Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Tenisi ni mchezo unaofurahiwa na washiriki wa rika zote na viwango vyote. Mchezo huo umekuwa ukivutia watazamaji na wachezaji tangu mwanzoni mwa karne ya 12.
Hapa kuna ukweli na maendeleo ya kupendeza ambayo yametokea tangu historia ya mapema ya tenisi.
RAKETI:
Raketi ni kifaa cha kuchezea mchezo wa tenisi, ambacho kazi yake ni kupigia mpira huo.
Kabla ya wachezaji wa tenisi kutumia raketi, watu walianza kutumia kiganja cha mikono yao kupiga mpira na kuurudisha juu ya wavu.
Watu katika karne ya 12 waliteseka kutokana na kuvimba mikono  katika mchezo wa jamii ya tenisi ulioitwa ”jeu de paume” unaomaanisha “mchezo wa mitende.”
Hali hiyo haikuchukua muda mrefu, kwani ilikwenda hadi karne ya 16 ambapo ‘racquets’ zilitumiwa ingawa kabla ya raketi walitumia matawi ya mnazi yaliyosukwa kupigia mpira.
RANGI ZA MIPIRA:
Kabla ya mipira ya tenisi yenye rangi ya njano kuletwa mchezoni, kulikuwa na mipira myeupe.
Mipira myeupe ilitumika tangu mchezo huo unatambulishwa duniani, hadi pale iipoanzishwa michuano ya Wimbledon mnamo mwaka 1986, wakati mipira ya tenisi ya njano ilipotumiwa.
Maafisa waliamini kuwa mpira wa njano ungekuwa rahisi kwa watazamaji kutazama kwenye TV, na hiyo ndiyo ikawa sababu ya kutumia mipira ya rangi hiyo.
MAILI TATU:
Wakati wa mechi ya tenisi, mchezaji kwa wastani hukimbia maili 3.
Kwa sababu ya udogo wa uwanja wa tenisi, hiyo ni maili 3 ngumu zaidi ya mchezaji kwenda mbele na kurudi nyuma mara zote.
MKANGANYIKO WA RAKETI:
Raketi ya tahajia ndiyo njia ya kawaida ya kutamka kifaa kinachotumika katika michezo ya wavu, kama vile tenisi.
Kwa Kiingereza, kuna maneno mawili yanatofautiana kwenye kuandika, lakini yanafanana kimatamshi. Racket na racquet hutofautiana kwenye matumizi, ambapo Racket ni kifaa ambacho hutumika kwa kuchezea tenisi, na Racquet hutumika kuchezea michezo mingine, kama vile skwashi.
Ingawa tovuti nyingi zitakuambia kuwa raketi ni tahajia sahihi, USTA mara kwa mara hutumia raketi ya tahajia.
DADA WA FAMILIA MOJA:
Venus na Serena Williams walikuwa seti ya kwanza ya kina dada kushinda medali za dhahabu za Olimpiki katika historia ya tenisi.
Akina dada hao walishinda medali yao ya kwanza ya dhahabu ya Olimpiki katika Michezo ya Olimpiki ya Sydney mwaka 2000.
Sasa wana medali mbili za ziada za dhahabu kutoka Beijing 2008 na London 2012.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Mtibwa Sugar ya Morogoro imesema kwa ubora inayouonyesha kwenye Ligi ya Chamionship kwa sasa, ni kama vile walitoka Ligi Kuu mara moja na kwenda kutalii, ili kuona hali ya hewa ya huko.
Mtibwa imekuwa ikionyesha kiwango bora tangu msimu wa Championship uanze, Ligi ambayo zamani ilifahamika kama Daraja la Kwanza, ambayo huzipokea timu zinazoshuka daraja kutoka Ligi Kuu.
Mtibwa ambayo ipo kileleni mwa Ligi hiyo, endapo itaendelea kukaza uzi, itafanikiwa kurejea tena Ligi Kuu, ambapo msimu uliopita ilishuka daraja baada ya kuwa na matokeo mabovu.
Afisa Habari wa ‘Wakata miwa’ hao. Thobias Kifaru alisema kwamba ushiriki wao wa Championship ni kama wanafanya utalii, ili kujua mandhari yake, na kisha kurudi Ligi Kuu kuwasimulia wengine maisha ya huko.
