Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Papa aguswa kimbunga kuipiga Libya

Baadhi ya maeneo yaliyoathirika na kimbunga nchini Libya. Baadhi ya maeneo yaliyoathirika na kimbunga nchini Libya.

TRIPOL, Libya

Katika telegramu kwa Balozi wa Vatican huko Rabat nchini Libya, Baba Mtakatifu Fransisko anaonesha uchungu, na kuwaombea marehemu zaidi ya 2,300 waliofariki dunia kutokana na mafuriko yaliyokumba eneo la mashariki mwa nchi na kueleza ukaribu kwa walionusurika na waokoaji.
Askofu Overend, Msimamizi wa Kitume wa Benghazi, alisema kuwa kuna hitaji kubwa la msaada wa kiutu kwa waathirika wa tukio hilo.
Kwa mujibu wa waraka wa Baba Mtakatifu, faraja, nguvu na ustahimilivu, ndiyo maombi yake kwa ajili ya watu wa Mungu walioathiriwa na uharibifu uliosababishwa na mafuriko mashariki mwa Libya.
Waraka huo wa Baba Mtakatuifu umewasilishwa kwa njia ya telegramu iliyotiwa saini na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican akielekezwa kwa Balozi wa Vatican, Askofu Mkuu Savio Hon Tai-Fai.
Baba Mtaklatifu alisema kuwa ameguswa ka kiasi kikubwa kuhusu hasara kubwa ya maisha na uharibifu uliosababishwa na mafuriko katika eneo la mashariki mwa Libya, na anawahakikishia maombi yake kwa ajili ya roho za marehemu na wale wote wanaoomboleza kupoteza wapendwa wao.
Baba Mtakatifu pia anaonesha ukaribu wa kina wa kiroho kwa waliojeruhiwa, kwa wale wanaoogopa wapendwa wao waliopotea na wafanyakazi wa dharura wanaotoa msaada na usaidizi. Kwa wale wote walioguswa na janga hilo, Baba Mtakatifu Fransisko kwa utashi wake mwema, anawaombea baraka za Mungu za faraja, nguvu na uvumilivu,” unasomeka Ujumbe huo uliotiwa saini na Katibu wa Vatican.
Idadi ya watu waliopotea kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na kimbunga Daniel kilichosababisha vifo vya watu 2,300 katika eneo la mashariki mwa nchi, kulingana na idadi kubwa ya watu waliopotea ni 10,000.
Mkuu wa ujumbe wa Msalaba Mwekundu katika Mkutano wa Umoja wa Mataifa uliofanyika mjini Geneva, Uswisi, aliyeunganishwa kupitia video na Tunisia alisema kuwa dhoruba kali baada ya kuzuru Ugiriki, Uturuki na Bulgaria, ilisababisha kuporomoka kwa wakati mmoja kwa mabwawa mawili ambayo yalitoa lita milioni 33 za maji. Kwa hiyo hali ni mbaya kama ile ya Morocco, ambayo inashughulikia matokeo ya tetemeko la ardhi.
Kwa upande wake Askofu Sandro Overend Rigillo, Msimamizi wa Kitume huko Benghazi, aliyefikiwa kwa njia ya simu na Vatican News, alisema kwamba mahali walipo kulikuwa kumetulia hata kama kulikuwa na dhoruba kali na mabomu ya maji, hapakuwapo na matatizo.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.