Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Wachezaji DR Congo watuma ujumbe wa amani

Cedrick Bakambu. Cedrick Bakambu.

ABIJAN, Ivory Coast
Wachezaji wa kikosi cha timu ya soka ya taifa ya DR Congo wametumia fursa ya kutoa ujumbe wa amani kupitia fainali za Mataifa ya Afrika, AFCON, kufuatia machafuko yanayoendelea katika eneo la Mashariki mwa nchi yao.
Makumi ya makundi yenye silaha ikiwa ni pamoja na waasi maarufu wa M23 kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliana na tajiri wa madini mashariki mwa taifa hilo la Afrika ya Kati, wakipigania udhibiti wa ardhi huko.
Mzozo kati ya makundi hayo ambayo ni pamoja na wanamgambo wanaoiunga mkono Serikali, ulipamba moto baada ya makubaliano ya amani ya miezi sita kumalizika mwezi Oktoba, huku takriban raia 60 wakiripotiwa kuuawa wakati wa mashambulizi huko Kivu Kaskazini mwezi huo huo pekee.
Mapigano yanaendelea ndani ya kilomita 25 (maili 15) kutoka Goma, mji mkuu wa mkoa huo, katika eneo ambalo Serikali ya Kinshasa imeshindwa kupata mtego wa usalama kwa miongo mitatu iliyopita.
Kulingana na Umoja wa Mataifa, mzozo huo uliokithiri, umesukuma watu milioni 6.9 kuyakimbia makazi yao, huku shirika hilo likisema kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inakabiliwa na majanga makubwa zaidi ya kibinadamu duniani.
“Kila mtu anaona mauaji mashariki mwa Congo, lakini kila mtu yuko kimya,” mshambuliaji wa DR Congo, Cedric Bakambu aliandika kwenye mtandao wa kijamii.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.