Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Ligi ya Kikapu Dar kuanza Machi

DAR ES SALAAM

Na Nicolaus Kilowoko

Katika kuhakikisha michezo wa kikapu unaendelea kukua nchini Tanzania, uongozi wa michezo huo kupitia mkoa wa Dar es Salaam, umekuja na mpango mkakati wa kufanya maboresho makubwa kwenye ligi yao.
Ligi hiyo ya kikapu mkoa wa Dar es Salaam (BDL) inatazamiwa kuanza rasmi Machi pili mwaka huu, huku pia kukiwa na baadhi ya maboresho kwenye ligi hiyo.
Kamishna wa mchezo wa kikapu Halleluja Kavalambi alisema kuwa kwa msimu huu, wamekusudia kuongeza msisimko kwenye ligi hiyo, hivyo wanatarajia kupata timu zenye ushindani zaidi.
Kuhusu usajili, Halleluya alisema kwamba dirisha la usajili kwa wachezaji wa ndani na nje limeshafunguliwa, na linatarajiwa kufungwa tena Februari 25 mwaka huu.
Alisema kuwa Ligi hiyo ambayo mwezi Machi inatarajiwa kuanza kuchezwa, itajumuisha timu 16 kwa upande wa Wanaume na 16 kwa Wanawake, na itakuwa na utofauti na ilivyokuwa katik miaka mingine.
Kuhusu ubora wa timu alisema kuwa bado timu zinaendelea na michezo mbalimbali ya kirafiki kwa ajili ya kujiweka sawa kabla ya ligi kuanza, na wamekusudia kuzifuatilia zaidi timu hizo ili wapate timu nzuri wakati timu zitakaposhiriki.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.