Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Wengi wateswa kwa kunyimwa haki

VATICAN CITY, Vatican

Imeelezwa kuwa watu wengi wamekuwa wakinyimwa haki ya matibabu, na haki ya kuishi.
Hayo yalisemwa na Baba Mtakatifu Fransisko wakati akizungumza baada ya Sala ya Malaika wa Bwana katika kuadhimisha Siku ya Wagonjwa Duniani.
Alisema kuwa kutokana na umaskini uliokithiri au kuteswa chini ya mabomu, katika mataifa ya Ukraine, Palestina, Myanmar na katika migogoro mingine, watu wengi wamekumbwa na matatizo.
Baba Mtakatifu alisema kuwa jamii inatakiwa kuwa karibu, na kuwa na huruma na wagonjwa au watu dhaifu, wakiwahudumia kwa upendo.
“Leo ametangazwa Mtakatifu María Antonia wa Amani wa Figueroa, Mtakatifu wa Argentina, tumpigie mikono Mtakatifu Mpya tunapoadhimisha kumbukumbu ya Bikira Maria wa Lourdes, sanjari na Siku ya Wagonjwa Ulimwenguni, ambayo mwaka huu inazingatia umuhimu wa uhusiano katika ugonjwa,” alisema Baba Mtakatifu, na kuongeza,
“Sote tunaitwa kuwa karibu na wale wanaoteseka, kuwatembelea wagonjwa, kama Yesu anavyotufundisha katika Injili. Hii ndiyo sababu leo nataka kueleza ukaribu wangu na ule wa Kanisa zima kwa wagonjwa wote, au watu dhaifu zaidi.
Baba Mtakatifu alisema kuwa jamii inatakiwa kutosahau mtindo wa Mungu wa ukaribu, huruma na upole, kwani haiwezi kupuuza ukweli kwamba kuna watu wengi walionyimwa haki ya kutunza, na haki ya kuishi.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.