DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam amewataka Waamini kumtangaza Kristo, aliyefufuka kutoka kwa wafu.
Kardinali Pengo aliyasema hayo hivi karibuni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Pasaka, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Benedicto Abate-Wazo Hill.
“Katika kumtangaza Kristo inatakiwa uwe tofauti na wengine kwa sababu wewe umepata Sakramenti, na uwe na msimamo wa kiimani na siyo kusema tu kwa sababu ni
maneno ambayo umeambiwa au kuhadithiwa, bali aone katika maisha yako kwamba una imani hiyo iliyo thabiti,”alisema Kardinali Pengo.
Kardinali Pengo alisema kwamba Kristo alimuita kila mmoja kudhihirisha ufufuko wake katika maisha ya kila mtu, na hiyo ndio iliwaongoza wafuasi wa Bwana tangu mwanzo wake na wote walikubali kufa kwa sababu hiyo.
Dar es Salaam
Na Laura Mwakalunde
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddeaus Ruwa’ichi amewataka Wanakwaya kutambua kwamba wanapoimba muziki Mtakatifu, wazo sio kutumbuiza bali ni kuinjilisha.
Rai hiyo aliitoa hivi karibuni katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Utume wa Kwaya Katoliki Tanzania (UKWAKATA), Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Petro-Oysterbay, jimboni humo.
“Wanakwaya siyo watumbuizaji na kama unataka kutumbuiza, basi ni vyema kwenda kwenye mahall ya disco… lakini ukitaka kuinjilisha kwa kuishi ukristo wako na katika kanisa lako, huku ukimshukuru Mungu kwa zawadi ya kipaji alichokujalia cha kuinjilisha kwa njia ya kuimba, salia Kanisani,”alisema Askofu Mkuu Ruwa’ichi.
Aidha, alisema kuwa kila mbatizwa anaitwa kuwa shahidi wa Kristo kwa kutumia Kipaji alichojaliwa na Mungu, akiwaasa Wanaukwakata hao, kutumia vyema vipawa vyao.
Dar es Salaam
Na Mwandishi wetu
Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia-Goba Mwisho, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Musa Kihoo, amewataka Waamini kufuata mafundisho ya Bwana Yesu Kristo, kwa sababu yeye ni njia ya ukweli ya kwenda Mbinguni.
Padri Kihoo alisema hayo wakati wa Ibada ya Ijumaa Kuu, Kuabudu Msalaba Mtakatifu iliyofanyika parokiani hapo.
Padri Kihoo alisema kwamba Waamini wengi wanamchukiza Bwana Yesu Kristo kwa kutenda dhambi, ikiwemo kusema uwongo, umbeya, kusengenya wenzao, kunyanyasa wapangaji na ujambazi.
VATICAN CITY-Vatican
Maadhimisho ya kumtangaza Mwenyeheri Carlo Acutis kuwa Mtakatifu yamesitishwa kufuatia kifo cha Papa Fransisko.
Maadhimisho hayo yaliyokuwa yafanyike Dominika ya Aprili 27, mwaka huu yamesitishwa kusubiria kupatikana kwa Baba Mtakatifu mpya.
Kijana huyo aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 15, kwa sababu ya ugonjwa wa saratani ya damu Oktoba 12, mwaka 2006 tayari ametangazwa Mwenyeheri huko Assisi Oktoba 10, mwaka 2020.
Mwili wake umekuwa ukipumzika tangu 2019, katika Kanisa la Mtakatifu Maria Mkuu (Maria maggiore), Assisi.
Kwa njia hiyo Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican imefahamisha kwamba, Adhimisho la Ekaristi Takatifu na ibada ya kutangazwa kuwa Mtakatifu iliyopangwa kufanyika katika Maadhimisho ya Jubilei ya Vijana, imesitishwa.
VATICAN City
Mkutano Mkuu wa kwanza wa Makardinali umeanza Aprili 22 mwaka huu, ikiwa ni siku moja baada ya kifo cha Baba Mtakatifu Fransisko.
Mkutano huo ulidumu kwa muda wa saa moja na nusu, ambapo Makardinali waliokuwepo katika Ukumbi wa Sinodi mpya walikuwa 90, walioanza kikao hicho kwa muda wa sala kwa ajili ya Papa Fransisko.
Makardinali hao waliapa kwa kuzingatia na kwa uaminifu kanuni za Katiba ya Kitume (Universi Dominici Gregis), kuhusu nafasi ya Kiti kilicho wazi cha Kitume na kuchaguliwa kwa Papa wa Roma, kasha wakaimba (Adsumus Sancte Spiritus), wimbo wa kumuomba Roho Mtakatifu awaangazie.
