Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Makosa ya jinai yaongezeka

September 02, 2022

MOSHI

Na Mwandishi wetu

Mkuu wa Jeshi la Polisi (Inspector General of Police: IGP) nchini, Camillus Wambura amesema kwamba takwimu za makosa makubwa ya jinai nchini yameongezeka katika kipindi cha Januari hadi Juni mwaka 2022.
IGP Wambura aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha maofisa wa waandamizi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, na makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi, akisema kuwa makosa hayo yameongezeka kutoka 24,848 kipindi kama hicho mwaka 2021 hadi makosa 27,848, sawa na ongezeko la asilimia 11.2.

CWT wahofia michango yao

September 02, 2022

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Wanachama wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wamesema wamekumbwa na mashaka kuhusu matumizi ya michango yao.
Kwa nyakati tofauti, wanachama hao  wamesema hawana imani kama michango yao bado ipo salama kutokana na hali ya namna ilivyokuwa ikiendeshwa ndani ya CWT.

DODOMA

Na Ndahani Lugunya

Wakristo nchini wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo, kuchangia Pato la Taifa, na kutatua changamoto katika maeneo yao.
Hayo yalielezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, George Simbachawene, wakati akizunguma katika sherehe ya kumweka wakfu Askofu wa  tatu wa Kanisa  la Anglikana, Dayosisi ya Mpwapwa, George Chiteto, iliyofanyika Jijini Dodoma, baada ya aliyekuwa Askofu wa Kanisa hilo, Askofu Donald Mtetemela kustaafu.
Simbachawene alisema kuwa changamoto nyingi za kiuchumi katika jamii zitatatuliwa endapo wananchi watajituma kufanya kazi na kuwa wabunifu  kwa kuanzisha miradi mbalimbali, kama ambavyo Maandiko Matakatifu yanavyoagiza watu kufanya kazi.
“Lazima Wakristo wa sasa tufanye kazi, lazima tutatue changamoto kwenye maeneo yetu kwa sababu imeandikwa katika Biblia, ‘asiyefanya kazi na asile’, kwa hiyo kufanya kazi ndio uhai wako, heshima yako na ukizalisha, utaweza kuendesha maisha yako binafsi,” alisema Simbachawene.
Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi za Dini, kwani zimekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo, kusimamia maadili na kupambana na vitendo vya mmomonyoko wa maadili kwa baadhi ya watu wasio na hofu ya Mungu.
Aidha, alibainisha kwamba Serikali inaendelea  kuchukua hatua za kisheria kwa watu wote wanaojihusisha na vitendo vya rushwa, ufisadi, utovu wa nidhamu kwa watumishi wa umma, pamoja na jamii kwa ujumla.
Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dk. Maimbo  Mndolwa, aliipongeza Serikali kwa kuwa mstari wa mbele kuziunga mkono Taasisi za Dini  katika nyanja zote, huku akimtaka Askofu Chiteto kufanya kazi kwa kumtegemea Mungu, hatimaye kufikia malengo ya Kanisa.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary  Senyamule  aliwataka wakazi wa mkoa huo kutumia fursa ya Serikali  kushusha bei ya  mbolea kwa kujikita katika kilimo.

Washington DC, USA
Mwanasiasa wa Kamanda wa Washington, Brian Robinson amefanyiwa upasuaji baada ya kupigwa risasi wakati wa jaribio la wizi wa kutumia silaha, au wizi wa gari.
Nyota huyo wa Washington Commanders, Brian Robinson alipata majeraha yasiyo ya kutishia maisha, baada ya kupigwa risasi.
Idara ya Polisi ya Washington DC ilisema kwamba Robinson alipata majeraha mawili ya risasi kwenye chini ya mguu wakati wa tukio hilo lililotekea Jumapili.
Tukio hilo lilitokea mwendo wa saa 18:00 kwa saa za huko, katika mji mkuu wa Marekani. Polisi walisema washukiwa wawili walitoroka eneo la tukio, na bunduki ilipatikana karibu.
Siku ya Jumatatu, Robinson aliandika kwenye Instagram kwamba “upasuaji ulikwenda vizuri.”
Kocha wake mkuu Ron Rivera alimtembelea Robinson Jumapili jioni, na kusema Robinson “anaendelea vyema”.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi (mwenye Fimbo ya Kiaskofu), akiwa na Maaskofu Wasaidizi wake, Mhashamu Henry Mchamungu (mbele kulia), na Mhashamu Stephano Musomba (mbele kushoto), wakiwa katika Maandamano ya kuingia katika viwanja vya Seminari Ndogo ya Visiga, kwa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kilele cha Miaka 50 ya Jubilei ya WAWATA, Jimboni humo. (Picha na Yohana Kasosi)

Page 1 of 3