Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Yanga: Guede atatikisa nyavu

JOSEPH GUEDE JOSEPH GUEDE

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Klabu ya Yanga imesema kwamba bado ina imani kubwa na mshambuliaji wake mpya Joseph Guede aliyejiunga nao kwenye kipindi cha dirisha dogo la usajili.
Guede mwenye uraia wa Ivory Coast, alikuwa akiimbwa na wanaYanga wengi mara baada ya kusajiliwa kwamba anaweza kuvaa viatu vya Fiston Mayele ambaye kwa sasa anaitumikia klabu ya Pyramids ya nchini Misri.
Akizungumza hivi karibuni, Afisa Habari wa Klabu hiyo Ali Kamwe alisema kuwa kwa jinsi alivyomtazama mshambuliaji huyo, ni imani yake kwamba atakuja kufunga mabao mengi.
Alisema kwamba mshambuliaji huyo ana sifa zote za washambuliaji mahiri, isipokuwa amekosa utulivu, hasa kutokana na kutozoea vyema mazingira ya timu na Ligi aliyoikuta.
“Mimi niwaambie mashabiki wa Yanga na wengine wote kuwa walioanza kumbeza. Guede atakuja kufunga mabao mengi, na wengi watashangazwa na hilo. Ameanza kuzoeana na wenzake kwa haraka na mwalimu kumuingiza kwenye mfumo moja kwa moja. Anakosa bahati tu ya kufunga magoli. Lakini kuna siku atawashangaza,” alisema Kamwe.
Alisema pia kuwa tatizo lililopo kwa mashabiki ni kutaka kuona mchezaji anacheza mechi moja na kufunga hapo hapo, kitu ambacho humpa shinikizo mchezaji na kujikuta akiwa na presha kubwa uwanjani.
Guede alizaliwa Agosti 23 mwaka 1994 huko Abidjan, Cote d’ Ivoire ambapo mwaka 2017 alikuwa akiitumikia klabu ya USC Bassam, na kisha kutimkia klabu ya AFAD Djekanou.
Baadae akajiunga na FAR Rabat kwa kitita cha dola 40,000 na kuhitimisha msimu wa 2019/2020 akiwa mfungaji bora wa klabu yake na mabao 10 kwenye Ligi, huku klabu yake ikimaliza nafasi ya sita katika Ligi.
Guede alisaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia Rabat ambapo alienda nayo hadi katikati ya mwaka 2023.
Kitu kinachowatia hofu mashabiki wa Yanga ni kitendo cha kukaa muda mrefu bila kuwa na timu, huku akikosa rekodi nzuri ya upachikaji wa mabao kwa timu alizopitia.
Mbali na Guede, Yanga kwa sasa inawategemea zaidi washambuliaji wengine kama Kennedy Musonda na Clement Mzize.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.