Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Vikundi mafunzo ya Sinodi vyazinduliwa

VATICAN CITY, Vatican
Baba Mtakatifu Fransisko amedinzua rasmi vikundi vya mafunzo ambavyo vitaratibiwa na Sekretarieti Kuu inayoshirikisha mabaraza yenye uwezo.
Kikao cha pili cha Sinodi kitafanyika kuanzia Oktoba 2 hadi 27 maka huu na kitatanguliwa na siku mbili za mafungo.
Sekretarieti kuu ya Sinodi imetaarifu kwamba Baba Mtakatifu Fransisko ameweka tarehe za kikao cha pili cha Mkutano Mkuu wa XVI utakaofanyika kuanzia Jumatano Oktoba 2 hadi Dominika  ya Oktoba 27 maka huu ili kuendeleza kazi ya Sinodi ya Kisinodi yenye kauli mbiu: “Kwa ajili ya Kanisa la Sinodi:ushirika, ushiriki na utume.”
Wakati huo huo kama taarifa hiyo, iyoandikwa kwa mkono (chirograph) kutoka kwa Papa pia ilichapishwa, ambayo itaanzisha vikundi vya mafunzo ili kuzama zaidi katika baadhi ya mada zilizoibuka katika kipindi kilichopita.
Vitaanzishwa vikundi kati ya Mabaraza ya Kipapa ya Curia Romana vyene uwezo na Sekretarieti Kuu ya Sinodi, ambayo itaratibu.
Katika barua ya mkono wake (chirograph), iliyowekwa kwa ushirikiano kati ya mabaraza ya Curia na Sekretarieti ya Sinodi, Papa Francisko anataja katiba ya Mtaguso wa Vatican, ya  hati ya Lumen Gentium ili kukumbuka kwamba Kanisa linaonesha uwepo wake, “katika Kristo, kwa njia fulani sakramenti, ambayo ni ishara na chombo cha ‘muungano wa karibu sana na Mungu na umoja wa jamii nzima ya binadamu’ na kwamba “inajidhihirisha kwa uwazi zaidi na uaminifu kwa ulimwengu katika tamaduni mbalimbali kama fumbo la ushirika wa kimisionari, Mwili mmoja, unaoshiriki katika Roho wake anayeufanya upya na kuuongoza katika kutangaza Injili kwa watu wote.”
Katika mwanga huu, katika katiba Mpya ya  Curia Romana ya  Praedicate Evangelium, tunasoma kwamba “maisha ya ushirika hulipatia Kanisa sura ya kisinodi. Hasa kusikiliza kwa pande zote na nguvu ya usawa katika kujiweka katika huduma ya utume wa watu wa Mungu kuhitimu kazi ya usaidizi wa Curia Romana kwa huduma ya Askofu wa Roma, ya mtu binafsi, maaskofu na Baraza la Maaskofu.
Ustadi wa kichungaji unaoutekeleza hupata madhumuni na ufanisi wao katika huduma ya ushirika wa kiaskofu na ushirika wa kikanisa katika muungano na chini ya uongozi wa Askofu wa Roma.
Tayari katika hati ya maandalizi ya “Kuelekea Oktoba 2024” ya Sekretarieti Kuu ya Sinodi, iliyochapishwa  mnamo tarehe 11 Desemba 2023, ilisisitizwa jinsi mkutano ujao ungezingatia mada ya ushiriki, kuhusiana na utekelezaji wa mamlaka, kama usemi wa ushirika katika huduma ya utume. Kwa hiyo  yangechunguza jinsi ya kuishi sinodi katika ngazi zote za Kanisa.
Sasa uamuzi wa Papa unaweka wazi kwamba baadhi ya dhamira muhimu zaidi zilizoibuka kutokana na kusikiliza Makanisa zinahitaji muda mwingi kwa ajili ya mafunzo ya kitaalimungu, kanuni na kichungaji kadiri ya utaratibu wa sinodi inayohusisha wataalam kutoka mabara yote na mbaraza ya Curia Roman kulingana na uwezo wao.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.