Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Watanzania vinara mabao ya mapema NBC

AWESU AWESU AWESU AWESU

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Wachezaji saba wa Kitanzania wanaoshiriki Ligi Kuu soka Tanzania Bara wanaongoza kwa kufunga mabao ya mapema zaidi kuliko katika mechi za duru la kwanza za Ligi hiyo.
Ligi hiyo ya timu 16 tayari imemaliza raundi 15 za duru la kwanza hivi karibuni, na hivyo kuanza mechi za duru la pili la Ligi hiyo.
Nyota hao wazawa waliofunga mabao ya mapema katika mechi mbalimbali ni Mudathir Yahaya(Yanga), Sospeter Bajana(Azam FC), Yassin Mgaza(Dodoma Jiji), Awesu Awesu (KMC), Ibrahim Ajib (Coastal Union), Zidane Sereri(Dodoma Jiji) na Feisal Salum(Azam FC).
Mudathir Yahaya wa Yanga ndiye anayeongoza kwa kufunga bao la mapema zaidi kuliko wengine baada ya kufunga bao katika sekunde ya 44 kwenye mchezo wa Februari 17 dhidi ya KMC ambapo Yanga ilishinda 3-0 kwenye dimba la Jamhuri mjini Morogoro.
Sospeter Bajana wa Azam FC anafuatia kwa kufunga bao la mapema katika sekunde ya 54 dhidi ya JKT Tanzania, ambapo Azam ilishinda 2-1 siku ya Desemba 11 mwaka jana kwenye uwanja wa Azam Complex.
Awesu Awesu wa KMC alifunga bao katika dakika ya kwanza na sekunde 33 kwenye mchezo dhidi ya Mashujaa FC katika dimba la Uhuru jijini Dar es salaam, ambapo KMC ilishinda mabao 3-2 Desemba pili mwaka jana.
Ibrahim Ajib aliifungia Coastal Union bao la mapema kwa njia ya penati katika dakika ya kwanza na sekunde 42 na kuipa pointi zote tatu timu yake baada ya mchezo kumalizika kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Dodoma Jiji kwenye dimba la Mkwakwani jijini Tanga.
Penati hiyo pia imekuwa ya mapema zaidi kutokea kwenye Ligi hadi sasa, baada ya kutokea katika sekunde ya 15 tu, kabla ya Ajib kufunga kwenye dakika ya kwanza.
Mchezaji Yassin Mgaza wa Dodoma Jiji alifunga bao katika dakika ya kwanza na sekunde 55 wakati walipocheza na wenyeji Tabora United kwenye dimba la Ali Hassan Mwinyi, mjini Tabora ambapo hata hivyo Dodoma ilipoteza mchezo huo kwa kufungwa 2-1.
Kiungo wa Dodoma jiji Zidane Sereri pia alifunga bao la mapema katika dakika ya pili dhidi ya KMC, huku Feisal Salum wa Azam FC akifunga bao katika dakika ya 3 dhidi ya Tabora United.
Kwa upande wa wachezaji wa kigeni waliofunga mabao ya mapema ni Zozuzoua Pacome na Kennedy Musonda, wote kutoka Yanga waliofunga katika dakika ya 3 kwenye mechi tofauti.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.