Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Maaskofu SECAM wapiga msumari ndoa za jinsia moja

Maaskofu Katoliki wanaunda Baraza la SECAM wakiwa katika maandamano kwa ajili ya Adhimisho la Misa Takatifu. Maaskofu Katoliki wanaunda Baraza la SECAM wakiwa katika maandamano kwa ajili ya Adhimisho la Misa Takatifu.

NAIROBI, Kenya

Baraza la Maaskofu wa Afrika na Madagaska (Symposium of Episcopal Conferences of Africa and Madagascar: SECAM) barani Afrika, wametangaza msimamo wao na kudumisha msimamo huo kwamba kama Bara, baraka za ziada za kiliturjia zilizopendekezwa katika Azimio la Baba Mtakatifu Fransisko kuhusu watu wa jinsia moja kubarikiwa haikubaliki na haiwezi kufanyiwa kazi Barani Afrika.
“Sisi, Maaskofu wa Kiafrika, hatuoni kuwa inafaa kwa Afrika kubariki ndoa za watu wa jinsia moja au wapenzi wa jinsia moja, kwa sababu katika mazingira yetu, hii inaweza kusababisha machafuko, na itakuwa kinyume cha moja kwa moja na maadili ya kitamaduni ya jamii za Kiafrika,”ilisomeka sehemu ya taarifa kutoka kwa Uongozi wa Kongamano la Baraza la Maaskofu wa Afrika na Madagaska (SECAM), iliyotolewa Januari 11, mwaka huu 2024.
Tamko hilo kutoka kwa Kanisa zima la Afrika kwa mujibu wa taarifa hiyo, limepokea makubaliano ya Baba Mtakatifu Fransisko na Mwadhama Kardinali Victor Manuel Fernåndez, Mkuu wa Dicastery kwa Mafundisho ya Imani.” Wakati huo huo Mapadre wanathibitisha tena kushikamana kwao bila kuyumbayumba kwa Mrithi wa Petro, ushirika wao pamoja naye na uaminifu wao kwa Injili, lakini hawatatekeleza jambo hilo, kwani ni kinyume na misingi ya Kaisa na Mungu Mwenyezi.
Muhtasari wa pamoja wa misimamo iliyopitishwa na Mabaraza mbalimbali ya Maaskofu wa Kitaifa na baina ya nchi katika Bara la Afrika, unakuja kufuatia ombi la SECAM kwa Marais wote wa Mabaraza ya Maaskofu wa Kitaifa Barani Afrika, kuchangia maoni yao kuhusu waraka wa Vatican ambao “umesababisha mshtuko mkubwa, uliopandwa dhana potofu, na misukosuko katika akili za wengi Walei waaminifu, watu waliowekwa wakfu, na hata wachungaji na imeibua hisia kali” tangu kuchapishwa kwake.
Kwa mujibu wa Maaskofu Barani Afrika katika ujumbe wao uliotiwa saini na Rais wa SECAM, Mwadhama Fridolin Kardinali Ambongo Besungu, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), uamuzi wao wa kutowabariki wapenzi wa jinsia moja, unatokana na wasiwasi kuhusu uwezekano wa kuchanganyikiwa na kashfa ndani ya nchi jumuiya nzima ya Kanisa Katoliki.
“Mafundisho ya mara kwa mara ya Kanisa yanaelezea vitendo vya ushoga kuwa “vilivyovurugika kwa ndani” (Congregation for the Doctrine of the Faith, Declaration Persona Human, No. 8) na kinyume cha sheria ya asili,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo ya Alhamisi inapoendelea katika rejea ya kile ambacho Kanisa Katoliki linafundisha.
“Vitendo hivi vinavyozingatiwa kuwa ni kufunga tendo la ndoa kwa zawadi ya maisha, na si kutoka kwa upendo wa kweli na ukamilishano wa kijinsia, havipaswi kuidhinishwa kwa hali yoyote” (Katekisimu ya Kanisa Katoliki, n.k. Na. 2357).

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.