VATICAN CITY, Vatican
Miongoni mwa maneno ya mwisho ya Baba Mtakatifu Fransisko yalikuwa ni shukrani zake kwa msaidizi wake wa afya binafsi, Massimiliano Strappetti, kwa kumtia moyo kufanya safari yake ya mwisho katika kigari kidogo cha “Popemobile Dominika Aprili 20.
“Asante kwa kunirudisha kwenye Uwanja. Kupumzika alasiri, chakula cha jioni na utulivu, kisha alfajiri hisia za ugonjwa, kukosa fahamu na kifo, baada ya siku yake ya kusalimia, na kubariki Ulimwengu baada ya muda mrefu.
Miongoni mwa maneno ya mwisho ya Papa Fransisko ambayo aliyasema ni asante kwa wale ambao walimuhudumia katika wakati huu wa ugonjwa.
Lakini hata muda mrefu uliopita, walimwangalia bila kuchoka, kama vile Massimiliano Strappetti, muuguzi ambaye - kama alivyowahi kusema - aliokoa maisha yake kwa kupendekeza afanyiwe upasuaji wa tumbo, na ambaye Papa alimteua kuwa kama msaidizi wake wa afya tangu mwaka 2022.
Dar es Salaam
Na Pd. Gaston George Mkude
Kristo amefufuka kwelikweli, Aleluia, Aleluia!
Somo la Injili Takatifu ya leo imegawanyika katika sehemu kuu mbili. Kwanza ni Yesu anawavuvia Roho Mtakatifu wafuasi wake, na hivyo kuwapa uwezo dhidi ya uovu na yule mwovu, na ndio kuwaondolea watu dhambi zao. Hivyo Pasaka ni sherehe ya kuonja upendo na huruma ya Mungu, na ndio leo Mama Kanisa anatualika katika Dominika hii ya pili ya Pasaka kutafakari Huruma ya Mungu kwetu. Sehemu ya pili ni ile ya mtume asiyeamini bila kuona na kugusa madonda yake Yesu, ndiye Tomaso aliyejulikana pia kama Pacha.
Kabla ya mateso, kifo na ufufuko wake, Bwana wetu Yesu Kristo anawafundisha wanafunzi wake kuwa Yeye ndio Uzima na Ufufuo. Hivyo baada ya ufufuko wake anapowatokea wanafunzi wake siku ile ya kwanza ya Juma anawadhihirishia waziwazi mitume wake kuwa kweli ni mzima, na kuwasalimu kwa kuwatakia amani nafsini mwao baada ya kujawa na hofu na mahangaiko mengi baada ya kushuhudia mateso na kifo cha Bwana na Mwalimu wao. Ni kweli yeye mzima, amefufuka na mauti hayana tena nguvu dhidi yake! Ufufuko ni ushindi dhidi ya mauti na dhambi, ni ushindi wa upendo na huruma ya Mungu dhidi ya uovu na muovu. Pasaka ni tangazo la upendo na huruma ya Mungu kwa ulimwengu mzima. Pasaka ni Habari Njema kwetu tunaokimbilia huruma na upendo wa Mungu!
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi akiwa na Mapadri na Viongozi wa UKWAKATA wa Jimbo baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Jumatatu ya Pasaka iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Petro-Oyesterbay, Jimboni humo.
Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Agostino Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Peter Assenga, akiwa katika picha ya pamoja na Watawa wa Kike, Viongozi wa Kamati Tendaji na Wakatekumeni baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Kesha la Pasaka, iliyofanyika parokiani hapo. (Picha zote na Yohana Kasosi)
Dekano wa Dekania ya Mtakatifu Thomas More, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Romwald Mukandala ambaye pia ni Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Kizito Kilongawima, jimboni humo akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Kamati Tendaji na wa Vyama vya Kitume baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Pasaka iliyoadhimishwa Parokiani hapo.
Dar es Salaam
Na Remigius Mmavele
Mwanamuziki Jean – Pierre Gina wa Gina ni mtoto wa Corneille EFONGE mwenye asili ya MONGO, kutoka mkoa wa Equateur na wa Élise LISIMO, mwenye asili ya Mongando (familia ya Justin Disasi),
Jean-Pierre EFONGE akiwa mdogo alionyesha ishara za uwezo mkubwa wa muziki. Alizaliwa Mei 13, 1953 katika Jiji la Kinshasa.
Akiwa na chombo chenye nguvu cha kuimba, Efonge alijiunga na Kwaya ya Parokia ya Mtakatifu Paulo, katika mji wa Barumbu mjini Kinshasa akiwa na umri mdogo sana.
