Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

MANCHESTER, Uingereza
Tangu amepoteza mara mbili mfululizo dhidi ya Zhilei Zhang mwaka 2023, Joe Joyce, raia wa Uingereza, hajakaa sawa licha ya kushinda pambano lililofuata dhidi ya Kash Ali, lakini bado alipoteza mbele ya Derek Chisora.
Aprili 05 mwaka huu, Joe Joyce atamkabili Mwingereza mwenzake Dillian Whyte jijini Manchester, lakini kabda ya pambano hilo, Joe ambaye amewahi kuwa bingwa wa World Boxing Organisation (WBO) Interim, atapasha misuli kwa pambano la raundi nane dhidi ya Patrick Korte wa Ujerumani, Machi mosi.

DAR ES SALAAM

Na Nicolaus Kilowoko

Kufuatia kuwa na mwendelezo mzuri tangu alipojiunga na klabu ya soka ya Simba, kocha raia wa Afrika Kusini Fadlu Davis, imeelezwa kuwa ameanza kuufatiliwa na viongozi wa juu wa klabu ya soka ya USM Alger, kutoka nchini Algeria.
Habari ambazo Tumaini Letu imepekua na kuzidaka zinaeleza kuwa matajiri hao kutoka Algeria wanataka kuvunja kibubu kwa ajili ya kuhakikisha kocha huyo wanamtwaa, ili akawasaidie kwenye Ligi yao pamoja na michuano ya Klabu Bingwa Afrika, kitu ambacho kinaonekana kuwachanganya Simba.
Ikumbukwe hata kocha Sead Ramovic aliwaponyoka Yanga hivi karibuni baada ya matajiri wa Belouizdad kuweka pesa nyingi mezani, dau ambalo inaelezwa liliwawia vigumu Yanga kumbakisha.

Mbunge wa Jimbo la Njombe, Deo Mwanyika (wa nne katikati), akipokea Kombe kutoka kwa nahodha wa timu ya Utalingoro, Adalbert Ngole, baada ya timu hiyo kuibuka mshindi katika Mashindano ya Kombe la Ng’ombe kwa kuichapa timu ya Uwemba 1-0 mshindi alipata zawadi ya ng’ombe. Kushoto kwa Mbunge ni Diwani wa Kata ya Utalingoro, Erasto Mpete. (Picha kwa hisani ya Bertold Njawike)

Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), Parokia ya Kristo Mfalme – Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakishangilia moja ya matukio wakati ya Sherehe yao WAWATA Day Kiparokia, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu. (Picha na Yohana Kasosi)

Waandishi wa Habari wakiwa kanisani wakifuatilia Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Wanamawasiliano, iliyoadhimishwa katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Fatima – Msimbazi, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam. (Picha na Mathayo Kijazi)

Paroko Msaidizi wa Parokia ya Kristo Mfalme – Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Bonaventure Kisoka akizindua mashine ya mazoezi iliyonunuliwa na Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) wa Parokia hiyo wakati ya Sherehe ya WAWATA Day kiparokia. (Picha na Yohana Kasosi)

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba (aliyeshika fimbo ya Kichungaji), akiwa katika picha ya pamoja na Wanandoa wa Parokia ya Mtakatifu Paulo Mtume - Kisegese, Rufiji mkoani Pwani, jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sikukuu ya Somo wa Parokia hiyo, iliyoadhimishwa parokiani hapo. Kulia kwa Askofu ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Gaspar Bolongola. (Picha na Yohana Kasosi)

Wanamoyo Mtakatifu wa Yesu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam na Jimbo Katoliki la Moshi, wakisali mbele ya sanduku lililobeba mwili wa Mwanashirika mwenzao, marehemu Theresia Nicholaus Massawe wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya kumwombea, iliyoadhimishwa kijiji cha Maua Kati wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro. (Picha na Yohana Kasosi)

