Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Magonjwa yasiyoambukiza - mwiba kwa Watanzania

DAR ES SALAAM

Na Alex Kachelewa

Magonjwa yasiyoambukiza (MYA), ni maradhi ambayo hayaambukizi na wala hayawezi kusambazwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine au mnyama, ndege, kwani mara nyingi huwa ni ya muda mrefu.
Mfano wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni kisukari, shinikizo la juu la damu, saratani, mfumo wa upumuaji, ajali, afya ya akili, na selimundu.
Taarifa ya hali ya MYA duniani zilionesha kuwa watu milioni 42 (sawa na asilimia 71 ya vifo vyote), walifariki dunia katika matimba mbalimbali duniani kote kutokana na magonjwa haya.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, Nchini Tanzania 33% ya vifo vyote vinachangiwa na magonjwa hayo ambayo huchangia kwa 75% ya vifo vyote vinavyohusu watu wenye umri wa miaka 30-70.
Viashiria vya Magonjwa Yasiyoambukiza:
Viashiria hatarishi vya magonjwa yasiyoambukiza vimegawanyika katika sehemu tatu; viashiria vya awali; utandawazi, ukuaji wa miji, ongezeko la watu wenye umri mkubwa.
Viashiria vinavyowezekana kubadilika; Ulaji-matunda na mbogamboga- 2.7%, matumizi ya pombe- 29.4%, Tumbaku-15.9%, tabia bwete na uzito uliozidi- na Kiribatumbo- 26%.
Mwaka 2021 jumla ya wagonjwa 3,440,708 wenye magonjwa yasiyoambukiza walitibiwa (OPD) ikilinganishwa na wagonjwa 3,852,973 waliotibiwa mwaka 2022 (ongezeko likiwa ni 412,265, sawa na 12%). Magonjwa ambayo yanaongoza ni pamoja na shinikizo la juu la damu, ugonjwa wa kisukari.
Taarifa ya vifo inaonesha kuwa katika kila vifo vitatu vinavyotokea nchini, kifo kimoja kinatokana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Na katika magonjwa 10 yanayoongoza kusababisha vifo nchini, kuna magonjwa manne yasiyoambukiza (Magonjwa ya Moyo (4.5%) yanashika nafasi ya Pili; Shinikizo la Damu (3.8%) nafasi ya tatu; pamoja na ugonjwa wa Kisukari (2.5%), nafasi ya 9.
Hali ya magonjwa ya saratani kila mwaka inaonyesha kuwa wagonjwa wapya 40,464 wa saratani wanagundulika, ambapo sehemu kubwa ya wagonjwa hao huwa na saratani zifuatazo:-
Saratani ya Mlango wa Kizazi (25.3%); Saratani ya Matiti (9.9%); saratani ya tezi dume (8.8%). Kila mwaka saratani husababisha vifo vya watu 26,945, wengi wao wakiwa ni kina mama wenye tatizo la saratani ya mlango wa kizazi.
Hali ya magonjwa ya selimundu nchini Tanzania ni miongoni mwa nchi tano zinazoongoza kwa ugonjwa wa selimundu duniani, ambapo mtoto mmoja katika kila watoto 100 huzaliwa na ugonjwa huu, na asilimia 15 ya Watanzania, wanaishi na vinasaba vya selimundu.
Hata hivyo, watoto 70 - 90 hufariki dunia kutokana na ugonjwa huu kabla ya kufikia umri wa miaka mitano, wengi hushindwa kupata elimu kutokana na kuumwa mara kwa mara.
Tanzania imeanza huduma za kupima watoto wachanga ili kubaini mapema kama wana ugonjwa. Huduma ya upandikizaji uloto imeanza Hospitali ya Benjamin Mkapa kama tiba pekee ya tatizo hili kwa sasa.
Hali ya Magonjwa ya Akili:
Jumla ya wagonjwa 260,894 walipatiwa huduma za afya ya akili katika mwaka 2022, wagonjwa wengi ni wale wenye kifafa, sonona, na wanaotumia dawa za kulevya.
Tanzania pia ni miongoni mwa nchi ambazo kuna hali ya juu ya kujiua, ambapo kwa ujumla katika kila watu 100,000, watu wanane wamepata tatizo hilo (MNH data 2020).
Kwa vijana kati ya, miaka 13 – 17, tafiti zinaonesha kwamba katika kila vijana 100, kuna vijana 12 ambao wanapata hisia za kutaka kujiua, na kati yao 10 kwa kila 100, wameshajaribu kufanya hivyo.
Athari zitokanazo na Magonjwa Yasiyoambukiza:
Ongezeko la vifo vinavyoweza kuepukika katika ongezeko la watu wanaoishi na ulemavu au changamoto zinazoweza kuzuilika:
