Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Na Arone Mpanduka

Alizaliwa Antoine Nedule Monswet mnamo Desemba 25, 1940, huko Leopoldville (sasa Kinshasa), jina la kisanii la Papa Noel kulikuwa na maelezo kuwa jina Noel lilikuja kutokana na  kuzaliwa kwake kwa Siku ya Krismasi. Papa Noel mwenyewe alifafanua kuwa kinyume na imani ya wengi, jina la Papa Noel (aliyezaliwa Antoine Nedule Monswet) halina uhusiano wowote na siku ya Krismasi, lakini jina hilo ni la kisanii kutoka kwa mshauri wake Leon Bukasa.Papa Noel Alianza kucheza gitaa ambalo mama yake alimpa, na mnamo 1957 aliombwa kufanya kazi na Léon Bukasa kwenye studio yake ya rekodi.
Papa Noel alisema kuwa ni gwiji Leon Bukasa ambaye alimpa jina la kisanii la “Papa Noel’, ambalo liliandikwa kinyume cha jina lake la Leon.
Mara baada ya hapo, aliombwa ajiunge na kikundi kipya cha Rock-A-Mambo,katika miaka iliyofuata, alikuwa mwanamuziki katika bendi kadhaa zilizokuwa maarufu wakati huo , Orchester Les Bantous de la Capitale kutoka Brazzaville, African Jazz, na Orchester Bamboula, ambapo alikuwa kiongozi wa bendi.
Kuanzia 1978 na kuendelea, alikuwa mpiga gitaa katika T.P.O.K iliyokuwa chini ya gwiji Franco ambapo alidumu na kundi hilo kwa miaka kumi na moja hadi kifo cha Franco mnamo 1989. Mwaka 1984 Papa Noel alitengeneza albamu yake binafsi inayoitwa “Bon Samaritain”, ambayo haikumfurahisha Franco ambaye hakupenda washiriki wa bendi yake kuwa na albamu zao binafsi .
Mnamo 1991, baada ya kifo cha Franco, TPOK Jazz ilizuru Ulaya, mwishoni mwa ziara hiyo, baadhi ya wanamuziki wa bendi hiyo waliamua kuhamishia makazi yao jijini Brussels nchini Ubelgiji na kuunda bendi ya Bana OK, Papa Noel alikuwa miongoni mwao. Alishiriki katika albamu ya Rondot ya Bakitani , ambayo ilitolewa kwa jina la Bana OK.
Papa Noel anaonekana kama mpiga gitaa anayeheshimika, katika upigaji wa magita yote yaani solo, rhythm na mi-solo ambaye alijizolea sifa kubwa ulimwenguni kote. Licha ya kutoa albamu yake binafsi mwaka 1984, Papa Noel amefanikiwa kushiriki katika albamu ya Sam Mangwana  Galo Negro (1998) uliovuta hisia zaidi kwake.
Mnamo 2000, albamu ya mkusanyiko << Bel Ami » ilitoka, ikifuatiwa na albamu ya kwanza ya Kékélé mnamo 2001.
Miradi mipya ilianzishwa, kama vile vipindi vya kurekodi na wanamuziki wa Cuba Adan Pedroso na Papa Oviedo, kujaribu kuchunguza mizizi ya pamoja ya muziki wa afro-cuba na rumba ya Kongo. Ugonjwa wa Papa Noël (Nedule ana kisukari) ulimzuia kwa muda kushiriki katika tamasha zaidi na ubia mpya. Hata ilimbidi kukosa albamu ya Kékélé ya 2003. Mnamo 2004, hata hivyo, alizunguka na kikundi kilichoitwa Bana Congo, na waimbaji Nana na Baniel (wote waliwahi kuwa na OK Jazz) na bendi ya Cuba nzima.
Maisha ya Papa Noel yanakaribia historia nzima ya muziki maarufu wa Kongo alianza kuonyesha uwezo wake katika muziki akiwa na umri wa miaka kumi na saba , aliingia studio ya Léopoldville’s (Kinshasa) ili kumsaidia mwimbaji- gitaa mwanzilishi Léon Bukasa.
Rekodi yao ya 1957 kuhusu mwanamke anayeitwa “Clara Badimwene” ilikuwa ya kwanza kwa Noel na mwaka uliofuata alihamia studio ya Esengo na kucheza na bendi iitwayo Rock’a Mambo iliyoongozwa na wanamuziki kutoka Kongo-Brazzaville, mkali Jean Serge Essous na mpiga sax Nino Malapet.
Mwaka wa uhuru wa kisiasa wa Kongo hizo mbili, 1960, Noel huko Gabon alishirikiana na Mbrazzaville mwingine, Guy-Léon Fylla, na bendi yake Makina Loka. Mwishoni mwa mwaka huo huo Noel alihamia katika bendi ya Bantous de la Capitale huko Brazzaville ambapo sifa yake ilipata mng’ao wa kwanza. Akiwa na bendi ya Bantous, Papa Noel alishiriki kikamilifu kwenye kundi hilo katika nyimbo kama vile “Basili Koyokana” (hawaelewi tena) na “Mobali Liboso” ( mwanaume kwanza).

