Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Stars kuongezwa nguvu

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars)

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (Tanzania Football Federation:TFF), Wallace Karia amesema kuwa wapo kwenye mchakato wa kuongeza idadi ya makocha katika timu ya Taifa Stars ili iweze kufanya vizuri.
Taifa Stars kwa sasa inasubiri upangaji wa timu(team draw) ya kujua kundi gani litakalokuwa la wapinzani watakaokutana nao katika fainali za Afrika zitakazofanyika kuanzia Januari 13 hadi Februari 11 mwakani 2024, nchini Ivory Coast.
Akizungumza na Kituo cha Redio cha UFM jijini Dar es salaam kwenye mahojiano maalum, Karia alisema kwamba wamepanga kufanya maandalizi makubwa ili Tanzania ifike mbali katika fainali hizo.
Alisema pia kuwa timu hiyo ina makocha wasaidizi wakiongozwa na Adel Amrouche, lakini kuna ulazima wa kuwa na benchi pana la ufundi, kama zilivyo timu za mataifa mengine.
“Tunaamini na Serikali itatusaidia katika eneo hili muhimu.Tunataka tupate wataalamu wa kutosha.Unakuta wenzetu benchi lao la ufundi lina wataalamu 15, na kila mmoja anafanya majukumu yake.Kwa kuwa tunakwenda kushindana na watu wa ngazi ya juu, tunataka walau tuwe na makocha saba,”alisema Karia.
Alisema pia kwamba wanataka hadi kufikia kwenye mechi za kalenda ya Federation of International Football Assocation(FIFA) za mwezi Oktoba, timu iwe na benchi pana la ufundi, na kwamba tayari hao makocha wapo, na kilichosalia ni kuwasainisha tu mikataba.
Alisema pia kwamba kuna makocha wengine walishaanza kuonekana kwenye benchi hilo, ingawa wamekuwa kama wanajitolea. Hivyo mipango ikikamilika na wao kusainishwa mikataba, watakuwa tayari kutangazwa makocha wapya.
Akizungumzia maandalizi ya jumla kuelekea fainali hizo, Karia alisema kuwa wameshaongea na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ambayo imewataka kuwasilisha mpango mkakati wa maandalizi, ili waangalie sehemu ipi Wizara inaweza kuwaunga mkono.
“Mwezi Oktoba kuna mechi za Kalenda ya FIFA ambazo tutazitumia kuiandaa timu yetu, na mwezi Novemba kuna nafasi pia ya mechi za timu za taifa, nako pia tutaangalia uwezekano wa kuiandaa timu yetu kuelekea michuano hiyo ya Januari,”alisema Rais huyo wa TFF.
Katika fainali zake mbili za Afrika zilizopita za miaka ya 1980 na 2019, Stars iliishia hatua ya makundi, na kutolewa pasipo kuingia 16 bora.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.