Kisukari huchangia asilimia 27 ya upofu unaotokana na mtoto wa jicho. Takribani asilimia 10 ya wagonjwa wa kisukari hupata matatizo ya miguu, ikiwemo kukatwa miguu kwa zaidi ya asilimia 10 ambao huanza kupata matatizo ya figo.
Shinikizo la juu la damu na kisukari, huchangia matatizo ya kiharusi (stroke), pamoja na tatizo la figo kwa zaidi ya asilimia 25 ya wagonjwa wote.
Magonjwa hayo yana athari za kiuchumi na kijamii, madhara kwenye rasilimali watu na hasara kwa Pato la Taifa  kupungua uzalishaji kwa wafanyakazi kushindwa kuhudhuria. Kushindwa kuwa na ufanisi gharama za kuajiri watumishi wapya, kupungua kwa rasilimali watu wenye ujuzi, Serikali kutumia fedha nyingi kwenye matibabu. Sekta Binafsi zinawekeza pia katika huduma za Afya (NCDs accounts for 20% of NHIF Budget).
Madhara kwa mtu na familia ni ongezeko la matumizi ya Serikali na Sekta Binafsi, husababisha kifo kupoteza kipato cha familia kuwa na ufukara kutokana na gharama za matibabu kupanda, pamoja na kupoteza muda kutokana na kuwahudumia wagonjwa, na pia familia kuachwa na yatima.
Mikakati mitano ya Serikali katika kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza ni kuimarisha huduma za Afya ya Akili, huduma za saratani pamoja na Bankable Document. Mkakati wa huduma za macho na mkakati wa (sickle cell) selimundu imeandaliwa kuongoza utekelezaji, na mwongozo wa mazoezi.
Kuongeza upatikanaji wa huduma za uchunguzi wa awali (newborn Screening), upatikanaji wa dawa ya Hydroxyurea na upandikizaji uloto kwa wagonjwa wa selimundu – ambapo tayari Bunge liliidhinisha kaisi cha Shilingi bilioni tano kwa huduma hizo.
Upanuzi wa huduma za saratani kwa ajili ya kutoa huduma za mionzi kwenye Hospitali zote za Kanda na Ujenzi wa Kituo cha Umahiri Mloganzila na Dodoma pamoja na kuimarisha huduma katika Mkoa wa Mbeya, Hospitali ya KCMC, Moshi, Mkoani Kilimanjaro, na Bugando mkoani Mwanza, ambazo tayari ujenzi wake umeanza.
Kuimarisha upatikanaji wa huduma za Elimu kwa Umma, uchunguzi na matibabu kuanzia ngazi ya Msingi, Wizara imewezesha Mafunzo kwa watendaji 2890 kwenye vituo 702 vya afya nchi nzima, vifaa vya kuwekeza katika utafiti, na tathmini ili kubaini viashiria vya magonjwa yasiyoambuza, utafiti kwenye hali na madhara ya kiuchumi yatokanayo na Tumbaku, hali ya ufanyaji mazoezi, na hali ya Lishe nchini.
Kuanzishwa kwa mpango wa Taifa (TaNCDP) – 2019, ni kwa sababu ya uhitaji wa Serikali na Wadau kuwekeza zaidi kwa kuhutubia Taifa ili Kuzindua Mpango wa Taifa.
Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya NCD kwa Kuzindua Miongozo na Initiatives mbalimbali (National Lifeystyle Reform Campaign).
Hatua ya Serikali kuandaa Mkakati wa III wa Magonjwa Yasiyoambukiza umetokana na HSSP – v na One Plan III kuwekeza katika maeneo yanayoainishwa, na mkakati wa ugharamiaji wa huduma za Afya kwa Wote (UHC).
Uwekezaji kwenye Afya ya msingi kwa kubuni njia za upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya magonjwa yasiyoambukiza, kuimarisha matumizi ya takwimu na tafiti, na kadhalika.
Aidha, mikakati harakishi ni kuimarisha uratibu kwa kuhusisha sekta 12 muhimu katika kusimamia afua kinga na udhibiti wa magonjwa yasiyoambuikiza.
Kubainisha na kuandaa kampeni maalum kwa makundi yaliyo kwenye uhatarishi mkubwa Wafanyakazi mahali pa kazi ili kuhakikisha walau 75% ya watu wote wanafikiwa na elimu hiyo, na 50% ya wenye umri wa miaka 40 na kuendelea, wanapimwa afya zao.
Pia kuhakikisha 50% ya shule zinafikiwa na elimu ya magonjwa yasiyoambukiza, 75% ya wanafunzi kwenye shule hizo wanafikiwa, pamoja na watu wenye umri mkubwa (zaidi ya miaka 60) wanafikiwa.
Kufanya tafiti za hali ya magonjwa yasiyoambukiza- STEPS 2023; Utafiti kwenye hali na madhara ya kiuchumi yatokanayo na Tumbaku; Hali ya Ufanyaji wa Mazoezi, pamoja na Hali ya Lishe nchini, ni Kampeni za Uhamasishaji katika Jamii.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.