DAR ES SALAAM

Bondia wa Masumbwi nchini, Hassan Mwakinyo amesema kuwa ujio wa pambano lake la ‘Usiku wa Utetezi wa Mkanda” ni sehemu ya kudhihirisha utemi wake kwenye mchezo huo.
Mwakinyo anautetea mkanda wake wa WBO Afrika aliouweka kama rehani ili kurudisha hadhi yake kwenye viwango vya ubora vya mchezo huo.
Pambano hilo litakalo fanyika Tarehe 16 Novemba 2024 katika ukumbi wa Werehouse Masaki Jijini Dar es Salaam, na litakuwa pambano ambalo litatoa taswira ya ubora wa bondia huyo kutoka hivi karibuni kuingia katika mvutano mkubwa na baadhi ya mabondia wenzake.
Hassan Mwakinyo amewaomba wadau na wapenzi wa mchezo wa ngumi kujitokeza kwa wingi siku hiyo kuona ukubwa wake kwenye masuala ya ngumi.
“Maisha yangu siku zote mimi ni mapigano kutokana na dunia ninayoishi, hivyo hata mpinzani wangu atambua hilo kuwa sitamuacha salama kutokana  na maandalizi niliyoyafanya”, alisema Mwakinyo.

DAR ES SALAAM

Klabu ya soka ya Tabora United imesema kwamba timu yoyote inayotaka huduma ya mchezaji wao Offen Chikola, inapaswa kutoa kitita cha shilingi bilioni moja ili imsajili.
Chikola kwa sasa anaimbwa na wapenzi wa soka nchini kwa mabao yake mawili aliyofunga hivi karibuni kwenya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Yanga katika uwanja wa Azam Complex, jijini Dar es salaam.
Akizungumza na gazeti Tumaini Letu kwenye mahojiano maalum hivi karibuni, Afisa Habari wa Tabora United ambaye pia anakaimu nafasi ya Mtendaji Mkuu, Christina Mwagala, alisema Chikola ana thamani kubwa kuliko watu wanavyodhani, na kwamba hiyo haitokani na kuifunga Yanga, isipokuwa thamani yake ni ya muda mrefu.
Alisema kwamba kwa kuwa mchezaji huyo bado ana mkataba wa muda mrefu na Tabora United, timu inayomtaka inabidi ijipange vilivyo kuvunja kibubu ili kumsajili.
“Sisi kila mchezaji wetu ana thamani kubwa.Huyu Chikola ni Mtanzania mwenzetu kutoka Morogoro tu pale. Wapo wale wa kimataifa, nao ukitaka kuwasajili bei yao imechangamka.Na thamani yao inaendana na wanachokifanya uwanjani.Sote tunaona Tabora United jinsi inavyocheza,”alisema Christina.
Alisema kuwa wachezaji wote wa Tabora wana ubora mkubwa, na kwamba hicho ndicho wanachojivunia kwa sasa huku wakiwa na matumaini ya kufanya vizuri katika msimu huu.
“Sisi malengo yetu ni kuwa mabingwa, na si vinginevyo.Tunaziheshimu sana timu za Simba na Yanga, lakini safari hii tunataka zitupishe kidogo ili na sisi tutambe na taji la ubingwa,”alisema.
Chikola ambaye ni kiungo mshambuliaji wa Tabora United, hadi sasa amefunga mabao matatu katika Ligi Kuu, huku akionyesha nia ya kutaka kuendelea kufunga mabao mengine.
Mabao hayo yote matatu amefunga kwa kutumia mguu wake wa kushoto, sawa na Nassoro Saadun wa Azam FC, na Joshua Ibrahim wa Ken Gold.

