Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Nairobi, Kenya
Mwendesha baiskeli wa Kenya Suleiman Kangangi amefariki dunia kufuatia ajali ya mwendo kasi katika mbio za magari nchini Marekani siku ya Jumamosi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 ambaye alikuwa akishiriki mbio za changarawe za Overland huko Vermont, shindano la kilomita 59 la barabara za udongo, likijumuisha takriban futi 7,000 za kupanda.
Kangangi alimaliza wa tatu katika Tour of Rwanda mwaka wa 2017 alipokuwa akikimbilia timu ya UCI Continental ya Ujerumani, Bike Aid, kabla ya kubadili mbio za changarawe.
Kwa upande wake Rachel Ruto, mke wa rais mteule William Ruto wa Kenya, alichapisha kwenye Twitter, “Sote tutamkosa kama mtu binafsi. Kenya imepoteza bingwa. Pumzika kwa amani Sule”.
Nayo taarifa ya klabu yake ilisema, “Sule ni nahodha wetu, rafiki, kaka. Yeye pia ni baba, mume na mwana”.

DAR ES SALAAM

Na Nicolaus Kilowoko

Kocha Msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars Mecky Mexime amefunguka kuwa kwa sasa Watanzania wanapaswa kuganga yajayo, hasa katika kuwekeza nguvu na mapenzi juu ya timu yao ya Taifa.
Mexime ameyasema hayo mara baada ya Watanzania wengi kusikitishwa na matokeo ya Taifa kushindwa kufurukuta katika mashindano mbalimbali wanayoshiriki, na kusababisha wengi kuumia.
Mexime alisema kuwa kwenye mpira hakuna kukata tamaa, na matokeo siku zote ni ya pande tatu, hivyo kwa sasa si vyema kulaumu sana, ila ni kuongeza nguvu kwa pamoja kama Watanzania.
Alisema kuwa timu ya Taifa ni ya Watanzania wote, na si ya mtu mmoja. Hivyo, kila jambo linawezekana ikiwa mataifa mengine yanafanikiwa kushiriki mashindano makubwa, hata Tanzania inaweza kushiriki katika mashindano hayo.
“Siku zote kuteleza siyo kuanguka, na hata kama ukianguka, unapaswa kusimama tena. Watanzania wazidi kupenda vya kwao na kuongeza nguvu kwa pamoja katika kuijenga timu yetu, na siyo kulaumu mtu”, alisema Mexime.
Alisema kuwa mchezo wa mpira kwa sasa ni vyema wote kwa pamoja tukatengeneza mkakati wa pamoja ili tuweze kufanya vyema katika michuano inayofuata na inayoshiriki timu hiyo.
Stars ilishindwa kufurukuta katika uwanja wa Benjamin Mkapa wakati wa mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya wachezaji wanocheza ligi za ndani, CHAN, mbele ya timu ya Taifa ya Uganda kwa kufungwa bao 1-0.
Huu ni mwendelezo wa matokeo mabovu ambayo Stars wameendelea kuyapata baada ya misimu iliyopita kushindwa kufuzu kucheza Kombe la Dunia, Afcon, Chan pamoja na michezo mbalimbali ya kirafiki.
Meck Maxime anachukua nafasi ya kocha msaidizi mara baada ya kuvunjwa kwa benchi la ufundi la Stars kutokana na matokeo mabovu. Hivyo anaungana kwa sasa na kocha Mkuu, Hanour Janza, akisaidiwa na kocha wa magolikipa, Juma Kaseja.
TFF ilitangaza kukubaliana na aliyekuwa kocha wa timu hiyo Kim Poulsen kumbadirishia majukumu, na sasa atabaki katika timu za vijana za Taifa.
Ikumbukwe kuwa Kim alitangazwa na TFF kuwa Kocha Mkuu wa Stars, Februari 15 mwaka 202, kabla yake aliwahi kuwa kocha wa Stars mwaka 2012 na 2013.
Kim mpaka anawekwa pembeni, amepoteza mechi 7, akipata ushindi kwenye mechi 6, na sare kwenye mechi 4. Alipewa mkataba wa miaka mitatu kuinoa timu ya Stars.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Afisa Habari wa Klabu ya soka ya Ruvu Shooting, Masau Bwire amesema kuwa timu yake imeanza maandalizi ya sherehe za ubingwa wa Ligi Kuu ya msimu huu, licha ya kwamba bado ni mapema.
Akizungumza hivi karibuni katika mahojiano maalum, Bwire alisema kwamba wanajivunia maandalizi waliyofanya kabla ya msimu kuanza na sasa wana kikosi imara.
Alisema pia kuwa wamesajili kikosi kizuri ambacho kinaweza kuhimili ushindani katika Ligi ikilinganishwa na timu zingine.
“Sisi tuna kikosi kizuri, na falsafa yetu siku zote ni kuwa na wachezaji wazawa.Hicho ndicho kitu tunachojivunia.Wanaotudharau wakija kucheza na sisi watakiona cha mtema kuni,”alisema Bwire.
Alisema kwamba hakuna timu iliyoandikiwa kupata ubingwa siku zote kwa sababu ubingwa ni haki ya kila timu inayowania, na kwamba hawapo kwenye Ligi kwa ajili ya kupoteza muda au kusindikiza tu timu zingine.
“Huwa tunasikia tu eti kuna timu zimesajili Wazungu, zingine Wabrazil, zingine Wajapan, lakini sisi hatutetereshwi na mbwembwe zao.Sisi tutawaonyesha uwanjani”       
Alisema kuwa kuna timu zinawadharau, lakini mechi inapokaribia matumbo yao yanavurugika kwa hofu ya kufungwa.