Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Wolff aendelea kusalia Mercedes hadi 2026

Mkuu wa timu ya Mercedes, Toto Wolff. Mkuu wa timu ya Mercedes, Toto Wolff.

VIENNA, Austria
Mkuu wa timu ya Mercedes, Toto Wolff, ambaye pia anamiliki theluthi moja ya mabingwa wa zamani wa mbio za magari atasalia katika jukumu lake hadi angalau mwaka wa kwanza wa mabadiliko ya sheria kuu ya F1.
Toto Wolff, ambaye ni raia wa Austria, ametia saini mkataba mpya wa kusalia kama Mkuu wa Timu na Mtendaji Mkuu wa Mercedes F1, na kumwezesha kumaliza hadi mwisho wa msimu wa 2026.
Wolff, ambaye anamiliki sehemu sawa ya theluthi moja ya timu ya F1 na INEOS na Mercedes-Benz, alisema kuwa watatu hao waliamua wafanye hivyo tena, huku wakipanga njia ya kurejea kilele cha mchezo huo.
Wolff ameshikilia jukumu kuu la timu pamoja na umiliki wa hisa katika Mercedes tangu ajiunge nayo kutoka Williams mwaka wa 2013, na kuwaongoza kwenye rekodi ya Mashindano nane ya Wajenzi tangu mwaka 2014 hadi 2021, kabla ya wapinzani wao Red Bull kumaliza ubabe wao.
Kulikuwa na uvumi juu ya mustakabali wa Wolff katika nafasi ya bosi wa timu ya kila siku huko Mercedes, lakini mzee huyo wa miaka 52 anahisi bado ndiye mtu bora zaidi kwa nafasi hiyo, maoni yaliyoshirikiwa na Sir Jim Ratcliffe, Mtendaji Mkuu wa INEOS, na Mwenyekiti wa Mercedes-Benz Ola Kallenius.
“Nadhani jambo muhimu zaidi kati yetu sisi watatu, ni kwamba tunaaminiana,” alisema Wolff.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.