BAGAMOYO
Na Mathayo Kijazi
Baada ya mchakato wa muda mrefu hatimaye Bagamoyo Lango la Ukristo Tanzania sasa historia yake imekamilika, kutokana na kuundwa kuwa Jimbo jipya Katoliki, huku Baba Mtakatifu Fransisko akimteua Mhashamu Askofu Mteule Stephano Musomba, kuwa Askofu wa kwanza wa jimbo hilo.
Kabla ya uteuzi huo Mhashamu Musomba alikuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, aliyekuwa akisimamia Mawasiliano jimboni humo.
DAR ES SALAAM
Na Mathayo Kijazi
Waamini wameonywa kuepuka kukata tamaa kutokana na majaribu wanayokutana nayo, kwani hayo ni sehemu ya maisha yao.
Kauli hiyo ilitolewa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia – Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Musa Kihoo wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Kwanza ya Kwaresima iliyofanyika parokiani hapo.
MBEYA
Na Angela Kibwana
Mhashamu Godfrey Jackson Mwasekaga, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Mbeya, amesema malengo ya Kwaresima ni kufanya toba, wongofu wa ndani na uaminifu kwa neno la Mungu.
Aidha, amesema kuwa Neno la Mungu ni chakula cha kiroho, na ni taa ya kuwaongoza waamini kwenye njia ya Ukristo wao.
Askofu Mwasekaga alisema hayo wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu, aliyoadhimisha katika Parokia ya Mtakatifu Clara wa Asizi- Shewa Jimbo Kuu Katoliki Mbeya.
Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Yakobo Mkuu Mtume – Kijitonyama, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika iliyoadhimishwa parokiani hapo hivi karibuni.
Mapadri na Viongozi wa Halmashauri ya Walei kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakifurahia jambo wakati wa mkutano wao, uliofanyika katika viwanja vya Kituo cha Msimbazi, jimboni humo hivi karibuni.
Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mlima wa Karmeli – Bunju, Jimbo Katoliki Teule la Bagamoyo, Padri Dominic akiwaombea Wakatekumeni wapya wanaojiandaa kubatizwa katika Mkesha wa Pasaka wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Kwanza ya Kwaresima iliyoadhimishwa parokiani hapo. (Picha zote na Yohana Kasosi)
DAR ES SALAAM
Na Joseph Mihangwa
Ghafla, Afrika imenyamaza kupiga kelele juu ya paa kutangaza sera zake za maendeleo zenye sura ya ubinadamu; sera zilizojaa kurasa za Vyombo vya Habari enzi za uhuru na zama za mageuzi ya uchumi kufuatia uhuru, kwa maandishi makubwa makubwa na kwa wino wa kuangaza:
“Ujamaa” kwa Tanzania; “Zambian Humanism” kwa Zambia; The Common Man’s Charter” – Uganda na “The Guinean Revolution” kwa Guinea ya Rais Ahmed Sekou Toure.
Ujenzi wa Miundo mbinu:
Mwishoni mwa mkutano waliunda Shirika lililoitwa: ‘Inter-Regional Episcopal Board of Eastern Africa (ITEBEA)’. Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Zambia, Fr. Killian Flynn, OFM Cap alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wake wa kwanza na kuanzia mwaka 1964 akawa na ofisi ya kudumu Nairobi, Kenya.
Fr. Killian Flynn ndiye Baba wa Amecea aliyehudumu hadi mwaka 1972. Askofu Mkuu Adam Kozlowiecki, (Baadaye Kadinali) wa Lusaka, Zambia alikuwa Mwenyekiti wake wa kwanza.
Mkutano wa Pili ulikuwa huko Roma: Wakati wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikani (1962 -65) Maaskofu walipata muda wa kufahamiana zaidi na mnamo Novemba 1964 Maaskofu walikutana Roma katika Chuo cha Mt. Anselmo.
SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY
DAR ES SALAAM
Na Paul Mabuga
Hivi karibuni kumekuwa na mjadala kuhusu muziki wa Singeli unaotutambulisha kama Watanzania.
Wapo ambao hawakubaliani na hilo na wengine wanaunga mkono hoja ya utambulisho huu kama ilivyotolewa mara kadhaa na mwanafunzi wa zamani wa Mzumbe Sekondari na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi.
SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY
DAR ES SALAAM
Na Arone Mpanduka
Kiongozi wa zamani wa kikundi cha ushangiliaji cha Timu ya Simba kijulikanacho kama ‘Kidedea’, Said Muchacho amesema kuwa mechi za Simba na Yanga za miaka ya sasa zimepooza, ikilinganishwa na miaka ya zamani.
Akizungumza na Tumaini Letu katika mahojiano maalum, Muchacho alisema kwamba kuanzia kipindi cha miaka ya 2000 kurudi nyuma, hekaheka zilikuwa kubwa sana kuelekea mechi za Simba na Yanga lakini kwa sasa haoni shamrashamra hizo.
SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY
Dar es Salaam
Na Nicolaus Kilowoko
Uongozi wa Klabu ya Soka ya Singida Black Stars kupitia kwa Meneja wa Habari na Mawasiliano, Hussein Massanza umeendelea kukazia kuwa wachezaji wanaocheza ndani ya klabu hiyo hawatoondoka, licha ya kuhusishwa na taarifa za kutaka kutimkia katika timu kubwa za Simba, Yanga na Azam FC.
Massanza alisema kuwa wao wanawashanga wapinzani wao na kuwacheka, kwani kila kukicha wachezaji wao wanahusishwa kwenda kwao lakini bado wanakipiga ndani ya timu ya Singida.
DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Wanandoa wametakiwa kupendana na kuvumiliana katika shida na raha siku zote za maisha yao, kwani katika maisha ya ndoa kuna mengi yanayotokea, hivyo bila kuvumiliana, ndoa hizo haziwezi kudumu.
Wito huo ulitolewa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Shukurani kwa Mungu kwa Jubilei ya Miaka 25 kwa Wanandoa jozi tatu ambao ni Thomas Uiso na Misuka Makani, Damas Mugashe na Rose Emanuel, Deusdedit Rutazaa na Jaove Ijumba, ilifanyika katika Parokia ya Mtakatifu Kizito – Kilongawima, jimboni humo.
“Ndoa ni uvumilivu, siyo mwezako akikukosea kidogo tu, wewe unakuwa na hasira muda huo huo, sio vizuri, lazima muwe watu wa kusameheana, kwa sababu ninyi mmekuwa mwili mmoja, lazima muwe watu wakulindana kwa makosa mnayokwazana,” alisema Askofu Musomba, na kuongeza;
Dodoma
Na Mwandishi wetu
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeshauri Serikali kusimamia vyema Mkandarasi anayejenga uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma ili akamilishe ujenzi huo kwa wakati.
Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso alisema kuwa ni vema mkandarasi akaharakisha ujenzi wa uwanja huo, ili kwenda na mkataba wa ujenzi.
Alifafanua kwamba kumekuwa na tabia kwa baadhi ya Wakandarasi kuomba kuongezewa muda wa ziada wanapopewa kazi, bila kujua muda utakapoongezwa na gharama nazo zinaongezeka.
Hivyo wao kama Kamati, wanashauri Serikali kwanza ni kumsimamia mkandarasi akamilishe ujenzi kwa wakati.
“Kumekuwa na tabia ya Wakandarasi wetu wanapopewa kazi wanaongeza muda wa ziada ambao hautakiwi uingezwa mara kwa mara, Hivyo tunaomba eneo hili Serikali isimamie, kwani anapoongezewa muda, na gharama zinazidi zaidi za ule mkataba uliokuwa umesainiwa,”alisema kiongozi.
DAR ES SALAAM
Na Mathayo Kijazi
Imeelezwa kwamba endapo ikatokea Askari ama Mwanajeshi akafanya mauaji ya mtu ama watu katika vita vya haki, siyo dhambi.
Aidha, mauaji hayo yanapaswa kuwa katika zile jitihada zilizotumika kusuluhisha, lakini imeshindikana, kwani lengo la kufanya hivyo, ni kuimarisha amani katika maisha ya wanadamu.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Padri Paul Sabuni, Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Ambrose – IPTL, Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakati akitoa ufafanuzi wa swali alilodai kuulizwa na baadhi ya Waamini wanaofanya kazi ya Uaskari, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 2025 ya Ukristo kwa Wafanyakazi wa Sekta ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama, iliyoadhimishwa katika Parokia ya Bikira Maria wa Rozari Takatifu – Makongo Juu, jijini Dar es Salaam.