Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Azam, Simba, Yanga zawindana

Kiungo wa Azam FC, James Akaminko Kiungo wa Azam FC, James Akaminko

Dar es Salaam

Na Mwandishi wetu

Imeelezwa kuwa timu za soka za Simba, Yanga na Azam FC zipo kwenye hekaheka za kuchomoleana wachezaji wenyewe kwa wenyewe ili kuzipa uimara timu zao kuelekea msimu ujao.
Tumaini Letu limebaini kwamba Azam FC baada ya kumchukua ‘kimafia’ Feisal Salum, wana mpango wa kumchukua beki wa Yanga Joyce Lomalisa pamoja na Djuma Shaban ambao hawaonyeshi nia ya kuendelea kubaki Jangwani.
Mbali na kutaka kuibomoa Yanga, Azam FC imeelezwa kutaka kufanya ‘vurugu’ kwa Simba kwa kuweka pesa ndefu kwa kiungo tegemeo Clatous Chama ili akaimarishe kikosi chao.
Chama amekuwa na msaada mkubwa kwa Simba, hasa kutokana na uwezo wake wa kutengeneza nafasi za kufunga katika mazingira magumu ya mchezo.
Yanga nao kwa kuonyesha kwamba si wanyonge, wanaendelea kumfukuzia kiungo James Akaminko ambaye miezi michache iliyopita, walithibitisha kupeleka barua ya maombi ya kufanya nae mazungumzo, ingawa mabosi wa Azam walikataa.
Kwa upande wao Simba SC, duru zinaeleza kwamba wanamfukuzia mchezaji wa Azam FC Sospeter Bajana ambaye msimu uliomalizika alionyesha uwezo mkubwa.
Sambamba na hilo, wekundu hao wanataka saini ya kiungo mkabaji wa Yanga, Mkongomani Yanick Bangala, ambaye naye taarifa za sasa zinadai hana nia ya kuendelea kubaki Jangwani.
Hata hivyo Afisa Habari wa Azam FC Hashim Ibwe na Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba Ahmed Ally, kwa nyakati tofauti wamenukuliwa wakisema kwamba hawana mpango wowote na wachezaji wanaohusishwa nao, huku wakiwataka mashabiki wao kusubiri mambo mazuri yajayo kuhusiana na usajili watakaofanya.
Ahmed Ally alisema kwamba wamechoka kuonewa na kufanywa wanyonge, hivyo msimu ujao watahakikisha wanarejesha heshima yao dimbani kwa kusajili wachezaji hatari wa kimataifa.
Kwa upande wake Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe alisema kwamba mipango ya kuwanasa wachezaji wakubwa wa Kimataifa inaendelea, na kwamba hata ikitokea hao wanaotajwa kuondoka wakafanikiwa kuondoka, bado kikosi chao hakitotetereka, kwa sababu Yanga ina viongozi makini na wenye weledi.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.