Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Mpira wa Kikapu na mambo usiyoyajua

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Mpira wa kikapu ni aina ya michezo inayopendwa katika sehemu nyingi za dunia, na watu wengi hutamani mchezo huu.
Kila timu huwa na wachezaji watano uwanjani, na hadi wachezaji wa kando 7 walio tayari kuchukua nafasi ya mchezaji mwingine muda wowote.
Mchezo huu ulianzishwa na mwalimu James Naismith kwenye Chuo cha Springfield College huko Massachusetts mwaka 1891. Alibuni mchezo huo kwa ajili ya wanafunzi wake ili wapate mazoezi wakati wa kipupwe waliposhindwa kucheza nje.
Mpira wa kikapu ulienea haraka kwenye vyuo vya Marekani, na katika karne ya 20, pia nje ya vyuo.Mwaka 1936 mchezo huu ulikubaliwa kwenye michezo ya Olimpiki.
Mpira unaotumiwa kimataifa ni mpira wa ngozi wenye kipenyo cha milimita 749 hadi 780, na uzito wa gramu 567 hadi 650.
Vipimo vya uwanja wa mpira wa kikapu huwa ni wa mita 28 urefu kwa mita 15 upana.
Wakati wa mchezo, kuna marefa wawili hadi watatu uwanjani. Kando ya uwanja hukaa waamuzi wengine wanaohusika na muda, kuhesabu pointi na makosa ya uwanjani.
Mchezo huu huchezwa kwa dakika 48  zenye vipindi vinne, ambapo kila kimoja huwa ni cha dakika 12.
TURN OVER
Katika mpira wa kikapu, ‘turn over’ hutokea wakati timu inapoteza umiliki wa mpira kwa timu pinzani, kabla ya mchezaji kushuti golini. Hili linaweza kutokea kutokana na mchezaji kuibiwa mpira, na mchezo kuwa chini ya umiliki wa timu pinzani, ama kutoka nje ya mstari wa uwanja, ama kufanya faulo, na mpira kulazimika kwenda kwa timu nyingine.
Turn overs zipo za aina kuu mbili, ambapo ya kwanza ni ya kulazimisha, na ya pili si ya kulazimisha.Turn over ya  kulazimisha ni ile ambayo mchezaji anaingia kwa nguvu na kuiba, ama kumpokonya mpira mpinzani, na kuufanya uwe kwenye umiliki wake.Na turn over isiyo ya kulazimisha ni ile inayotokea wakati timu inayoshambulia kufanya makosa yenyewe, ikiwemo kucheza rafu, ama kutoa mpira nje kwa bahati mbaya, au makosa mengine madogomadogo yatakayolazimu mpinzani auchukue mpira.
BLOCKS
Hii inatokea wakati mchezaji wa eneo la ulinzi la timu anapomzuia mshambuliaji kushuti mpira kwenye goli lake.Tukio hili huhusishwa pia katika takwimu za mchezo huo.
REBOUND
Hili ni tukio ambalo hutokea wakati mpira uliorushwa kuelekea kwenye goli, kugonga ubao wa goli, na kisha kurudi uwanjani ama kupitiliza upande wa pili wa chuma cha goli ikiwa ulirushwa na mfungaji kutokea pembeni mwa uwanja.Wakati mwingine, rebound huwa faida kwa mfungaji ambaye huwahi kuudaka mpira ulioshindikana kuingia wavuni, na kisha kufunga, ama beki anayezuia kuuwahi ule mpira usirudi tena kwa mpinzani, na kisha kuanzisha mashabulizi.
STEAL
Hii hutokea wakati mchezaji anapoiba mpira kutoka kwa mpinzani.Mara nyingi haitumiki nguvu kubwa zaidi ya akili ya mlinzi kuona namna ipi bora ya kuuchukua mpira kwa haraka kutoka mikononi mwa mpinzani.
FREE THROW
Hutokea hasa kwenye faulo ambapo timu inayofanyiwa faulo hupewa fursa ya kuwa na mrusho huru, ambapo mchezaji mmoja husimama akiwa anatazamana na goli, na kisha anahurusha mpira kuelekea golini. Na mpira unapoingia golini, faida yake ni pointi moja.
POINTI
Kwa kawaida, matokeo ya kwenye mchezo wa mpira wa kikapu hutokana na kuhesabiwa pointi, na si kuhesabu mara ngapi mpira umeingia golini.
Kila goli katika kikapu linahesabiwa kama pointi 2 au 3, kutegemeana na umbali wa kurusha.Kama ni karibu na goli, zinatolewa pointi mbili, na kama ni mbali na goli, zinatolewa tatu.Goli la penati (adhabu), huzaa pointi moja tu.
ASSIST
Hii ni pasi ya mwisho anayotoa mchezaji mmoja kwenda kwa mfungaji, nayo ni sawa tu na ilivyo kwenye mchezo wa soka.
FAULO
Hii hutokea wakati mchezaji anapomchezea vibaya mpinzani, na adhabu yake ni ‘free throw’ ambayo imeelezwa hapo juu.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.