Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Michezo ya Kimataifa yaineemesha Azam

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Uwanja wa soka wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam, unatazamiwa kuiingizia Klabu ya Azam FC zaidi ya shilingi milioni 42.7 kupitia mechi za Kimataifa katika kipindi cha wiki mbili zilizobaki za mwezi huu.
Kwa kipindi kirefu, uwanja wa Azam Complex umekuwa msaada kwa timu mbalimbali za Kitaifa na Kimataifa ambazo hazina viwanja vya nyumbani kuutumia kucheza mechi zake ndani na Kimataifa.
Kwa sasa timu za Simba, Yanga na Singida Fountain Gate zinautumia uwanja huo katika mechi zake za nyumbani za michuano ya Kimataifa, ambapo Singida inashiriki Kombe la Shirikisho Afrika, huku Simba na Yanga zikiwa zinashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.
Kwa mujibu wa Idara ya Habari ya Azam FC, timu ya Tanzania inayotaka kuutumia uwanja huo kwa ajili ya mechi moja, inatakiwa kulipia kiasi cha shilingi 5,900,000, huku timu ya kigeni ikitakiwa kulipa dola 5,000 ambazo ni sawa na zaidi ya shilingi 12,527,945.
Katika kipindi cha kuanzia Septemba 15 hadi 30 mwaka huu, timu za Simba, Yanga, Singida Fountain Gate, Bumamuru (Burundi) na Artar Solar (Djibout) zitautumia uwanja huo kwa mechi zake za nyumbani kwenye michuano ya Kimataifa ngazi ya klabu.
Septemba 17 mwaka huu Singida Fountain Gate itaikaribisha Future FC ya nchini Misri katika mchezo wa Shirikisho Afrika, na mwisho wa mwezi huu Simba itaikaribisha Power Dynamo ya Zambia, na Yanga itaikaribisha Al Merreikh ya Sudan katika mechi za marudio za Ligi ya Mabingwa Afrika.
Kwa mechi hizo tatu, Azam FC itanufaika kwa kuvuna shilingi milioni 17.7 huku pia ikikusanya kiasi kingine cha dola 10,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 25 kutoka kwenye mechi mbili za Kimataifa kutoka kwa timu za nje ya nchi za Artar Solar na Bumamuru, ambazo zinatumia uwanja huo kama wa nyumbani.
Bumamuru ya Burundi imeialika Mamelodi ya Afrika Kusini, na Artar Solar ya Djibout imeialika Zamalek ya Misri, zote zikitumia uwanja huo.
Jumla ya gharama ya mechi zote hizo ni zaidi ya shilingi milioni 42.7, kiasi ambacho ni tofauti na kile ambacho kitatokana na mazoezi ambayo timu za Singida Fountain Gate, Artar Solar na Bumamuru zinaendelea kufanya zikitumia uwanja huo.
Gharama ya mazoezi kwa timu ya ndani ni shilingi 600,000 kwa muda wa mchana, na usiku ni shilingi 1,500,000, huku timu za nje zikitakiwa kulipa dola 1,000.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.