Dar es Salaam

Na Mwandishi wetu

Wanajumuiya wametakiwa kulishika na kuliishi Neno la Mungu kwa ukamilifu bila kuwa na hofu yoyote katika maisha yao ya kila siku.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni na Padri Bonaventure Kisoka, Paroko Msaidizi wa Parokia ya Kristo Mfalme – Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sikukuu ya Somo wa Jumuiya ya Mtakatifu Fabiano, parokiani hapo.
“Waamini muwe watu wa kusali kila mnapokutana, kwa sababu ninyi ni Wakrito, mnapoishi kwa umoja msije mkatengana, endeleeni kusali pamoja kama hivi leo mnaposherehekea Sikukuu yenu mmeungana kitu kimoja, hivi ndivyo inavyotakiwa Wakristo,”alisema Padri Kisoka na kuongeza,
“Tambueni kwamba Jumuiya ni kanisa ndogo la nyumbani, mnakuwa Wakrito wenye umoja. Endeleeni kusali pamoja kama hivi kila wakati, mfuateni Mtakatifu wenu wajumuiya, Mtakatifu wenu alikuwa mtu mwema ambaye alimsikiliza sana Mungu, na ninyi muwe watu wema.”
Aidha, aliwasihi kuungana kwa pamoja ili waweze kuwa na furaha katika Jumuiya yao, Kanda, pamoja na Parokia yao ya Kristo Mfalme, kwa ujumla.
Padri huyo aliwasihi Waamini wenye tabia za kujilimbikizia uongozi, waache kufanya hivyo, akisema kwamba baadhi yao wakipata uongozi, wanajiona ndiyo wameshafanikiwa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ya Mtakatifu Fabiano, Alfred Kunambi alisema kuwa kwa sasa Jumuiya yao ni changa ina miezi michache tangu Paroko wa Parokia hiyo awatangaze, bali wanaishi Ukristo wao kwa furaha.
Kunambi aliongeza kuwa mwaka huu mpya, Jumuiya yao imejipanga vyema, hasa katika mavuno ya Parokia na Jimbo, pamoja na kushiriki katika michango mbalimbali wanayoambiwa na Parokia yao.
Hata hivyo, aliwaomba Viongozi wa Vyama vya Kitume kila Parokia na Parokia Teule, kumuunga mkono Askofu Mkuu wa Jimbo hilo, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi kwa kutoa michango yao ili kukamilisha ujenzi wa Kanisa Kuu Mbadala la Gezaulole.

MOSHI

Na Mwandishi wetu

Watanzania wametakiwa kutoruhusu Vyama vya Siasa viwagawe na kuwafanya watengane kwa itikadi hizo, kwani sifa kubwa ya Taifa hilo, ni kuwa na amani.
Hayo yalisemwa na Paroko Msaidizi wa Parokia ya Bikira Maria Mshindaji, Jimbo Katoliki la Kigoma, Padri George Muhanuka wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya kumuombea marehemu Theresia Nicholaus Massawe, iliyofanyika Parokia ya Bikira Maria Mpalizwa Mbinguni – Kibosho- Singa, Jimbo Katoliki la Moshi.
Aidha, Padri huyo aliwasihi Waamini kuwa wamoja, huku wakiachana na tabia ya ubinafsi katika imani yao.
“Waamini, tujitahidi kuwa wamoja, tuachane na tabia ya ubinafsi katika imani. Lakini pia Vyama vya Siasa CCM, CHADEMA, au chama chochote kile, visitugawe katika umoja wetu tukiwa Watazania wenye amani,” alisema Padri Muhanuka.
Padri Muhanuka aliongeza kwa kusema, “Ndugu zangu Waamini tujiandae, hatujui muda wala saa tutakapoitwa na Mungu, maana tunakuwa Waamini wa Jumapili tu, wala hatupo kama Waamini wa kuwa na Mungu karibu.”
Padri huyo alisema pia kuwa Theresia Massawe enzi ya uhai wake, aliuishi Ukristo wake kwa imani moja ya Kanisa Katoliki, ambaye pia alikuwa mwanashirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu, na alijiunga pia na Shirika la Mtakatifu Anna.
“Je, wewe Mwamini umejiunga na chama gani cha Shirika la Kanisa? Jitathmini Ukristo wako unaoishi kwa sasa, Mungu ametuleta hapa duniani ili tumtambue na tumtumikie, ili siku ikifika, tuwe mahali pa wokovu. Huyu mama aliishi kiukamilifu bila shaka lolote,” alisema Padri huyo.
Alibainisha pia kuwa Waamini wengi hawauishi Ukristo wao kikamilifu, kwa sababu ya kutangatanga katika Makanisa mbalimbali kutafuta miujiza.