Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Ifahamu mipira ya kuchaji kama simu

Mchezaji wa timu ya Taifa ya Uingereza, Kieran Trippier. Mchezaji wa timu ya Taifa ya Uingereza, Kieran Trippier.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Katika miaka ya zamani, mipira ya kuchezea soka ilikuwa inajazwa upepo tu, na kisha timu kuchezea, lakini sasa hali imekuwa tofauti.
Sasa hivi ipo mipira ya kiteknolojia ambayo kabla ya kutumika uwanjani, lazima uifanyie vitu viwili ambavyo ni kujaza upepo na kuchaji.
Teknolojia hiyo ilianza mwaka jana mwishoni katika fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika nchini Qatar.
Mipira hiyo ndani yake imewekewa ‘chip’ maalumu, ambazo zinahitaji kuwa na nishati ya umeme ili kufanya kazi kwa usahihi.
Mipira hiyo ya kuchaji ilitengenezwa na kampuni ya Adidas, ina sensa ndani yake, ambayo inakusanya takwimu mbalimbali, kasi na uelekeo wa mpira, na kutuma ujumbe kwenye mashine za VAR kutambua kama kuna mchezaji ameotea (offside) au la.
Mfano kwenye fainali za mwaka jana, mipira ilikuwa ikichajiwa kama simu za mkononi, ambazo zilichomekwa kwenye umeme kabla ya mechi za Kombe la Dunia kuanza huko Qatar, na baada ya hapo waamuzi husika walikuwa wakikagua kila kitu na kuruhusu itumike. Hii ni tofauti na zamani ambapo kazi ya mwamuzi ilikuwa kukagua kiwango cha upepo tu.
Sensa iliyopo ndani ya mpira huo, inapewa nguvu na betri ndogo, ambayo uwezo wake wa kukaa na chaji wakati ukitumika ni saa sita na chaji itadumu kwa siku 18 kama hautakuwa unatumika.
Uzito wa sensa hiyo ni gramu 14 ambayo kazi yake ni kufanya uwelekeo wa mpira, huku ikiwa imeunganishwa na kamera mbalimbali zilizopo uwanjani ili kuwasaidia waamuzi juu ya mchezaji kuotea, na mambo mengine.
Mpira utakapopigwa kwa mguu, kichwa, kurushwa hata ukiguswa tu, meseji 500 zinakuwa zimetumwa ndani ya sekunde moja.
Data zinatumwa kwa wakati na haraka, kupitia antena za mtandao zilizowekwa kuzunguka uwanja wa mchezo, na hivyo kuhifadhiwa kwenye kompyuta kwa ajili ya matumizi inapohitajika.
Kama mpira utatoka nje ya eneo na kuingizwa mpira mwingine uwanjani, mfumo unakamata haraka na data zinanaswa zenyewe bila ya kuhitaji usaidizi wa kibinadamu.
Adidas imetengeneza mpira mwepesi na wenye kasi kubwa, kitu ambacho kilimfanya beki wa England, Kieran Trippier kufichua kuwa umekuwa ukimpa shida kwenye kupiga mipira ya adhabu ndogo.
Alisema kwamba kila alipojaribu kupiga mpira wakati wa adhabu ndogo, aligundua kuna utofauti, lakini hata hivyo hicho hakiwezi kuwa kisingizio katika jambo lolote.
Alisema kuwa mipira ipo tofauti, siyo suala la joto wala kitu kingine, na kwamba ikitumika nguvu kubwa kupiga mipira hiyo, ni rahisi kupaa.
Kwa miaka kadhaa, kampuni hiyo ya Adidas imekuwa ikitengeneza mipira mbalimbali yenye teknolojia ya kushangaza watu katika michuano mikubwa.
Kuna wakati walishawahi kutengeneza mipira yenye ‘sensor’ ndani yake, ambayo ilikuwa maalum kwa ajili ya kugundua kama mpira umevuka mstari wa goli.Na hii ilikuwa inaambatana na saa maalum anayovaa mwamuzi, ambayo ilikuwa inatetemeka kama ishara kwamba mpira umevuka mstari wa goli.
Kama saa ya mwamuzi haitetemi, ni dhahiri kwamba mpira haujavuka mstari, na mwamuzi hawezi kukubali goli.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.