunzi wa Vyuo Vikuu kutoka Taasisi 26 za Elimu ya Juu nchini Kenya, wamepewa ujuzi unaojumuisha ubora wa kiakili na huduma ya kujitolea, ili kufikia uongozi wenye mabadiliko na athari kubwa kwa jamii.
Programu ya Uongozi ya Kizazi Kijacho (NGLP), ambayo hapo awali ilikuwa Programu ya Udhamini wa Kikatoliki, ambayo inazingatia mafunzo ya kitaaluma na uongozi kwa wanawake, wanaume, na Waamini wa kidini wa Kiafrika, inawafunza wasomi wake kuwa Miale ya Matumaini, ambapo imeitwa Kutumikia, Kubadilisha, na Kuhamasisha.
Katika tafakari iliyotolewa na Padri John Webootsa, mwanachama wa Comboni Missionaries of the Heart of Jesus (MCCJ), kwa zaidi ya wanafunzi 150 wakati wa kumbukumbu zao katika Bustani ya Ufufuo, katika Mji Mkuu Nairobi, Kenya, alisema kuwa jamii kwa sasa ina njaa ya uongozi halisi na uwazi wa maadili.

VATICAN CITY, Vatican

Katibu Mkuu wa Vatican, Mwadhama Pietro Kardinali Parolin, ametaka ushiriki wa Marekani na jukumu kubwa kwa Ulaya, katika juhudi za kukomesha mzozo wa Ukraine, akisisitiza kwamba China pia ina neno la kusema kwa ajili ya amani.
Aliyasema hayo hivi karibuni, aliposhiriki katika Hospitali ya Watoto ya Bambino Gesù, akiashiria kumbukumbu ya miaka 40 ya kutambuliwa kwake, kama Taasisi ya Kisayansi ya Kulazwa Hospitalini na Matibabu.
Akizungumzia mkutano na Waziri Mkuu wa Hungaria, Viktor Orbán, aliuelezea kama majadiliano mazuri, na kwamba wanajaribu kuleta misimamo yao karibu zaidi.

DAR ES SALAAM

Na Shemasi George Timalias

Karibu ndugu msikilizaji wa Radio Vatican, katika tafakari hii, inayotugusa kwa karibu sana, ambayo inakumbusha Sikukuu ya Watakatifu wote, kila ifikapo tarehe Mosi Novemba ya kila mwaka, lakini pamoja na Watakatifu, kuna ndugu zetu Marehemu wote waliotutangulia mbele ya haki, ambapo Mama Kanisa anatupatia fursa ya kuwakumbuka, kila ifikapo  tarehe 2 ya mwezi Novemba na kuendelea hadi mwisho wa mwezi.
Kwa hiyo tuanze tafakari hii, sehemu ya kwanza ya Watakatifu. Fundisho kuu tunalopata katika siku hii ya watakatifu wote, ni msisitizo wa maisha yetu kuishia mikononi mwa Mungu aliyetuumba huko mbinguni.

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya kuibuka kwa Dola ya Kikristo, hususani tuliwajuza kuhusu Faida na Hasara za Dola ya Kikristo. Leo tunawaletea historia ya Miundombinu ya Kanisa kuanzia Karne ya nne na tano. Sasa endelea…

Watumishi wa Kanisa na Mitaguso:
Bwana wetu Yesu Kristo, aliacha amewachagua na kuwaweka mitume 12 na wafuasi 70 (72), ili waendeleze kazi aliyoianza (Lk. 6:13-16; 10:1-12). Hawa walirithiwa kama Maaskofu na Mapadri.
Katika Kanisa la mwanzo, polepole kufuatana na mahitaji katika misingi aliyoiweka Kristo, miundombinu hiyo iliongezeka na kuboreshwa.
Kuanzia Karne ya nne na tano, palikuwepo na madaraja saba katika watumishi wa Kanisa. Kati ya madaraja hayo, madogo ni manne yakiwemo Mfungua Mlango, Msomaji, Mtoa Mashetani na Mtumishi wa Ibada, na madaraja makubwa ni matatu, Ushemasi, Upadri na Uaskofu.

Padri Andreas Chitanda Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Malkia-Luagala Jimbo Katoliki la Mtwara, akibariki kinanda kipya cha Kigango cha Kutukuka kwa Msalaba-Lyenje jimboni humo, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika iliyoadhimishwa hivi karibuni.

Waimarishwa wa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wa Parokia ya Mtakatifu Toma – Muungano, Jimbo Katoliki la Bagamoyo, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti hiyo, iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha na Mathayo Kijazi)