Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Berry afungiwa kwa kutumia madawa

Washington, USA
Mrusha nyundo Gwendolyn Berry amepigwa marufuku kwa miezi 16 na Wakala wa Kupambana na Dawa za Kulevya nchini Marekani, kwa kukutwa na dawa iliyopigwa marufuku.
Kusimamishwa huko kunamaanisha kwamba Mmarekani huyo mwenye umri wa miaka 34, atakosa Mashindano ya Riadha ya Dunia mwezi huu huko Budapest.
Ukiukaji wa Berry ulitokana na matumizi yake ya dawa ya juu, krimu inayotumika kutibu maumivu katika sehemu mahususi ya mwili iliyokuwa na ‘spironolactone.’
Ni marufuku ya pili ya kutumia dawa za kusisimua misuli ndani ya kipindi cha miaka 10 kwa Berry, ambaye alikuwa mwanachama wa timu za Olimpiki za 2016 na 2020 za Marekani.
Kupigwa marufuku kwake kunamaanisha kuwa atakosa pia Michezo ya Olimpiki ya Paris ya mwaka 2024, itakayoanza Julai ijayo.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.