Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Siasa zaiondosha timu ya Dynamo

Amadou Gallo Fall Amadou Gallo Fall

BUJUMBURA, Burundi
Ushiriki wa klabu ya Dynamo ya Burundi katika Ligi ya Mpira wa Kikapu Afrika, umefikia ukomo baada ya kukataa kuvaa jezi yenye nembo ya ‘Visit Rwanda’.
Timu hiyo ilifunika ujumbe huo katika mchezo wao wa ufunguzi katika Kongamano la Kalahari mjini Pretoria, lakini wakapoteza mechi zao mbili zilizofuata.
Hayo yanakuja huku kukiwa na mvutano wa kisiasa kati ya nchi hizo mbili.
Burundi ilifunga mipaka yake na Rwanda mwezi Januari baada ya kumtuhumu jirani yake kufadhili mashambulizi ya waasi.
Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye alidai serikali ya Rwanda inayoongozwa na Paul Kagame inaunga mkono kundi la waasi la Red Tabara baada ya shambulio la wanamgambo hao kuwaua watu 20 mwezi Disemba.
Rais Kagame anakanusha shtaka hilo, lakini serikali ya Burundi imemtaja kuwa “jirani mbaya”.
Rais wa Ligi ya Mpira wa Kikapu Afrika (BAL) Amadou Gallo Fall alisema kuwa ligi hiyo haikuwa na budi, ila kuifukuza klabu hiyo kwa kukataa kufuata kanuni za ligi hiyo zinazosimamia mahitaji ya jezi na sare.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.