Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Farah awaacha watu midomo wazi

LONDON, Uingereza
Mo Farah, mmoja wa wanariadha wakubwa wa Uingereza wa wakati wote, alimaliza wa nne katika mbio za mwisho za taaluma yake katika Great North Run.
Bingwa huyo wa Olimpiki mara nne mwenye umri wa miaka 40, aliteleza mapema katika mbio maarufu za maili 13.1 kutoka Newcastle hadi South Shields.
Alimaliza dakika tatu na sekunde 30 nyuma ya Muethiopia Tamirat Tola, ambaye alishinda kwa dakika 59, sekunde 58.
Alisema kuwa kukimbia ndiyo kila kitu kwake na ndiko kulikomuokoa na amewashukuru washabiki wake wote waliomuunga mkono katika nyakati zote za maisha yake kwenye kazi yake hiyo.
“Inatia moyo sana, kulikuwa na mengi yaliyokuwa yakipita akilini mwangu, ila ninachojua ni kukimbia, na hilo ndilo lililonifurahisha kwa miaka mingi,” alisema Farah.
Farah anastaafu akiwa na wasifu unaometa, kwani alikuwa Mwingereza wa kwanza kukamilisha Olimpiki ya mita 5,000 na 10,000 mara mbili kwa ushindi mbele ya umati wa watu wenye furaha huko London mwaka 2012, na kutetea mataji yake huko Rio mwaka 2016.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.