“Huku ni kama tumekuja kutalii na kujionea maisha ya Chamionship yalivyo, halafu tutarejea zetu Ligi Kuu tukiwa tuna taarifa zote za kinachoendelea huko kwa sababu kwa sasa hatukamatiki na tunajihisi hatuna mpinzani wa kutusumbua,”alisema Kifaru.
Alisema kwamba imani yao ni kuona wanarejea kwenye Ligi Kuu msimu ujao na kujiwekea mipango ya kuhakikisha hawashuki tena daraja kwa sababu chanzo wameshakijua, na wamejifunza.
Hivi karibuni Mtibwa ilicheza mechi ya kirafiki na Azam FC na kuiadabisha kwa kuichapa bao 1-0 kwenye mchezo uiopigwa Manungu Complex mjini Morogoro.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Siku chache baada ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara kupaa hadi nafasi ya nne kwa ubora barani Afrika, timu shiriki za Ligi hiyo zimeshauriwa kuongeza ushindani ili kuondoa mazoea ya timu zile zile kupokezana ubingwa.
Hayo yamesemwa na beki wa zamani wa Taifa Stars Bakari Malima wakati akitoa mtazamo wake kuhusiana na ubora wa Ligi hiyo ikilinganishwa na ilivyokuwa katika miaka ya zamani.
Alisema kuwa bado kumekuwa na kasumba ya Ligi hiyo kuwa na ushindani wa timu tatu ama nne zinazowania ubingwa kila msimu, huku timu zingine zikiwa zinashiriki kuwania kutoshuka daraja.
“Ligi Kuu ni bora, lakini kila msimu kumekuwa na ushindani wa timu tatu ama nne pekee, ambazo zinawania ubingwa.Sasa kwenye hilo, kunahitaji uboreshaji hasa kwa timu zenyewe kuongeza ushindani ili kuleta uimara,”alisema Malima.
Alisema pia kuwa ifike wakati bingwa wa Ligi Kuu asitabirike kirahisi, kwa maana ya kwamba ikitokea Yanga ameyumba, basi Simba anapewa nafasi, au ikitokea Simba kayumba kwenye msimu, Yanga anapewa nafasi ya ubingwa katika wakati ambao hata msimu haujafika katikati.
Malima alisema kwamba hata mechi zinazohusisha Simba, Yanga na Azam FC dhidi ya timu zingine, bado imekuwa ni rahisi sana kutabiri nani atashinda, tofauti na ilivyo katika Ligi zingine.
Alitolea mfano Ligi Kuu ya Uingereza, ambayo kila msimu imekuwa ni ngumu kumtabiri bingwa pamoja na mechi moja moja zinazochezwa ambazo mshindi amekuwa haeleweki, na hivyo kuwapa shida watu wanaobashiri mechi hizo.
Katika hatua nyingine, Malima alisema kuwa uongozi bora na ubora wa miundombinu, ndiyo silaha kubwa ya kupanda viwango kwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Alisema kwamba katika miaka ya zamani ambayo yeye alicheza soka, Chama cha Soka nchini FAT (Football Association of Tanzania) kwa wakati ule, kilitawaliwa na migogoro ya mara kwa mara, huku viwanja vingi vya kuchezea vikiwa chakavu.
“Ninakumbuka zamani uwanja mzuri ambao wachezaji tulikuwa tunapenda kuuchezea ni wa CCM Kirumba uliopo jijini Mwanza lakini zaidi ya huo, hakukuwepo na uwanja mwingine mzuri. Hata wa Uhuru haukuwa sawa kwenye eneo la kuchezea,”alisema Malima.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akisalimiana na Calistre Camilius Lekule wa Parokia ya Bikira Maria wa Rozari Takatifu  - Makongo Juu, wakati wa kumshika mkono Askofu kwenye Adhimisho la Misa Takatifu ya Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana, iliyoadhimishwa parokiani hapo sanjari na uzinduzi wa Shule mpya ya Awali na Msingi ya Mary of The Rosary Pre & Primary School-Makongo.