NEW DELHI, India
India imeliarifu Baraza la Kimataifa la Kriketi kwamba haitasafiri kwenda kwenye Kombe la Mabingwa, kulingana na wenyeji Pakistan.
Mvutano wa kisiasa unaoendelea, unamaanisha kuwa nchi hizo mbili hazijacheza nje ya mashindano makubwa ya wanaume tangu mwaka 2013, wakati India haijacheza nchini Pakistan kwa miaka 16.
Pakistan inatazamiwa kuandaa hafla ya kimataifa kwa mara ya kwanza tangu 1996 mwezi Februari, na Machi mwaka ujao, timu nane, zaidi ya 50 ya Mabingwa.
Lakini, Bodi ya Kriketi ya Pakistani (PCB) ilisema Bodi ya Udhibiti wa Kriketi nchini India imeiambia ICC timu ya India haitavuka mpaka.
“TAKUKURU imepokea barua pepe kutoka kwa ICC, ikisema kwamba BCCI imewafahamisha kwamba timu yao haitasafiri hadi Pakistan kwa ajili ya Kombe la Mabingwa wa ICC 2025”, alisema msemaji wa PCB.
Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza baada ya siku mia moja, tarehe 19 Februari. Ratiba bado inapaswa kuthibitishwa na ICC.
ICC haijajibu moja kwa moja taarifa ya PCB, lakini iko kwenye majadiliano na Pakistan na mataifa mengine saba yanayoshindana juu ya ratiba. BCCI imeombwa majibu.

LONDON, Uingereza
Mwamuzi wa Premier League, David Coote (kushoto) amesimamishwa baada ya video inayodaiwa kumuonyesha akitoa kauli za dharau kuhusu Liverpool na meneja wa zamani wa klabu hiyo Jurgen Klopp, kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii.
Bodi ya Waamuzi PGMOL inasema kusimamishwa kutaanza kutumika mara moja na inasubiri uchunguzi kamili.
Video hiyo, iliyosambazwa sana kwenye mitandao ya kijamii, haijathibitishwa na haijulikani ni lini ilirekodiwa au uhalisi wake.
Coote, 42, alichezesha ushindi wa 2-0 wa Liverpool dhidi ya Aston Villa Jumamosi na ni mmoja wa maafisa wa Premier League walio na uzoefu mkubwa, na amekuwa waamuzi katika ligi kuu tangu 2018.
Video inayoshirikiwa inaonekana kurejelea mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza ambayo Coote alisimamia mechi kati ya Liverpool na Burnley mnamo Julai 2020, ambayo iliisha 1-1.
Klopp alimkosoa Coote baada ya mechi, akisema mwamuzi alishindwa kutoa faulo kwa changamoto zilizowakabili wachezaji wa Liverpool.

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, Naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.

Salamu Maria umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.

Maria Mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

Ndimi mtumishi wa Bwana, Nitendewe ulivyonena.

Salamu Maria umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.

Maria Mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

Neno wa Mungu akatwaa mwili, Akakaa kwetu.

Salamu Maria umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa.

Maria Mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu.

Amina.
Utuombee mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.

Tuombe:
Tunakuomba Ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika, kwamba Kristo mwanao amejifanya mtu;

kwa mateso na msalaba wake, utufikishe kwenye Utukufu wa ufufuko.
Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu.

Atukuzwe baba na mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina x3

Raha ya Milele, uwape Ee Bwana na Mwanga wa Milele uwaangazie, Wapumzike kwa amani. Amina x3

Mt. Yosefu, mfano wa watu wote wanaofanya kazi, unijalie neema ili nifanye kazi kwa bidii, nikifanya wito wa kazi zaidi kuliko kawaida;

nifanye kazi kwa moyo wa shukrani na furaha, nikiona heshima ya kufanya kazi na kuleta maendeleo kwa njia ya fadhili zitokazo kwa Mungu,

bila kujali matatizo na uchovu, nifanye kazi zaidi kwa nia njema, na kuepuka ubinafsi wakati huo daima nikiona kifo mbele yangu,

na hesabu ambayo nitapaswa kutoa kutokana na muda ninaopoteza, mema ninayoshindwa kutenda, mawazo batili ya mafanikio,

ambayo ni hatari kwa kazi ya Mungu. Yote kwa ajili ya Yesu, yote kwa ajili ya Maria, yote kutokana na mfano wako, Ee Baba Mt. Yosefu.

Hili litakuwa neno langu la kuzingatia katika Maisha na hata kifoni. Amina.

Ee, Mtakatifu Yosefu ulikuwa mtiifu kabisa kwa maongozi ya Roho Mtakatifu.

Unijalie neema ya kujua hali yangu ya maisha ambayo Mungu katika ukarimu wake amenichagulia.

Kwa furaha yangu hapa duniani, na Pengine hata kuhusu hatima yangu huko Mbinguni, itategemea uchaguzi huu,

nisiwe mwenye kudanganyika kwa kufanya hvyo. Nipatie mwanga wa kujua mapenzi ya Mungu,

na kuyatekeleza kwa uaminifu, na kuchagua wito ambao utaniongoza kwenye heri ya milele.

Sala Zetu...

Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri na Viongozi wa Kamati Tendaji ya Parokia ya Mtakatifu Vincent wa Paulo, Kibamba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.