Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

NAIROBI, Kenya

Katibu Mkuu wa Chama cha Mabaraza ya Maaskofu Wanachama Afrika Mashariki (AMECEA), Padri Anthony Makunde wakati wa uzinduzi wa Sera ya Mawasiliano ya AMECEA, ameeleza kuwa waraka huo unaweza kutumika kama mwongozo wa mikutano mingine katika kanda hiyo, wakati wa kuandaa sera zao za mawasiliano.
Akiwahutubia washiriki mtandaoni na waliokuwepo  wakati wa uzinduzi, katika Madhabahu ya Consolata jijini Nairobi, Kenya, Padri Makunde alisema “Sera ya Mawasiliano ya Kijamii sio waraka wa ndani wa Sekretarieti tu, bali inakusudiwa kutumika kama marejeleo ya mikutano ya wanachama na dayosisi, wakati wanaunda sera zao za mawasiliano kitaifa na Jimbo.

NAIROBI, Kenya

Chama cha Wanachama wa Mabaraza ya Maaskofu Afrika Mashariki (AMECEA), kimezindua Sera yake ya Mawasiliano na kuzindua Programu mpya ya redio ya kidijitali.
Afisa kutoka Kongamano la Mabaraza ya Maaskofu Afrika na Madagascar (SECAM), Charles Ayetan, amepongeza hatua hiyo akisema kwamba hatua hiyo muhimu sio tu kuhusu teknolojia, bali pia ni kuhusu kuimarisha ushirika, ushirikiano na utume wa Kanisa wa Uinjilishaji.

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu amezindua Warsha kwa Waamini wote wa Jimbo hilo, inayotarajiwa kufanyika Novemba 29 mwaka huu, katika viwanja vya Parokia ya Kristo Mfalme - Tabata.
Uzinduzi huo aliufanya hivi karibuni Posta jijini Dar es Salaam, akiwasihi Waamini wote kujiandikisha na kushiriki kwa wingi katika Warsha hiyo, ambapo ndani yake kutakuwa na semina itakayohusisha mada mbalimbali.

Dar es Salaam

Na Laura Mwakalunde

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewasihi Waamini kuacha kuzificha imani zao kwa kubadilika badilika kila wakati.
Aliyasema hayo hivi karibuni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Martha- Mikocheni jimboni humo.

Morogoro

Na Angela Kibwana

Kanisa Katoliki limehitimisha mfungo maalumu kote nchini, ambapo Wakatoliki walifunga, kuabudu Ekaristi Takatifu na kuiombea nchi haki na amani, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Hatua ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), kutoa sala maalumu na agizo la kuwashirikisha Waamini kufunga, kusali na kuombea haki na amani si mara ya kwanza, bali limefanya hivyo mara kwa mara hasa inapoonekana kuna viashiria vya uvunjifu wa amani, ambayo ni tunda la haki.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amelipongeza Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), kwa kuongezeka kwa thamani ya soko hilo na kufikia shilingi trilioni 21.0, katika kipindi cha kufikia Julai mwaka huu.
Waziri Mkuu Majaliwa alisema  kwamba, soko hilo limeongeza ukuaji wa mauzo ya hisa kwa zaidi ya asilimia 246, pamoja na ongezeko la idadi ya wawekezaji hadi zaidi ya akaunti 683,000, ikiwa ni ishara ya ukuaji imara wa sekta ya mitaji nchini.

Ahadi ya serikali ya kufikisha umeme wa gridi ya taifa katika wilaya zote za Mkoa wa Kagera, imetekelezwa baada ya kusaini mikataba ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 220, kutoka Benako-Ngara hadi Kyaka wilayani Misenyi.
Aidha, hatua hiyo imekwenda sanjari na kituo cha kupoza umeme cha Benako cha msongo wa kilovoti 220/33, na kutoa uhakika kwa Mkoa huo kupata umeme wa gridi na kuacha kutegemea umeme kutoka Uganda.

Askofu wa Jimbo Katoliki la Kahama Mhashamu Christopher Nkoronko, (pichani) amewataka Waimarishwa kuwa tofauti na wengine hasa wanapokuwa kanisani, nyumbani au shuleni.
Alisema hayo hivi karibuni, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, iliyofanyika katika Parokia ya Watakatifu Joachim na Anna-Mwime Jimbo Katoliki la Kahama.

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Waandishi wa Habari wametakiwa kuwa wabunifu na wenye kujitolea kufanya vitu vya tofauti katika kazi zao, ili waweze kuzalisha vipindi na habari zenye ubora.
Hayo yalisemwa na Derik Murusuri, Mwezeshaji katika Semina ya Waandishi wa Habari, iliyofanyika hivi karibuni Msimbazi Centre, jijini Dar es Salaam.

Mtwara

Na Mwandishi wetu

Askofu wa Jimbo Katoliki la Musoma, Mhashamu Michael Msonganzila amewataka wanawake kuwa wanyenyekevu kama Mama Bikira Maria.
Alisema hayo wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 40 ya Parokia, na Miaka 20 ya Utume wa Padri Fintani Mrope, Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme, Tandahimba Jimbo Katoliki la Mtwara, iliyofanyika parokiani hapo.
Askofu Msonganzila alisema kwamba Waamini wengi wanayumbayumba kila sehemu katika imani, hiyo yote ni kutangatanga bila kuelewa wanachokitafuta.