Dar es Salaam

Na Pd. Richard Mjigwa- C.PP.S

Mwenyeheri Giovanni Merlini ni Mtume mwenye ari na mwamko wa Fumbo la Pasaka ya Kristo linaloleta wokovu, shuhuda, amini wa Injili na mshauri mwenye busara.
Hayo yamo katika Waraka wake wa Kitume wa Baba Mtakatifu Fransisko wa kumtangaza Mwenyeheri huyo, ambaye Sikukuu yake itaadhimishwa kila mwaka Januari 12.
Mwenyeheri Giovanni (pichani) yeye alikuwa ni mhubiri mahiri; Mshauri mwenye busara na mjumbe wa matumaini na amani katika Kristo Yesu.
Katika maadhimisho ya Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana, Kristo Yesu, Nafsi ya Pili ya Fumbo la Utatu Mtakatifu anajifunua, kwa watu wake waliokuwa wamepokea Ubatizo wa toba na maondoleo ya dhambi.
Hii ni siku ya Ufunuo wa Fumbo la Utatu Mtakatifu, yaani Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu. “Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu ninayependezwa naye” (Mt, 3:13-17, Mk, 1:9-11, Lk, 3:21-22). Ni tukio linalotakatifuza maji yote ya Ubatizo, na umuhimu wa maisha ya sala. Rej Lk, 3:21 na katika kusali, Kristo Yesu anawafundisha Wafuasi wake kusali. Rej KKK 2607.
Huu ni mwaliko kwa Waamini kutafakri ufunuo wa Sura na Sauti ya Mungu. Ubatizo wa Bwana unahitimisha maadhimisho ya Kipindi cha Noeli, Mwanzo wa: maisha na Utume wa Kristo na ni siku maalum ya Ubatizo kwa watoto wachanga, changamoto na mwaliko kwa wazazi na walezi kuwarithisha watoto wao zawadi ya imani.
Ni katika muktadha wa maadhimisho ya Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana, Kardinali Marcello Semeraro, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Kuwatangaza Waamini kuwa Wenyeheri na Watakatifu kwa niaba ya Baba Mtakatifu Fransisko, Dominika Januari 12, 2025 amemtangaza Mtumishi wa Mungu Giovanni Merlini, kuwa ni Mwenyeheri na ambaye alizaliwa tarehe 28 Agosti, 1795 huko Spoleto, Perugia nchini Italia.
Akapewa daraja Takatifu la Upadri Desemba 19, 1818. Agosti 15, 1820 akajiunga na Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu, lililokuwa limeanzishwa na Mtakatifu Gaspari del Bufalo Agosti 15, 1815. Alijiunga na Shirika baada ya kuvutiwa sana na mahubiri yaliyotolewa na Mtakatifu Gaspari, kuhusu Fumbo la Ukombozi chemchemi ya upendo wa kimisionari.
Kumbe, Tasaufi ya Damu Azizi ya Yesu ni msaada kwa kila Mkristo kwa kuwa Damu ya Kristo ndiyo msingi wa ukombozi wa mwanadamu, na ni kielelezo cha juu kabisa cha upendo wa Mungu kwa watu wote.
Tasaufi hii ina msingi wake katika, na Neno la Mungu na katika Fumbo la Ekaristi Takatifu, ambalo ndilo chanzo na kilele cha maisha ya kila siku ya Kanisa, na maisha ya Mkristo kwa jumla.
Tena Ekaristi Takatifu ni ujumuisho mzima wa Imani ya Kikristo, na ni msingi wa mitazamo sahihi ya Kikristo. Rej KKK 1324 na 1327. Tasaufi ya Damu Azizi ya Yesu, Agano Jipya na la Milele, ikawa ni msingi wa maisha na sadaka, kwa bidii ya kutafakari na shauku ya kitume “cum ardore contemplativo et passione apostolica.”
Mwenyeheri Giovanni Merlini aliishi nyakati za Mapinduzi ya Napoleone, wakati wa mchakato wa mafundisho tanzu ya Kanisa. Papa Pio IX Desemba 8, 1854 akatangaza rasmi kwamba, Mwenyeheri kabisa Bikira Maria, tangu nukta ya kutungwa kwake mimba, kwa neema na upendeleo wa pekee wa Mwenyezi Mungu, kwa kutazamia mastahili ya Kristo Yesu, Mwokozi wa wanadamu wote, alikingiwa na kila doa la dhambi ya asili.