ANKARA, Uturuki
Kocha Jose Mourinho ametoa heshima za dhati za kuguswa na kifo cha Baba Mtakatifu Fransisko, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 88.
Mourinho, ambaye kwa sasa anainoa Fenerbahce lakini hapo kabla amewahi kuzinoa Chelsea, Tottenham na Manchester United za Uingereza, alitumia ukurasa wa Instagram kumuenzi Baba Mtakatifu Fransisko.
Mreno huyo aliandika: “Ili kuwa mkuu, zaidi ya yote unahitaji kujua jinsi ya kuwa mdogo. Unyenyekevu ni msingi wa ukuu wa kweli. Papa Fransisko. Matumaini ni mwanga usiku. Grande Papa.”
Baba Mtakatifu ambaye aliugua ugonjwa wa mapafu na sehemu ya pafu moja kuondolewa akiwa kijana, alilazwa katika hospitali ya Gemelli mnamo Februari 14 kwa shida ya kupumua ambayo ilikua ni nimonia.
Alitumia siku 38 huko, muda mrefu zaidi wa kukaa hospitalini kwa upapa wake wa miaka 12.
Vilabu kadhaa vya Ligi Kuu ya Italia, Serie A vilituma salamu za heshima kwa Papa, kufuatia kifo chake ikiwemo timu kongwe ya AS Roma.
“Roma inaungana na kuomboleza kifo cha Papa, msiba ambao unahuzunisha sana jiji letu na ulimwengu mzima,” Roma ilisema katika taarifa.
NEW YORK, Marekani
Mchezaji wa zamani wa NBA na mwanaharakati wa haki za binadamu Enes Kanter Freedom, amesema kuwa Baba Mtakatifu Fransisko ni zaidi ya kiongozi wa kiroho duniani na ishara ya matumaini na amani.
Mchezaji huyo wa Kiislamu alieleza kuwa alianzisha uhusiano wa maana na kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki, jambo ambalo lilimpa msukumo wa kuanzisha kambi ya mpira wa kikapu mjini Vatican, na kuwaleta pamoja watoto wa imani tofauti.
“Michezo huwaleta watu pamoja. Haijalishi historia yako, dini yako, rangi yako, yeyote yule,” Freedom aliiambia NewsNation.
“Tulileta watoto wa Kiislamu, watoto wa Kikristo, watoto wa Kiyahudi, na tulikuwa na wakati mzuri.”
Freedom alikumbuka ushirikiano wake na Papa, ikiwa ni pamoja na wakati ambapo Baba Mtakatifu alipomuomba asimame, ili aone urefu wa mchezaji wa mpira wa vikapu.
“Kila wakati ninapomwona, bila shaka aliweka tabasamu usoni mwangu,” alisema.
Alisema kwamba viongozi kutoka kote duniani wamekuwa wakitoa heshima kwa Papa tangu kifo chake.
Dar es Salaam
Na Arone Mpanduka
Mshindi wa pili wa mbio za Boston Marathon Alphonce Felix Simbu, amesema kuwa kifo cha Baba Mtakatifu Fransisko kimeleta simanzi kubwa ulimwenguni, hasa kwa Wakatoliki.
Akizungumza na Tumaini Letu kwa njia ya simu, Simbu alisema kwamba kifo chake pia kimeleta pigo kubwa kwa wanamichezo kwa kuwa alikuwa mpenda michezo enzi za uhai wake.
“Sijapata nafasi ya kumfuatilia sana kwa upande wa michezo, lakini nimekuwa nikisikia kwamba alikuwa mdau mkubwa wa michezo mbalimbali. Mimi ninamuombea kwa Mungu apate pumziko la milele,”alisema.
Hivi karibuni Simbu aliandika historia mpya katika mbio za kilomita 42 kwa kushika nafasi ya pili, mbio za Boston Marathon zilizofanyika huko Massachusetts, Marekani.
Alimaliza mbio hizo kwa muda wa saa 2:05:04, akitanguliwa kwa sekunde chache na Mkenya John Korir aliyeibuka kidedea kwa muda wa saa 2:04:45, ikiwa ni muda wa pili kwa kasi zaidi katika historia ya mbio hizo.
Katika mbio hizo, Simbu alionesha ushindani wa hali ya juu, akiibuka kinara kutoka kwa kundi kubwa la wanariadha waliotabiriwa kufanya vizuri, akiwemo Cybrian Kotut wa Kenya aliyeshika nafasi ya tatu na Mmarekani Conner Mantz aliyemaliza wa nne.