Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu, akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri na vijana waliopokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara katika Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia – Temboni, jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu. Kulia kwa Askofu, ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Festo Ngonyani. (Picha na Mathayo Kijazi)

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi akimbariki mtoto katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Takatifu, Makongo Juu, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa parokiani hapo. Kulia kwa Askofu Mkuu, ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Joseph Massenge, na aliyesimama ni Paroko Msaidizi wa Parokia hiyo, Padri Canisius Hali.

Watoto wa Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu wa Parokia ya Mwenyeheri Antonio Rosmini, Mpiji Magoe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara. Kushoto aliyesimama ni Mlezi wa Shirika hilo, Krista Kimalio.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri  na Viongozi wa Halmashauri ya Walei wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Takatifu, Makongo Juu jimboni humo, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha zote na Yohana Kasosi).

Vijana Waimarishwa wa Parokia ya Mwenyeheri Antonio Rosmini, Mpiji Magohe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo.

Waamini wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Takatifu, Makongo Juu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa parokiani hapo hivi karibuni.

Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Maria De Mathias, Mivumoni, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika.

Wasimamizi wa Zaka wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli, Bunju Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika.

Waamini wa Parokia ya Mwenyeheri Antonio Rosmini, Mpiji Magohe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo.

Wanakwaya wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Takatifu, Makongo Juu Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara iliyofanyika parokiani hapo hivi karibuni. (Picha zote na Yohana Kasosi)