Mwenyeheri Giovanni Merlini akatangaza na kushuhudia tunu msingi za Kiinjili katika maisha ya kila siku kwa kutambua mbegu za Ufalme wa Mungu, na hivyo akajipambanua kuwa ni chombo cha huruma ya Mungu na amani; na shuhuda wa matumaini yasiyotahalisha. “Spes non confundit.”
Kati ya Mwaka 1847 hadi 1873 aliteuliwa kuwa ni Mkuu wa tatu wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu. Kama kiongozi, akaonesha utakatifu wa maisha, udugu, ari na mwamko wa kimisionari; ukaribu na majadiliano katika ukweli na uwazi; kupima mang’amuzi ya maisha na utume wa Kimisionari mbele ya Msalaba. Ni katika wakati wa uongozi wake, Shirika likapanuka na kuenea nje ya mipaka ya Italia hadi Kaskazini mwa Ulaya na nchini Marekani.
Katika maisha na utume wake alibahatika kuwa ni kiongozi wa maisha ya kiroho kwa Mtakatifu Maria De Mattias, utume alioutekeleza kwa kipindi cha miaka arobaini na miwili.
Akasaidia kujenga na kuwaimarisha Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu, ASC. Katika mashauri yake alikazia: majadiliano katika utu, heshima na ukuaji wa maisha ya kiroho, daima wakitafuta mapenzi ya Mungu.
Mwenyeheri Giovanni Merlini, alisaidiana na Mtakatifu Gaspari del Bufalo kupyaisha maisha ya Waamini na Makleri kwa namna ya pekee kama yaliyoasisiwa na Papa Pio VII (1800-1823: wa 251) na Pio 1X kwa njia ya mahubiri, mafungo, na hata wakati mwingine akahatarisha maisha yake kwa kutangaza Injili miongoni mwa majangili, kielelezo cha mtume wa msamaha unaobubujika kutoka katika Damu Azizi ya Kristo.
Fumbo la Pasaka ni kiini cha maisha na utume wa Kanisa na kwamba Waraka wa Kitume wa “Amantissimus human” wa Mwaka 1862 ulionesha umuhimu wa Tasaufi ya Damu Azizi ya Kristo, na kunako mwaka 1849 katika Waraka wa Kitume wa “Redempti sumus,” Sikukuu ya Damu Azizi ya Yesu, ikatangazwa kuwa ni Sikukuu kwa Kanisa zima. Mwenyeheri Giovanni Merlini akaitupa mkono dunia tarehe 12 Januari 1873 kwa ajali.
Tarehe 10 Mei 1973, Baraza la Kipapa la Kuwatangaza Waamini kuwa Wenyeheri na Watakatifu, likamtangaza kuwa ni Mtumishi wa Mungu. Tarehe 23 Mei 2024 Baba Mtakatifu Fransisko akaruhusu atangazwe kuwa ni Mwenyeheri. Katika Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana, Dominika tarehe 12 Januari 2025 akatangazwa kuwa ni Mwenyeheri.
Jumamosi tarehe 11 Januari 2025, kukafanyika Ibada ya mkesha wa nguvu ukiongozwa na AskofuVincenzo Viva wa Jimbo Katoliki Albano, nchini Italia. Misa ya shukrani imeadhimishwa Jumatatu, tarehe 13 Januari 2025 kwa kuongozwa na Askofu Mkuu Renato Boccardo wa Jimbo Kuu la Spoleto, Italia.
Baba Mtakatifu katika Waraka wake wa Kitume wa kumtangaza Mtumishi wa Mungu Giovanni Merlini kuwa ni Mwenyeheri, anasema, kwa hakika alikuwa ni Mtume mwenye ari na mwamko wa Fumbo la Pasaka ya Kristo linaloleta wokovu, shuhuda amini wa Injili na mshauri mwenye busara.
Sikukuu yake itakuwa inaadhimishwa kila mwaka tarehe 12 Januari. Baba Mtakatifu Fransisko wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana alisema, Giovanni Merlini, Padri Mmisionari wa Shirika la Damu Azizi, alijisadaka bila ya kujibakiza kwa ajili ya utume kwa watu wa Mungu, akawa mshauri mwenye busara kwa roho nyingi, na mjumbe wa amani.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba - OSA (mwenye fimbo ya kichungaji), akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri na Viongozi wa Kamati Tendaji wa Parokia ya Mtakatifu Pio wa Pietrelcina - Ulongoni ‘B’, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sherehe ya Miaka 10 ya Parokia hiyo. Kushoto kwa Askofu ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Leonard Amadori - OFMCap (Picha na Mathayo Kijazi)

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri, Viongozi wa Kamati Tendaji na Kamati ya Ujenzi wa Shule mpya ya Awali na Msingi ya Mary of The Rosary Pre & Primary School ya Parokia ya Bikira Maria wa Rozari Takatifu - Makongo Juu.

Shule mpya ya Awali na Msingi ya Mary of The Rosary Pre & Primary School ya Parokia ya Bikira Maria wa Rozari Takatifu - Makongo Juu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam kama inavyoonekana pichani baada ya kubarikiwa na kuzinduliwa na Askofu Mkuu wa Jimbo hilo, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi.

Mwanza

Na Paul Mabuga

Kuna makundi kadhaa ya vizazi kutokana na mazingira na matukio katika nyakati mbali mbali.
Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia, na hasa mapinduzi ya kidijitali, yamechangia zaidi kuongezeka kwa tofauti kati ya makundi ya vizazi, hali ambayo imeathiri mahusiano, mitindo ya maisha, na makuzi.
Uhusiano wa kizazi kimoja kwenda kingine, limekuwa ni jambo lenye changamoto kulimudu. Katika muktadha huo, mwandishi wetu Paul Mabuga  anaangalia uhusiano kati ya wanandoa kutoka zama za ‘baby boomer’ na ‘milenia’.
Harufu ya sangara anayekaangwa, imetanda katika nyumba moja iliyopo katika mtaa wa Nyamanoro jijini Mwanza. Kwa hakika inavutia, kwani hata kwa mwenye hisia ndogo ya kunusa, anaweza kuitambua, na kwa mwenye njaa aliye jirani, ni lazima aombe msaada.
Baba mwenye nyumba tunayemwita Adam Fungamwango, yupo sebuleni akisoma gazeti. Unamtazama, unapokewa na sura yenye mikunjo inayokutangazia kuwa Bwana huyu umri wake kwa makadirio ni miaka 64. Na wewe ni mgeni pekee sebuleni.
“Karibu, lakini kabla ya yote fanya ufanyavyo kwenye mahojiano, lakini jina langu sitaki lijulikane! Vinginevyo hakuna mahojiano hapa,” anasema bwana huyu akikukaribisha na kuendelea na mazunguzo baada ya kuhakikishiwa kuwa litatumika jina bandia ili kuficha utambulisho wake, “Mie nilikuwa dereva, na nimeendesha maafisa wengi wakubwa, na sasa ni miaka minne tangu nimestaafu.”
Anasema, mkewe ambaye naye, tunamtambulisha, kwa jina la bandia la Diana Fungamwango, bado ni mfanyakazi kama katibu muhtasis katika moja ya mashirika ya umma jijini Mwanza, na ana umri wa miaka 44 kwa sasa. Walioana miaka 23 iliyopita, na kwamba  Diana anatumia muda mwingi kazini isopokuwa siku za mwisho wa juma.
Diana ambaye ndiye anayekaanga samaki, hana makuu, katopea katika simu yake ya mkononi akitaradika na yaliyomo. Pengine anaanza leo wasanii gani wamechambana kwenye mitandao,  anashuka na wale wasemaji wa timu za mpira na washabiki wao, na baadaye anatambaa na darasa la sifa za mume bora, na kumalizia na hadithi. Yeye ameshika mbili na wala hazimponyoki, huku ana simu, na kule  anakaanga.
Hii ni ndoa kati ya mume  ambaye katika zama za vizazi, yupo kwenye kundi la ‘Baby Boomer,’ ambao wamezaliwa kati ya miaka ya 1946 na1964  na mke ambaye yupo kwenye lile linalojulikana kama ‘milenia’, ambao walizaliwa kati ya  1981 na1996. Makundi haya ya vizazi na mengine,  kila moja  lina sifa zake,
Kwa maana hiyo  watu katika kundi la ‘baby boomer’ wana umri kati ya miaka 61 na 79 kwa mwaka huu wa 2025. Kwa idadi kulingana na taasisi mbali mbali [Shirika la Takwimu la Taifa linalosimamia Sensa ya Watu na Makazi, (National Bereau of Statistics: NBS), na Benki ya Dunia, idadi yao hapa nchini ni kama milioni tatu, ama asilimia tano, ya Watanzania .  
Wale walioko kwenye kundi la milenia, wana umri kati ya miaka 29 na 44, na idadi yao kulingana na taasisi hizo,  inakadiriwa kuwa kama nilioni 12 ama asilimia 20 ya Watanzania kwa kadirio. Ni sawa na kusema ni  kundi lenye watu wengi, na ambalo kwa idadi, ni mara nne ya lile la ‘baby’ boomer. Licha ya changamoto kadhaa, lakini kuna ndoa baina ya makundi haya kama ilivyo katika makala haya.
“Ni kweli kuna tofauti za kimtazamo katika baadhi ya mambo kati yangu na mke wangu, mathalan, mimi najali sana mambo ya maendeleo kitaifa, nikiona mtu anaonewa siwezi kupita bila kuhakikisha haki inapatikana;
Ninajali majaliwa ya taifa letu siku za usoni, na nipo tayari kujitolea kwa ajili ya jamii yangu,” anasema Fungamwango wakati alipotakiwa kufafanua baadhi ya mambo   anayopendelea katika fikra zake,
Sifa hizi anazozieleza  Mfungamwango, zinaelezwa na watafiti kuwa zinatokana na ukweli kwamba, ‘baby boomers’ walizaliwa katika kipindi cha harakati za kuleta mabadiliko katika jamii, na kupambania haki za binadamu, na hii ndiyo sababu ya wao kuwa hivi,
Kwa upande mwingine, tafiti zinaonesha kizazi cha  milenia, kimetekwa na  teknolojia, hasa kwa sababu wamekulia katika mazingira ya kuibuka na kushamiri kwa matumizi ya  ‘internet’. Wana mapokeo yenye uwanda mkubwa ikilinganishwa na baby boomer na hivyo kuwafanya wao kuwa huru. Wanapenda kuwa wajasirimali na wanafanya kazi kwa uwiano na uhuru. Wanajali sana mitindo ya mavazi na vifaa vingine

MIAMI, Marekani
Kocha wa klabu ya soka ya Inter Miami Javier Mascherano amejibu maoni ya Neymar kuhusu uwezekano wa kuungana tena na Lionel Messi na Luis Suarez katika klabu ya Inter Miami.
Akizungumza na vyombo vya habari, Mascherano alisema kuwa hawawezi kumzungumzia Neymar kwa sababu hawana lolote, japokuwa ni wazi kwamba Neymar ni mchezaji mkubwa.
Mascherano alisema kwamba kila kocha duniani anamtaka, lakini kwa sasa, Ligi yao inatawaliwa kuhusu kikomo cha mshahara kwa wachezaji, hivyo kwao kwa wakati huu, haiwezekani kujaribu kufikiria juu yake.
Neymar amekuwa akihusishwa na uwezekano wa kuondoka Al-Hilal msimu wa joto, huku timu hiyo ya Saudi Pro League ikiripotiwa kutokuwa na uwezekano wa kuongeza mkataba wake kwa mwaka mwingine.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, amesalia kimya kuhusu mustakabali wake, huku akitarajia kupata tena utimamu kamili na kujenga mdundo ufaao kabla ya kutamba na Brazil kwenye Kombe la Dunia la 2026.
Neymar amekuwa akihusishwa na kutaka kujiunga na klabu ya Ligi Kuu ya Soka ya Inter Miami ili kuungana na wachezaji wenzake wa zamani wa Barcelona Messi, Suarez, Jordi Alba na Sergio Busquets, na kuchochea tetesi za uhamisho wiki ya jana.